Jamii Check

Jukwaa maalum la wananchi kushiriki mchakato wa kuthibitisha taarifa wanazokutana nazo mtandaoni au nje ya mtandao
Mdau wa JamiiForums analalamika kuwa alitumia dawa za kutibu Ugonjwa wa Malaria zinazoitwa EKELFIN ambazo baadaye zilimsababishia kupatwa na mchubuko sehemu za siri na midomoni. Anashangaa kwanini Serikali haitoi taarifa kwa watumiaji juu ya madhara ya dawa hizi kwa binadamu. Ni kweli kuwa dawa hizi zinaweza kusababisha athari tajwa?
Nadhani wengi tumetizama movie ya Titanic, ikielezea penzi la vijana wawili na pia kuzama kwa meli hiyo. Inasemekana ina uhalisia kiasi fulani na tukio la kweli la kuzama kwa meli hiyo mwaka 1912. Jambo la kutafakarisha, imekuwa ikidaiwa kuwa aliyekuwa kapteni mkuu wa Meli hiyo Edward John Smith kabla ya kung'oa nanga alisikika akisema kuwa ''Hata Mungu Mwenyewe asingeweza kuzamisha hii meli'' - ( "Even God himself couldn't sink this ship") Kauli hiyo inayodaiwa kutamkwa na Kapteni wa TITANIC, imetafsiriwa na wengi kama chukizo kubwa kwa Mwenyezi Mungu hivyo kupelekea kuwaadhibu maelfu ya watu waliokuwa kwenye meli hiyo. Edward John Smith Meli ya Titanic
Tanzania yasaini mikataba minne na Falme za Kiarabu ndani ya mwaka mmoja. 1. Kuendeleza uwanja wa ndege wa KIA 2. Ushirikiano na Posta Tanzania 3. Kuendeleza misitu yote nchini na TFS 4. DP World na TPA
Wakuu kwema? Katika pitapita zangu mtaani nimesikia barabara ya Njombe - Songea imejengwa na Malkia wa Uingereza na kwamba Hayati Queen Elizabeth II ndiye mmiliki wa mashamba ya chai maeneo hayo. Ila kubwa zaidi ni kuwa, Njombe kuna kijiiji kizima ambacho ni mali ya Malkia huyo. Je, hili lina ukweli ndugu zangu?
Wote mnaweza kufikiria ni namna gani mtu asiye mkazi au mfanyakazi au mwenye appointment kwenye makazi rasmi ya Malkia wa Uingereza angeweza kupenya bila kuonekana, akafanikiwa kuingia ndani ya jumba hilo, akapiga misele kidogo, akaingia ofisi ya Malkia Elizabeth kufyonza mvinyo maalum wa Malkia, na mwisho wa siku akazama ndichi kwenye hiyo room ya Malkia na kumkuta Malkia akiwa katikati ya njozi tamu, akaketi pembeni yake na kumsubiri Malkia aamke ili wayajenge/wapeane maelekezo. Basi kunaye dogo mmoja alileta makwaru na kufankiwa mpaka Malkia mwenye alipomsanukisha. Inadaiwa tukio hilo lilisababisha ulinzi zaidi uimarishwe na baadhi ya walinzi walifukuzwa.
Hii dunia ina vitu vya ajabu sana na vya kushangaza. Kuna historia baadhi unaweza unaweza kushangazwa nazo mojawapo ikiwa hii niliyopata kusimuliwa. Msitu wa Nyumbanitu una historia nyingi za kushangaza. Msitu huu upo katika Wilaya ya Wanging'ombe mkoa wa Njombe. Msitu huu nimepata kusimuliwa kuwa endapo mwanamke atakuwa kwenye siku zake basi hatoruhusiwa kuingia katika msitu huo, Ikiwa atakaidi basi akiingia kwenye huo msitu ndio utakuwa mwisho wake wa kuonekana maana atapotea mazima. Nadhani hili jambo mnaona linavyostaajibisha. Najiuliza huu msitu una nguvu na miujiza gani mpaka uweze kuwatendea hivyo dada zetu.
