JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums
Mdau wa JamiiForums analalamika kuwa alitumia dawa za kutibu Ugonjwa wa Malaria zinazoitwa EKELFIN ambazo baadaye zilimsababishia kupatwa na mchubuko sehemu za siri na midomoni. Anashangaa kwanini Serikali haitoi taarifa kwa watumiaji juu ya madhara ya dawa hizi kwa binadamu. Ni kweli kuwa dawa hizi zinaweza kusababisha athari tajwa?
JamiiCheck ni Moja kati ya Majukwaa yanayopatikana ndani ya tovuti ya JamiiForums.com. Jukwaa hili limewekwa mahsusi kwa ajili ya kufanya uhakiki, kutafuta uthibitisho au uhalisia wa habari, taarifa, matukio, picha au video mbalimbali zinazojitokeza au kuibuka kutoka katika vyanzo mbalimbali ndani na nje ya mtandao. Tofauti na Majukwaa na vyombo vingine vya kuhakiki ukweli wa habari, JamiiCheck ni Jukwaa pekee linalotoa fursa kwa watumiaji wake (Wanachama wa JamiiForums.com) kushiriki katika uhakiki kwa kuleta taarifa, picha au Video mbalimbali ambazo wanahitaji kuzichunguza kupata ukweli au chanzo chake pamoja na kuchangia/ kutoa maoni kwenye taarifa nyingine zilizohakikiwa. Ikiwa utakutana na habari au taarifa yoyote inayokutatiza...
Leo wakati nimepanda bajaj ya kushea, deree katika moja na mbili akasimulia kuwa mtaani kwao alikamatwa mwizi, kwa kuwa wamekuwa wakisumbuliwa sana bila mamlaka ya usalama wa raia na mali zao kuwajibika ipasavyo, walichukua hatua hatu ya kumpa adhabu mbadala. Adhabu yenyewe ni kwamba anabebwa na watu wanne halafu anachekechwa kwa muda mrefu, wakijiridhisha wanamwambia aende zake akapumzike. Akasema kitendo cha kuchekechwa kinapelekea viungo kuachana na kuvurugana humo ndani hivyo hupelekea kifo chake. Swali langu kwa team ya JamiiCheck, je hili suala linaweza kuwa kweli au ni kamba tu za walimwengu? Hivi inawezekanaje mtu utikiswe halafu viungo ndani viachan achane?
Wakati wa uchaguzi, baadhi ya watu hutengeneza taarifa za uongo au kuficha ukweli kuhusu historia ya mgombea fulani ili kuathiri taswira yake kwa umma. Taarifa hizo zinaweza kuwa mwaka wa kuzaliwa, historia ya uraia wake, au elimu yake. Mathalani, mtu au kundi la watu linaweza kusambaza taarifa za uwongo kuhusu umri wa mgombea kuonesha kama ni mdogo au mkongwe zaidi kuliko uhalisia, ikitegemea jinsi umri unavyoweza kuathiri jinsi watu wanavyomwona mgombea. Vilevile, historia ya uraia au elimu ya mgombea inaweza kupotoshwa ili kujenga mazingira ya kumsafisha au kumharibia katika uchaguzi husika. Mfano, kwenye uchaguzi wa Marekani mwaka 2018 historia ya Barack Obama ilipotoshwa kwa watu kumzushia kuwa asili ya Obama ni Kenya taarifa...
Nimeona taarifa mtandaoni ikisema watumishi wa Umma na Binafsi ambao wamechangia kwa zaidi ya miezi 108 yaani miaka 9 katika NSSF au PSSSF sasa rukhsa kutumia michango yao kama dhamana ya kuchukulia mkopo wa kujenga, kuboresha au kununua nyumba nchini Tanzania. Kanuni namba 141 za Mwaka 2024 zimeanza kazi tangu Machi 8, 2024. JamiiCheck tusaidieni kujua ukweli wake.
Leo nimesoma mtandaoni kuwa Vidonda vya tumbo(Ulcers) huweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Naomba kujua kama ni kweli maana siku zote mie najua vidonda vya tumbo huvipata mtu kutokana na mtindo wake wa maisha(kutokula) au kwa kutumia baadhi ya dawa ambazo zinaweza kuchubua utumbo. Sasa hii ya kuambukiza kwangu imekuwa mpya sana, tena mwandishi alifafanua zaidi kuwa eti iwapo mwenza wako ana ulcers basi uwezekano wa wewe kuupata ni mkubwa maana anaweza kukuambukiza.
