Kwa hili lililojitokeza la tengua pangua wananchi wa Mwanza tutakukumbuka sana CP Makalla kwa muda mfupi umeonyesha weledi na umakini wa kushughulikia miradi ya hapa Mwanza ie uwanja wa ndege, meli, soko kuu, timu ya Pamba, madarasa, Daraja la JPM nk kwa kweli ninakumbuka maneno ya Mbunge...
Nimefuatilia kwa umakini hafla ya kusaini mkataba wa ujenzi wa jengo la abiria Mwanza linalokusudia kuifanya Mwanza Airport kuwa International ifikapo desemba 2024 by ICAO standards.
Kwenye maelezo ya Bw Mbura DG jengo hili litabeba watu 200 kutoka nje ya nchi(international pax)kwa mkupuo...
Mimi kama mwananchi Nimekuwa nikifuatilia kwa umakini uboreshaji wa jengo la Abiria la Uwanja wa ndege Mwanza.
Cha kushangaza ahadi na maelezo matamu yamekuwa yakitolewa kila mara kuwa mkataba na kazi itaanza hivi karibuni, lakini imekuwa ni maneno tu bila vitendo mnakwama wapi kiasi cha...
Sisi wazalendo tunakerwa sana na uzembe wa TAA kuanza ujenzi wa jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza, wameahidi mara kadhaa kwa Mkuu wa Mkoa, kuwa pesa imetolewa na Rais bilioni 30 sasa.
Kinachochelewesha ni nini? Songwe imeishakamilika, Tabora, Iringa, Tanga, Msalato, Arusha, Moshi vinajengwa...
Ni kweli suala la mchakato wa ujenzi wa jengo la abiria uwanja wa ndege Mwanza limechukua muda mrefu na sasa wananchi waliahidiwa Mwezi February 2024 mkataba ungesainiwa hapahapa Mwanza. Tuliamini baada ya TAA kukabidhiwa na mkoa kasi ingeongezeka na hususani baada ya Rais kutoa bn 30 kazi...
kiukweli Mzee Alhaji Ali Hassan Mwinyi aliongoza vizuri sana Zanzibar na baadaye Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kilichochangia Watanzania wawe na imani naye sana ni mageuzi ya kiuchumi na kijamii aliyoyafanya Zanzibar kwa kipindi kifupi wakati wa awamu yake na hivyo wananchi wengi hususani...
Mimi nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kinachoendelea kuhusu ziara za Makonda mikoani, na zoezi la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi. Kimsingi hali inafikirisha sana, na hapa Mwanasheria Mkuu wa serikali ameliona hili. Tuna wakuu wa Wilaya,wakuu wa mikoa , wabunge Takukuru nk wote kweli...
Akiwa Mwanza tarehe 30.1.2023 Rais na Amiri Jeshi Mkuu katoa maelekezo ya wazi ya kujenga jengo la abiria uwanja wa ndege na majokofu ya kuhifadhia samaki, nyama nk
Je, watendaji wakiwemo wakurugenzi, katibu mkuu na waziri wa uchukuzi Mbarawa hawatamwangusha Rais na kumchafua kanda ya ziwa...
Leo nimemsikiliza Musukuma akizungumzia kuchelewesha kuhusu jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza na miundo mbinu yake kuufanya uwe wa kimataifa.
Hali hii kwa sasa inatoa picha kama alivyosema Msukuma dharau kwa kanda ya ziwa haijalishi Makonda ni Mwenezi au Dotto ni Naibu Waziri Mkuu,kisiasa...
Ni kipindi cha miaka karibu 23 hivi tathmini ya kwa ajili ya uhamisho wa Kipunguni imekuwa ikifanyika bila mafanikio, hivi karibuni imefanyika tena na Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akathibitisha kuwa malipo yako kwenye hatua za mwisho, mwezi wa nane yatafanyika.
Na kuwa hakuna mkutano...
Kuna nafasi ya udereva hotel ya Lahe Mwanza, mwombaji awe na sifa zifuatazo
Umri miaka 21-30
Awe na cheti cha Veta cha kuhitimu mafunzo ya udereva
Vyeti vya kundesha gari
Uwezo wa kuendesha gari safari ndefu.
Maombi yapelekwe kwa meneja wa hoteli kabla ya tarehe 10.7.2023 ukiambatanisha...
Leo nimemsikia RC Makala akitembelea jengo la uwanja wa ndege Mwanza nakutoa maelekezo kadhaa ya kukwamua mradi huu, kitu kikubwa alichokieleza ambacho anapaswa akifanyie kazi ni kukabidhi jengo hili TAA bila hata masharti yeyote.
Masharti ya kupewa asilimia halmashauri eti kwa vile...
Mimi nianze kwa kumpongeza mbuge wa nyamagana na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa mwanza bw adam malima kwa kusemea kwa nguvu kubwa ukamilishaji wa uwanja wa ndege wa mwanza, jengo la abiria na miundo mbinu yake.
Suala la uwanja wa ndege ni la muda mrefu sana kila mara hupigwa chenga,hata bajeti ya...
Ninauza shamba kubwa hekta 18 zilizopimwa karibu na ziwa huku Mwanza jamani nipeni maarifa namna ya kupata wateja linafaa kwa hoteli,kilimo,mifugo na apartments. Nipeni maarifa. 0622290094
Eneo kubwa heka 18 za ardhi kandokando ya ziwa viktoria lenye mifugo, vizimbwi vya samaki,malambo linauzwa kwa usd 300000 piga simu 0739290084 au 0622290084. Bei inaweza kupungua. Ni zuri kwa hotel,apartment,mifugo,kilimo nk.
Pamoja na jitihada kubwa ya awamu ya sita kukamilisha miradi mbalimbali ipo miradi kadhaa km uwanja wa ndege Bukoba, Mwanza, baadhi ya barabara Jiji la Dar,Mbeya jijini, Mwanza nk ebu tuitambue kumsaidia Rais kuijua ili mambo yaende. Mwenye orodha yake aitaje.
Mhesh Rais Samia ni wakati wa kuingilia suala la malipo ya fidia kwa wananchi wanaohamishwa eneo la Kipunguni na Kigilagila ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa JNIA.
Ni miaka zaidi ya 15 sasa malipo haya yanasuasua mbali na tahmini ya mali zilizomo kwenye eneo hilo kufanyika miaka ya 90...
Nimetafakari kwa kina kuhusu kukatika kwa umeme maeneo mengi nchini na ukosefu wa maji si jambo la kuleta siasa na matumaini ya kwamba umeme utakuwa vizuri 2025. Hii si sawa, umeme ni uti wa mgongo wa uchumi kuanzia viwanda, usafirishaji, biashara ndogo ndogo,mahoteli, madini, mahospitali...
Mimi ni mdau wa maendeleo nchini nimesoma mijadala kuhusu ujenzi wa jengo la abiria uwanja wa ndege mwanza ninakubaliana na wale wanaosema halina viwango vya kimataifa, na wala haliwezi kutumika kwa abiria wa kimataifa na au kuidhinishwa na taasisi zinazosimamia ubora wa viwanja duniani...
Hivi ujenzi wa jengo la abiria uwanja wa ndege wa Mwanza kuna nini?
Je, linakwamishwa na maslahi binafsi au kuna mkono wa mtu unazuia lisimaliziwa kwa viwango. Juzi Mkuu wa Mkoa Adam Malima amefoka sana kuhusu mikingamo ya ujenzi wa jengo hili.
Kwanini Serikali kuu isilichukue na kulimalizia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.