Kanda ya Ziwa tusikilizwe kuhusu uwanja wa ndege. Haivumiliki tena

dndagula

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
1,461
1,445
Leo nimemsikiliza Musukuma akizungumzia kuchelewesha kuhusu jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza na miundo mbinu yake kuufanya uwe wa kimataifa.

Hali hii kwa sasa inatoa picha kama alivyosema Msukuma dharau kwa kanda ya ziwa haijalishi Makonda ni Mwenezi au Dotto ni Naibu Waziri Mkuu,kisiasa haitatosha kuwashawishi wananchi ambao ni wazi wanaonekana kutengwa kupitia uwanja huu, Songwe umejengwa, Arusha, Tanga,Dodoma,Tabora, Kigoma lakini kwenye mpango wa sasa uwanja huu haumo.

Ni nani anayeupiga vita. Rais kwa hili tunaomba uingilie kati kwa jinsi utakavyoona inafaa. Aidha barabara njia nne za kuingia jijini zimetupiliwa mbali hakuna anayezungumzia kwenye Mpango. Nadhani miji kama Mwanza Mbeya ni wakati wa kujenga njia nne kama ilivyo kwa Dar.

Kura ziko nyingi sana kwenye maeneo haya siyo ya kufanyia mzaha. Makonda pata maelezo ya miradi hii uondoe lawama.
 
Kura ziko nyingi sana kwenye maeneo haya siyo ya kufanyia mzaha. Makonda pata maelezo ya miradi hii uondoe lawama.
Hizi tabia za kulia lia wanazipenda sana CCM, hasa hawa wahujumu wa nchi waliopo madarakani sasa hivi.

Unalia lia hapa leo, kesho unatupia kimfupa ulambe unasahau kila kitu kilicho kuwa kinakuliza.

Wewe unalilia uwanja wa ndege, ambao kwa kweli umechezewa sana toka hata enzi za Magufuli. Ule uwanja ulitakiwa kuwa umekamilika siku nyingi, hata kabla ya ule wa Kisumu.

Ni kweli pia, kwamba uwanja huo unapigwa vita, hasa na wale walioko mashariki, kama huo wa Arusha ulioutaja wewe.

Hawa akina Msukuma unaowataja humo, ni mapambo tu hayo. Umeona mwenyewe swala la IGA ya DP World na mambo mengi mengine. Hao ndio malaya wa kisiasa aliowahi kuwazungumzia Mwalimu enzi zile.

Kanda ya Ziwa, sasa labda mtazameni kwa makini Luhaga Mpina, vinginevyo sioni chochote huko, na mtaendelea kulia sana kama majuha.
 
Acheni kuifundisha serikali majukumu yake,wananchi hamtakiwi kuwa watu wa maneno maneno bali vitendo hakuna mabadiriko yanapatikana kwa maneno maneno.. kama mkiamua jambo fulani hamlitaki na mkaandamana kwa umoja na uwingi pasipo kukata tamaa jambo lenu litapita tu

Viongozi wabishi na wasiojitambua mtawatoa kwenye sanduku la kura na hata kama mtahitaji mabadiliko kikatiba,utawala,Sheria ama mtu fulani awajibishwe hamtashindwa nguvu yenu ikiwa Moja kwa uwingi wenu hakuna litashindikana.

Swala la kura litaonekana kama halina nafasi ktk mageuzi mnayoyataka hiyo nikwasababu wananchi husika mmetaka iwe hivyo,lkn mkitaka kura yenu iwe na nguvu hamshindwi ni maarifa kidogo tu yanahutajika ktk Kila kichwa cha mtanzania basi nchi inabadilika nakuwa nchi ya ahadi yenye asali na maziwa.
 
Tutaendelea kupiga kelele kwa vile tumegundua Uwanja huu unapigwa vita. Hili ni eneo CCM wanaweza kucheza nalo na hata Rais kuacha legacy. Je wabunge kanda ya ziwa mko wapi. Wakuu wa mikoa wanne wamehangaika nao lakini hamna kitu. siasa na propoganda tu. pia Niliona Msukuma akiwasema wabunge kuwa wanapiga makofi tu. nashangaa hata akina Luhanga Mpina naye kimya kulikoni?

Makonda haya ndiyo maeneo yaliyosahauliwa yanayoweza kukupa promo kanda ya ziwa.wakubwa wanapitia uwanja huu wanaona hali halisi chukueni hatua.Nimesikia kesi imefunguliwa kuhusu ubadhirifu wa pesa uwanja wa ndege wa Mwanza na wakili je kwenye uwanja huu tu au ni mbinu ya kuzidi kuuzorotesha ujenzi wake.wacha tuone mwisho wake.Mh Rais atie neno wanamharibia Mawaziri husika. Hapa kuna siasa.
 