Nani asiyemjua mbabe Simba mfalme wa nyika? Yaani ukutane naye paaah! Utamzame machoni aone aibu na kuondoka? Bado siamini hili jambo naona hawa vijana wa ovyo wanataka kuniingiza chaka siku nikikutana naye mbashara nisichukue njia nyingine za kujiokoa eti nimtizame. Hivi kweli Simba huyu kweli wa kumwonea aibu binadamu kisa kumuangalia machoni ana kwa ana kwa ujasiri. Wakuu naombeni taarifa sahihi kuhusu hili jambo, huenda mada ikawa kichekesho lakini hili jambo linasemwa sana mtaani.
Alhamisi ya pili ya Mwezi Machi kila mwaka, Dunia huadhimisha Siku ya Figo Duniani ili kutoa ufahamu na kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa afya ya figo na magonjwa yanayohusiana na figo. Kupitia maadhimisho haya, watu hupata fursa ya kujifunza kuhusu njia za kuzuia magonjwa ya figo, kudhibiti magonjwa ya figo, na umuhimu wa kuwa na maisha yenye afya ya figo. Aidha, maadhimisho haya huchangia katika kuongeza uelewa wa umma kuhusu haja ya kuchangia katika juhudi za kuzuia na kutibu magonjwa ya figo, pamoja na kusaidia watu wenye matatizo ya figo kupata msaada unaohitajika. Hata hivyo, ugonjwa huu huambatana na dhana nyingi potofu zinazofifisha kasi ya kupambana nao hivyo JamiiCheck imekuandalia ufafanuzi wa Dhana hizo kama sehemu ya...
Mzee Mwinyi alijiuzulu Uwaziri Mambo ya Ndani mwaka 1977 na Nafasi yake kuchukuliwa na Mzee Natepe. Natepe alipoingia tu ofisini alimtaka Waziri Mzee Mwinyi kutoka katika nyumba ya Waziri arudi kwao Zanzibar ili yeye aweze kuishi hapo kama Waziri. Ilikuwa shida kidogo maana Mzee Mwinyi bado alikuwa anatafuta makazi lakini alitakiwa haraka kutoka. Nasikia Mzee Mwinyi ilibidi atoke hivyo hivyo bila kujiandaa lakini siku anatoka pale nyumbani alizuiwa na Mzee Natepe kuchukua mabati na mifuko ya simenti aliyokuwa amenunua kwa pesa zake mwenyewe kwa ajili ya ujenzi wa nyumba binafsi. Natepe alimkatalia kuvichukua akidai ni mali ya Serikali. Kweli Mzee Mwinyi akaviacha akaondoka. Baada ya miaka kadhaa tu Mzee Mwinyi akateuliwa kuwa Rais wa...
Zipo imani na madai ya mbalimbali ya kijamii yanayobainisha namna ambavyo mama anaweza kumdhoofisha (kumbemenda) mtoto wake baadhi ya madai hayo ni: 1. Baba na Mama hawapaswi kujamiiana wakati kipindi cha unyonyeshaji kwa sababu kufanya hivyo hupelekea mtoto wao kudhoofika (kumbemendwa). 2. Lazima mama aoge ajioshe na sabuni kwanza baada ya kujamiiana ndipo amnyonyeshe mtoto wake ili asimbemende. 3. Mama akipata ujauzito wakati bado ananyonyesha anaweza kumbemenda mtoto wake. 4. Mzazi akijamiiana nje ya ndoa akishiriki tena tendo na mwanamke wake anayenyonyesha anambemenda mtoto.
Shirika la habari la AFP wakiwa wanatoa mafunzo mtandaoni wamebainisha namna upotoshaji wakati wa Uchaguzi unaweza kutokea kwa Mgombea, Chama pamoja na Mfumo. Wanaeleza, Upotoshaji kwa Mgombea hulenga kutoa taarifa zisizo sahihi kuhusu Mgombea fulani. Upotoshaji wa Chama cha Siasa hukusudia kutoa taarifa za uongo kuhusu chama fulani cha siasa kinachoshiriki uchaguzi. Aidha, Upotoshaji unaohusu mfumo wa Uchaguzi hulenga kutoa taarifa za uongo zinazoathiri zoezi la upigaji kura na utangazi matokeo ya Uchaguzi. Aina zote hizo za upotoshaji hulenga kuharibu au kutengeneza upande fulani wa chama cha Siasa ili kiweze kunufaika au kuathirika na Uchaguzi unaoendelea
Uhakiki wa Picha kwa kutumia Google Image Search ni njia muhimu ya kubaini asili au maelezo zaidi kuhusu picha fulani. JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha 1. Tembelea Google Image Search Fungua kivinjari chako na nenda kwenye ukurasa wa Google. Bonyeza kwenye sehemu ya 'Images' au 'Picha' kwenye ukurasa wa kwanza wa Google, au ingiza 'Google Image Search' moja kwa moja kwenye sanduku la utafutaji wa Kifaa chako 2. Ingiza Picha Kuna njia kadhaa za kuingiza picha kwenye Google Image Search: Bonyeza kitufe cha kamera kilichopo kwenye sanduku la utafutaji ili kuwezesha utafutaji wa picha kwa kutumia kamera. Kama picha unayo kwenye kifaa chako, unaweza kuiweka moja...