Kevin Carter alikuwa ni mpiga picha, sasa katika kazi zake alifanikiwa kufika Sudan na alikuta eneo fulani nchini Sudan likikabiliwa na njaa kali sana. Wakati anaendelea kuchukua matukio katika picha, alikutana na mtoto dhoofu mwenye utapiamlo aliyekuwa akikabiliwa na njaa kali pamoja na kiu, cha kusikitisha zaidi nyuma ya mtoto huyo dhoofu kulikuwa na ndege hatari aina ya TAI akimuwinda huyo mtoto ili kujipatia kitoweo. Inadaiwa Kevin Carter alipiga picha na kusepa. Inasemekana huko nyuma mtoto yule kutokana na kuwa dhoofu aliweza kuuawa kirahisi na TAI yule. Inasemekana picha ile ya Kevin Carter ilipata umaarufu sana mpaka kupata tuzo ya Pulitzer iliyoanzishwa na Joseph Pulitzer. Inadaiwa Kevin Carter umaarufu aliopata...
VVU/UKIMWI vinasalia kuwa janga kuu la afya ya Umma duniani, janga lililogunduliwa zaidi ya miaka 40 iliyopita likiwa limechukua uhai wa watu zaidi ya milioni 40.4 huku maambukizi yakiendelea katika nchi zote duniani. Hadi kufukia mwishoni mwa mwaka 2022, kulikuwa na wastani wa watu milioni 39.0 wanaoishi na VVU, theluthi mbili kati yao (milioni 25.6) wakipatikana barani Afrika. Pia, mwaka 2022 pekee, watu 630 000 walipoteza maisha kutokana na sababu zinazohusiana na VVU na watu milioni 1.3 walipata VVU.
Ingawa ni kama utani na inachekesha ila huwezi amini kuwa ng'ombe akijamba/kutoa ushuzi basi kile kitokacho huambatana na gesi ya methane ambayo huzalisha joto na moto/mwanga. Wanaharakati mbalimbali wa mazingira wamekuwa wakidiscourage ufugaji/uzalishaji wa ng'ombe kwa wingi na kusema wazi kuwa ushuzi wa ng'ombe huleta mabadiliko ya hali ya hewa, kwa sababu ng'ombe hutoa methane, gesi chafu inayohusishwa na ongezeko la joto duniani. Ng'ombe akiwa anajamba, ukiwasha njiti ya kiberiti moto unawaka kutokana na gesi ya methane. Ningependa kujua ukweli wa hili jambo.
Inadaiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi, amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kusitisha mkutano wake uliopangwa kufanyika kesho Julai 23,huko Buriaga, Temeke jijini Dar es Salaam. Barua inayodaiwa kuandikwa na Sisty Nyahoza, Naibu Msajili wa vyama.
Huu Muungano ni chenga kabisa una kero nyingi mno, naona kwa Zanzibar wao ni raha kwenda mbele. Sisi wote ni Watanzania lakini ajabu Mtanganyika akienda Zanzibar endapo atahitaji kuendesha gari basi atatakiwa kuomba kibali maalum kinachotolewa na mamlaka za huko, vinginevyo utakuwa unavunja sheria. Hili suala halijakaa sawa kabisa, sawa na lile la kulipia kodi electronics kutoka Zanzibar, au Mzanzibar kumiliki ardhi Bara wakati Mtanganyika anawekewa vikwazo mfululu kumiliki ardhi Zanzibar. Huu Muungano ni wa kishenzi sana.
Habari Wakuu, Hata hivyo kumekuwa na dhana kuwa mtu anayejichora tattoo hawezi kumchagia mtu damu na sababu za kutokufanya hivyo hazijawekwa bayana zikaeleweka Je, ni kweli kwamba mtu aliyechora tattoo hawezi kuchangia damu? Na kama ni kweli zipo ni sababu za kisayansi ya kushindwa kufanya hivyo?
Aprili 27, 2023, akaunti ya Mtandao wa Twitter inayotumia jina la MainLandAfrica iliweka chapisho linalodai kuwa Bilionea wa Marekani Dan Friedkin amekodisha takriban Ekari 6,000,000 za ardhi nchini Tanzania. Chapisho hilo lilienda mbali zaidi kwa kudai kuwa Friedkin ni mmiliki wa Ekari zingine 25,000 za ardhi zinazounda pori la Akiba la Mwiba. Wanaojua kuhusu huyu jamaa watupe details anafanya biashara gani na ardhi kubwa kiasi hicho?