Leo nimemsikiliza Musukuma akizungumzia kuchelewesha kuhusu jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza na miundo mbinu yake kuufanya uwe wa kimataifa.

Hali hii kwa sasa inatoa picha kama alivyosema Msukuma dharau kwa kanda ya ziwa haijalishi Makonda ni Mwenezi au Dotto ni Naibu Waziri Mkuu,kisiasa haitatosha kuwashawishi wananchi ambao ni wazi wanaonekana kutengwa kupitia uwanja huu, Songwe umejengwa, Arusha, Tanga,Dodoma,Tabora, Kigoma lakini kwenye mpango wa sasa uwanja huu haumo.

Ni nani anayeupiga vita. Rais kwa hili tunaomba uingilie kati kwa jinsi utakavyoona inafaa. Aidha barabara njia nne za kuingia jijini zimetupiliwa mbali hakuna anayezungumzia kwenye Mpango. Nadhani miji kama Mwanza Mbeya ni wakati wa kujenga njia nne kama ilivyo kwa Dar.

Kura ziko nyingi sana kwenye maeneo haya siyo ya kufanyia mzaha. Makonda pata maelezo ya miradi hii uondoe lawama.
Nyie mlishajengewa Chato na Shujaa wenu ,ndio mkautumie Sasa
 
Tutaendelea kupiga kelele kwa vile tumegundua Uwanja huu unapigwa vita. Hili ni eneo CCM wanaweza kucheza nalo na hata Rais kuacha legacy. Je wabunge kanda ya ziwa mko wapi. Wakuu wa mikoa wanne wamehangaika nao lakini hamna kitu. siasa na propoganda tu. pia Niliona Msukuma akiwasema wabunge kuwa wanapiga makofi tu. nashangaa hata akina Luhanga Mpina naye kimya kulikoni?

Makonda haya ndiyo maeneo yaliyosahauliwa yanayoweza kukupa promo kanda ya ziwa.wakubwa wanapitia uwanja huu wanaona hali halisi chukueni hatua.Nimesikia kesi imefunguliwa kuhusu ubadhirifu wa pesa uwanja wa ndege wa Mwanza na wakili je kwenye uwanja huu tu au ni mbinu ya kuzidi kuuzorotesha ujenzi wake.wacha tuone mwisho wake.Mh Rais atie neno wanamharibia Mawaziri husika. Hapa kuna siasa.
Mlishajengewa na shujaa wenu Chato msituchoshe.

Pili Samia hana roho mbaya saana ,amewaletea pesa mnapinga Kwa kujifanya Wasomi

View: https://twitter.com/Jambotv_/status/1722620029735510326?t=wwkTNy-b0TkvQJpKtSCHpw&s=19
 
Leo nimemsikiliza Musukuma akizungumzia kuchelewesha kuhusu jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza na miundo mbinu yake kuufanya uwe wa kimataifa.

Hali hii kwa sasa inatoa picha kama alivyosema Msukuma dharau kwa kanda ya ziwa haijalishi Makonda ni Mwenezi au Dotto ni Naibu Waziri Mkuu,kisiasa haitatosha kuwashawishi wananchi ambao ni wazi wanaonekana kutengwa kupitia uwanja huu, Songwe umejengwa, Arusha, Tanga,Dodoma,Tabora, Kigoma lakini kwenye mpango wa sasa uwanja huu haumo.

Ni nani anayeupiga vita. Rais kwa hili tunaomba uingilie kati kwa jinsi utakavyoona inafaa. Aidha barabara njia nne za kuingia jijini zimetupiliwa mbali hakuna anayezungumzia kwenye Mpango. Nadhani miji kama Mwanza Mbeya ni wakati wa kujenga njia nne kama ilivyo kwa Dar.

Kura ziko nyingi sana kwenye maeneo haya siyo ya kufanyia mzaha. Makonda pata maelezo ya miradi hii uondoe lawama.

View: https://twitter.com/Jambotv_/status/1722620029735510326?t=wwkTNy-b0TkvQJpKtSCHpw&s=19
 
Hali hii kwa sasa inatoa picha kama alivyosema Msukuma dharau kwa kanda ya ziwa haijalishi Makonda ni Mwenezi au Dotto ni Naibu Waziri Mkuu,kisiasa haitatosha kuwashawishi wananchi ambao ni wazi wanaonekana kutengwa kupitia uwanja huu, Songwe umejengwa, Arusha, Tanga,Dodoma,Tabora, Kigoma lakini kwenye mpango wa sasa uwanja huu haumo.

