📍HECHE AITAKA SERIKALI KUHARAKISHA MCHAKATO WA MARIDHIANO NCHINI
Na Mwandishi Wetu
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Heche, ameitaka serikali kuharakisha mchakato wa maridhiano nchini, akisisitiza kuwa hatua hiyo ndiyo njia sahihi ya kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa.
Akizungumza leo katika mkutano uliofanyika katika Kata ya Kibamba, Heche amesema kuwa maridhiano ni msingi muhimu wa kujenga taifa lenye umoja na maendeleo endelevu.
Alieleza kuwa jamii haiwezi kusonga mbele ikiwa itaendelea kugubikwa na migawanyiko na misuguano ya kisiasa, hivyo ni wajibu wa serikali kuweka kipaumbele katika juhudi za kuleta maelewano miongoni mwa wananchi.
“Maridhiano ni njia sahihi ya kudumisha...