Kumekuwepo na ujumbe unaosambazwa kwenye mitandao , hususan WhatsApp, ukidai kuwa Umoja wa Mataifa (UN) ulitoa ripoti katika robo ya kwanza ya mwaka 2025 ikisema kuwa dunia ina watu bilioni 7.8, wakiwemo wanawake bilioni 5.6 na wanaume bilioni 2.2.
Ujumbe huo pia unadai kuwa UN iliwashauri wanawake kuwa makini katika mtazamo wao kuhusu wanaume, kwa sababu kati ya wanaume bilioni 2.2, bilioni moja tayari wameoa, milioni 130 wako gerezani na milioni 70 wana matatizo ya afya ya akili au magonjwa mbalimbali. Kwa mujibu wa ujumbe huo, baada ya kuwaondoa makundi hayo, kuna takriban wanaume bilioni moja pekee wanaopatikana kwa ajili ya ndoa.
Ujumbe huo unaendelea kudai kuwa kati ya wanaume hao bilioni moja, asilimia 56 hawana ajira, asilimia...