Mimi nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kinachoendelea kuhusu ziara za Makonda mikoani, na zoezi la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi. Kimsingi hali inafikirisha sana, na hapa Mwanasheria Mkuu wa serikali ameliona hili. Tuna wakuu wa Wilaya,wakuu wa mikoa , wabunge Takukuru nk wote kweli wameshindwa kutatua kero mpaka Makonda aje huko. Hii ni aibu kwa serikali. kiukweli wana mwangusha Rais kiaina.Mwenezi hawezi kumaliza kero zote zaidi ni asilimia 0.1 %ya kero zilizopo kwenye jamii.Njia nzuri ni kila mtendaji aliyeteuliwa na Rais atimize wajibu wake au mifumo rasmi itumike.vinginevyo watamchukia bure Makonda kuwa anawafitinisha lakini utaratibu anaotumia utachokwa na yeye mwenyewe atachoka tu na hapo wananchi watazidi kuichukia serikali yao. utataribu huu ni temporary tu kisiasa.