Hivi kwa uelewa wako unadhani ni kanda ipi nyingine ina uwanja wa kimataifa ambao jengo lake ni zuri labda mithili ya JKNIA?

Tafadhali kama hujawahi kufika Songwe usiutaje maana jengo lake ni kama jengo la sekondari, wala usitaje KIA sababu hata haifikii ule uwanja Terminal 2...
 
Hivi kwa uelewa wako unadhani ni kanda ipi nyingine ina uwanja wa kimataifa ambao jengo lake ni zuri labda mithili ya JKNIA?

Tafadhali kama hujawahi kufika Songwe usiutaje maana jengo lake ni kama jengo la sekondari, wala usitaje KIA sababu hata haifikii ule uwanja Terminal 2...
Na ule wa Chato?
 
Chadema wakuteua ngosha kuwa mgombea urais, wapiga kura wa CCM watakuwa ffu, tccm na nec.
 
Leo nimemsikiliza Musukuma akizungumzia kuchelewesha kuhusu jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza na miundo mbinu yake kuufanya uwe wa kimataifa.

Kura ziko nyingi sana kwenye maeneo haya siyo ya kufanyia mzaha. Makonda pata maelezo ya miradi hii uondoe lawama.
Siungi mkono hoja hii kwasababu uwanja wa ndege sio hitaji la walio wengi Mwanza. Usafiri wa ndege ni hitaji la few matajiri wachache wapanda ndege. Kanda ya Ziwa bado ni Kanda primitive, hivyo wananchi waliowengi bado wanatumia primitive means of transport, usafiri wetu mkuu kutembea kwa miguu vichochoroni, na barabarani, baada ya miguu ni baiskeli, boda boda, bajaji na magari. Kwa sasa Busisi barabara inakwenda kukamilika. Kwa wale wahitaji kuruka, zile ndege zetu za asili za kupaa zipo!.

Msitishie kuhusu kura 2025 ni kura bwelele!. Tayari tumepewa Doto Biteko huyo ndiye Waziri Mkuu ajaye, Makonda huyo anakuja kuingia Bungeni kuwa Waziri. Luhaga Mpina huyo kwa sasa anapiga sana kelele, soon atatupiwa fupa lenye bonge la nyama, atanyamaza!. 2025 kura zote Kanda ya Ziwa ni kule kule kwa siku zote!.
Mnataka tupewe nini tena wakati nchi yote ni yetu!.

P
 
Wakati tunashauri kujenga chato ni upotevu wa hela na tulisema zile hela mlizojengea chato mngeboresha uwanja wa Mwanza mlikuja na kauli za kibabe sana. Mlitudhihaki kwa maneno makali sana. Huu uwanja ulikuwepo na ulikuwa very strategic na tulisema sana juu ya hili.

Shida mnajiziba masikio mnatawaliwa na ukanda.

Uliona wapi katika nchi zetu za kimaskini hizi kukawa na International Airports 2 kwa utofauti wa 127km (Air line)??
 
Leo nimemsikiliza Musukuma akizungumzia kuchelewesha kuhusu jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza na miundo mbinu yake kuufanya uwe wa kimataifa.

Hali hii kwa sasa inatoa picha kama alivyosema Msukuma dharau kwa kanda ya ziwa haijalishi Makonda ni Mwenezi au Dotto ni Naibu Waziri Mkuu,kisiasa haitatosha kuwashawishi wananchi ambao ni wazi wanaonekana kutengwa kupitia uwanja huu, Songwe umejengwa, Arusha, Tanga,Dodoma,Tabora, Kigoma lakini kwenye mpango wa sasa uwanja huu haumo.

Ni nani anayeupiga vita. Rais kwa hili tunaomba uingilie kati kwa jinsi utakavyoona inafaa. Aidha barabara njia nne za kuingia jijini zimetupiliwa mbali hakuna anayezungumzia kwenye Mpango. Nadhani miji kama Mwanza Mbeya ni wakati wa kujenga njia nne kama ilivyo kwa Dar.

Kura ziko nyingi sana kwenye maeneo haya siyo ya kufanyia mzaha. Makonda pata maelezo ya miradi hii uondoe lawama.
WASUKUMA KWA UKABILA HAMJAMBO
 
Back
Top Bottom