Mara nyingi nikiwa na stress na kupelekea kukosa usingizi, huwa navuta sigara ili kupunguza stress hizo. Hata iwe usiku wa manane nitajitahidi niende kwenye Club zinazokesha nikafuate sigara. Suala la kuwa inanisaidia au lah, sidhani lakini pale napokuwa navuta huwa nakuwa katika hisia nyingine kabisa. Chanzo cha kutumia sigara kama relief ya stress, ni baada ya kuona kwenye muvi mara kwa mara, na ushauri kutoka kwa marafiki. Nachotaka kujua kitaalam ni kama kweli sigara inasaidia kupambana na msongo wa mawazo tunaokumbana nao mara kwa mara.
Baada ya Afrika, bara la Amerika Kusini ndilo lenye watu weusi wengi zaidi wakikadiriwa kuwa zaidi ya milioni 170 huku Brazil ikiongoza ikiwa na watu weusi takriban milioni 120. Nchi ya Argentina inatajwa kuwa mpaka sasa watu weusi ni chini ya laki mbili wakiwa takriban asilimia 0.5% kutoka asilimia 48% miaka ya 1800. Inadaiwa watu weusi baada ya kuisaidia Argentina kupigana vita na maadui zake, watu weusi waliosalia waliwekwa kwenye maeneo maalumu ambayo kwa kipindi hicho kulikuwa na ugonjwa wa hatari unaosababishwa na bacteria “Plague” ambapo serikali iliwanyimwa huduma muhimu hivyo upelekea vifo vyao. Zitto kupitia ukurasa wake wa Twiiter aliwahi kumhoji jamaa kuhusu kuishabikia Argentina, nanukuu 'Una support argentina ambayo...
Kumekuwepo na barua inayiosambaa Mtandaoni ikionesha kuandikwa na Mfalme Mswati III ametoa tangazo linalodai kuwa kutokana na uhaba wa Wanaume kwenye nchi yake, amewaomba wananchi wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara kuomba uraia kwenye nchi yake, na kila mwanaume atayeoa walau wanakwake 5 atamlipia gharama za harusi zao pamoja na kuwanunulia nyumba. Ukweli wa taarifa hii upoje?
Katika pitapita mitandaoni nimekutana na huyu chawa wa Mtoto wa Rais Museveni, Kainerugaba Muhoozi akimtuhumu Kakwenza Rukira kuingia makubaliano ya siri na umoja wa Ulaya nchini Uganda katika kuhamasisha ushoga nchini humo. Nakumbuka Uganda imezuia mahusiano ya jinsia moja na Rais Museveni amebana kweli kweli wazungu hawana pa kupumulia, naona wameamua kupitia njia za panya kuleta ushenzi wao.
TinEye ni nyenzo nzuri ya kutafuta picha kwenye wavuti ambayo inaweza kutumiwa kufanya uhakiki wa Picha. JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha. 1. Fungua Kivinjari Chako Anza kwa kufungua kivinjari chako kwenye kifaa chako cha mkononi au kompyuta. 2. Tembelea Tovuti ya TinEye Ingiza 'TinEye' kwenye sanduku la utaftaji la kivinjari chako na bonyeza kwenye matokeo yanayofanana na tovuti rasmi ya TinEye. 3. Pakia Picha Kuna njia mbili za kupakia picha kwenye tovuti ya TinEye Bofya kwenye kitufe cha 'Pakia Picha' au "Upload' kisha pakia picha unayotaka kufanya uhakiki. Ikiwa picha tayari iko kwenye wavuti, unaweza kunakili URL (Link) ya picha hiyo na kuibandika...
Back
Top Bottom