Miaka kadhaa nyuma niliwahi kusikia mwanamke mmoja nchini Uganda kajifungua watoto wawili (mapacha) wenye baba tofauti, hali hii ilinishangaza sana. Hali kama hii iliripotiwa pia Septemba 9, 2022 kwenye jarida la CNBC ambapo mwanamama mmoja kutoka Minerois, Brazil alithibitika kuwa na ujauzito wa mapacha ambao baada ya kupimwa DNA zao ilibainika kuwa walikuwa wa baba tofauti. Kisayansi, ni kweli kuwa jambo hili linaweza kutokea? Kama jibu ni ndio, linatokeaje?
Kwa kawaida inafahamika kwamba ikitokea Waziri Mkuu amejiuzulu, na Baraza zima la Mawaziri linavunjwa. Swali langu ni kwamba, Ikiwa Waziri Mkuu atajiuzulu na wakati huo pakiwa na Naibu Waziri Mkuu, Je Baraza la Mawaziri litavunjwa ama halitovunjwa kwasababu tayari patakuwa na Naibu Waziri Mkuu?
Huyu ni Spika wa Bunge la Gabon alipokuwa anataka kutoroka leo hii asubuhi, Agosti 31, 2023. Ukiona viongozi tuliowaamini wanasaini mkataba mbovu kama DPW ujue nyuma yake kuna mambo kama haya! Video inayodaiwa kumuonesha Spika wa Bunge akiwa amekamatwa na Mabegi ya fedha akitoroka
Kijana wa miaka 29 aliushangaza ulimwengu kwa kitendo cha kikatili kisichokuwa na chembe ya utu. Inadaiwa baada ya kumpindua na kumuua Rais aliyekuwa madarakani William Tolbert, Samuel Doe alihakikisha anamaliza mizizi ya mtangulizi wake kwa kuua viongozi wote waandamizi. Inadaiwa Aprili 22, 1980 viongozi 13 walifikishwa ufukweni mwa bahari ya Atlantic nchini humo, wanaume hao 13 walikuwa nusu uchi ambapo walifyatuliwa risasi na vikosi vya Rais Samuel Doe. Kati ya waliouawa ni pamoja na Frank E. Tolbert ambaye alikuwa Kaka yake na rais Tolbert, na Rais wa Bunge la seneti. Picha: hali ilivyokuwa siku ya mauaji Muosha huoshwa, Rais Samuel Doe naye alikuja kupinduliwa na kuuawa kikatili sana na waasi.
Je ni imani za kweli kuwa kitovu cha mtoto mchanga kikiangukia uume huyo mtoto atakua hasimamishi? Wajuvi wa mambo tunaomba mtusaidie.
Mzee Mwinyi alijiuzulu Uwaziri Mambo ya Ndani mwaka 1977 na Nafasi yake kuchukuliwa na Mzee Natepe. Natepe alipoingia tu ofisini alimtaka Waziri Mzee Mwinyi kutoka katika nyumba ya Waziri arudi kwao Zanzibar ili yeye aweze kuishi hapo kama Waziri. Ilikuwa shida kidogo maana Mzee Mwinyi bado alikuwa anatafuta makazi lakini alitakiwa haraka kutoka. Nasikia Mzee Mwinyi ilibidi atoke hivyo hivyo bila kujiandaa lakini siku anatoka pale nyumbani alizuiwa na Mzee Natepe kuchukua mabati na mifuko ya simenti aliyokuwa amenunua kwa pesa zake mwenyewe kwa ajili ya ujenzi wa nyumba binafsi. Natepe alimkatalia kuvichukua akidai ni mali ya Serikali. Kweli Mzee Mwinyi akaviacha akaondoka. Baada ya miaka kadhaa tu Mzee Mwinyi akateuliwa kuwa Rais wa...
Kumekuwepo na madai yanayosambaa mtandaoni kuwa makasha ya dawa za meno huwa na rangi (code) za aina mbalimbali zinazofafanua aina ya kemikali zilizotumika kutengenezea dawa hiyo. Aidha, madai hayo yanafafanua zaidi kuwa kemikali husika ni hatari kwa afya na husababisha saratani, na kwamba makampuni yanayozalisha dawa hizi hayawezi kukupa siri hii. Ukweli wake upoje?
Back
Top Bottom