Jamani ni mimi peke yangu ndio naona hivyo?

Mikutano ya Lissu tofauti na mikutano ya Magufuli. Watu kwenye mikutano ya Lissu huenda kumpokea mgombea huyo kwa sherehe, shangwa, nderemo na fifijo.

Hakuna wasanii wengi na sijui wana wimbo mmoja tu,"Tundu Lisu wapeleke, mchakamchaka. Tundu Lisu wapeleke kikamada" wimbo huu mmoja tu watu wanaurudi hatari, wanapagawa hatari, wanasisimuka hatari, wanaserebuka hatari.

Sijui wimbo huo umerekodiwa au kuna mtu huwa anauimba lakini Furaha iliyopo huko CCM na wasanii wa nchi nzima na wa nje ya nchi hakuna. Watu wa CCM hata wakifurahi ni kama wanawafurahia wasanii tu, hata hao ni wanawashangaa tu.

Nasikia kuna sehemu umeme ulikatika, ilikuwa jioni sana, makutano wakaamua kumsindikiza Lissu hadi mahala salama, hebu fikiria umati ule unaingia Mjini wakimsindikiza mgombea wao, ni upendo ulioje.

Nasikia sehemu fulani watu walikua wakicheza Reggae, wimbo maarufu wa Bob Marley, One Love. waliucheza wimbo huu pamoja na Lissu, ni furaha iliyoje?

Kuna ujumbe mkubwa sana kwenye mikutano ya Lissu. Lissu katengwa na kila huduma anazostahili kama kuoneshwa na TV au Redio au Magazeti ya Taifa, lakini anafarijiwa na wanyonge wenzie, tena furaha halisi itokayo ndani ya nyumba vya mioyo ya wapigakura wake.

Furaha, upendo na hamasa waliyonayo watu wa Lissu sio ya kulazimisha, ni furaha halisi.

Nakumbuka ni hawahawa walimchangia alipopigwa,walimsalia apone, walisoma al badir ili watesi wake wapate adhabu ya Mungu, waliwachangia Viongozi wa Chadema walipowekwa ndani, walimchangia damu, walijitokeza kwa wingi kwenda Uwanja wa ndege kumpokea bila kujali vitisho vya Polisi na sasa wanaojitokeza kwa wingi kwenye mikutano yake ambayo imegekua kuwa Shule ya Uraia.
Ni upendo, furaha na elimu.

Chagua Rais Lissu, chagua mbunge Chadema, chagua diwani Chadema.

Wagombea wa CCM wote huwa wanaunga mkono hoja ambazo leo ndio mwiba mchungu kwa Watanzania, na safari hii wanaenda kuunga mkono hoja ya kuondoa ukomo wa Rais kukaa madarakani.

Fikiria mateso ya miaka hi mitano, itakuaje kama Rais akibaki bila kikomo.
 
Wakati Lisu alikimnbia DAR kwa mikutano kumdodea
Check TABATA hapo hao ni wakazi wa jimbo la Tabata tu alipoenda Mama SULUHU kampeni check alivyojaza
 
Lissu ni kiongozi wa watu, siyo kiongozi unakuwa unahutubia mkutano huku watu wamekunja ndita kama wamekunywa gongo
EF947724-1585-4F0D-803C-C01909411E01.jpeg
 
Issue waandike nini alichosema? hela alizoomba kwa wafanyabiashara na kutishia kuwa haaendelea na kampeni wasipomchangia? Au waandike nini?

Haongelei sera unatarajia waandishi waandike au watangaze kitu gani?

Waandike na kutangaza alivyocheza muziki wa Bob Marley au?
 
Chadema ipo na hali mbaya sana baada ya kukosa watu kwenye mikutano.

Wamebakia kutishia NEC tu
😁😁😁,Mataga mnahangaika!Nyomi la Lissu mnasema amekosa watu?Ndio maana nyinyi mnafunga shule na kujaza watoto lakini pia mnasomba watu na malori ili kumdanganya mwenyekiti wenu!
 
Ameandika mdau @dr.johnheshima huko mjini Instagram

Ni swali jepesi lenye jibu la ndio au hapana, lakini kabla hujajibu linahitaji tafiti isiyo rasmi kujihakiki.

Iko hivi, bi mkubwa, mamaake mwenyewe yupo mjini baada ya kaziara kafupi ka kuwatembelea marafiki zake wa zamani miji kadhaa ya kusini mpaka Kaskazini mwa Tanzania(kama mgombea vile )

Wakati tumekaa tukipiga stori jinsi alivyoona mabadiliko ya nchi, maana kuna miji imepita miaka 20 tangu alipoenda mara ya mwisho. TBC wakawa wanaonyesha nyomi la kampeni za @tunduantiphaslissu akiwa Mbarali. Nikamsikia akisema "NINGETAMANI APITE KASULU NIKIWA NIMERUDI, NAMI NIKAMUONE" Basi nami nikamjibu kimasikhara tu "tuombe uzima utamuona tu mama yangu, bado kuna miji mingi mnaweza kukutana huko"

Baada ya kumjibu hivyo huku TBC wakamuonesha rais Magufuli akimvisha kofia mwanamuziki @officialalikiba__ akaniuliza ile kofia ni ya nini!? Nikamjibu ni zawadi ya heshima na sio yeye wakwanza alishamvisha diamondplatnumz na @harmonize_tz akauliza tena mbona mikutano ya @chadematzofficial sioni wasanii!?

Nikamjibu hawana na nyomi wanakusanya na hapo hapo nikamuuliza "mama unampenda Sana Lissu" jibu lake ndio lilonifanya nijiulize HIVI NI KWELI!? Nikaona sio mbaya nikawauliza na ndugu zangu hapa

HIVI NI KWELI!?
Mama Alinijibu hivi "SIO KWAMBA NAIPENDA CHADEMA WALA LISSU, NAMPENDA SANA MAGUFULI ILA NATAKA KUMUONA LISSU MAANA SIMFAHAMU NA NIKASHANGAE MIUJIZA YA MUNGU...
Walimu walikula ada ya bure! hata kuandika hujui!!!
 
Kuna kitu cha kushangaza kwenye mikutano ya CCM. Kwanza zaidi ya nusu ya umati wamevalishwa sare za CCM.

Pili ni pale wahutubi wanaposema CCM OYEE! Waitikiaji ni kidogo mno tena wa mistari ya mbele na hawana bashasha, nderemo au vifijo.

Tatu hadhira ni kubwa lakini ni kama mazombie, yaani utafikiri imepigwa ganzi.
 
Watu wa DAR ES SALAAM huwa hawajifichi wakiamua kukudharau wala hawakufichi ona huu msafara wa Lissu siku unaenda kwenye uzinduzi wa kampeni MBAGALA ulivyodharaulika na watu wa Dar es salaa hadi unaingia uwanjani njia nzima watu walionyesha kutokujali wala kuwa na habari naye ndio maana akakimbia mji kukimbilia mikoani kwa aibu



LAKINI ona mahudhurio ya uzinduzi hapa chini wa siku ya kwanza ya LOWASSA Dar es salaam 2015 LINGANISHA na hayo ya LISSU hapo juu
Lissu watu wa DAR hawamtaki


Kwani hujui kua LOWASA alikua kiongozi wa ukawa yaani muunganiko wa vyama vyote vya upinzani hivyo watu lazima wawe wengi? Unamlinganisha aje na mtu mmoja ambae amesimama yeye mwenyewe pekee na chama chake kimoja bila muunganiko?
 
Back
Top Bottom