Ikiwa ni siku chache tangu chombo cha habari cha kimataifa cha BBC News kuchapisha makala iliyomhusu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, zimeendelea kusambaa taarifa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, ametoa kauli ya kutaka BBC Swahili ifungiwe kufanya kazi nchini Tanzania.
Chapisho hilo, ambalo limesambazwa kupitia Facebook, linaambatana na nukuu isemayo:
"Baada ya BBC Swahili kuchapisha video yenye habari ya Tundu Lissu kuhoji demokrasia ya Tanzania, Kikwete atoa tamko kuu kwa TCRA kuifungia BBC Swahili."
Hata hivyo, uchunguzi wa taarifa mbalimbali za umma, ikiwemo hotuba, mahojiano na taarifa rasmi zilizochapishwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete, haukubaini...