Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 1,914
- 6,033
Kuna tetesi kuwa Tundu Lissu amekamatwa na Polisi asubuhi hii akiwa hotelini huko Karatu.
Taarifa zaidi kukujia hapahapa jukwaani.
UPDATE:
Waliokamatwa Karatu hadi sasa ni
Polisi wanaendelea kuwatafuta wengine walio ambatana na Tundu Lissu Wilayani Karatu
====
Leo Septemba 10, 2023 Majira ya saa nne asubuhi Jeshi la Polisi wilaya ya Karatu lilifika Hotel ya Ngorongoro iliyopo Karatu na kuizingira, Polisi hao wakiwa na mitutu ya bunduki pamoja na mabomu. Jeshi hilo liliwaeleza wahudumu wa hotel hiyo kuwa wanataka kujua chumba alicholala Makamu Mwenyekiti wa Chama Bara Mhe. Tundu Lissu wakaelezwa na kwenda kwenye chumba hicho.
Baada ya purukushani ya Jeshi la Polisi na walinzi wa Mhe. Lissu, Jeshi hilo lilingia kwa nguvu katika chumba alichofikia Mhe. Lissu na kuondoka nae bila kueleza wanaenda nae wapi.
Baadae wengine waliokamatwa na Jeshi hilo ni Mhe. Susan Kiwanga, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. Catherine Ruge Katibu Bawacha Taifa, Mhe. Twaha Mwaipaya, walinzi wa Mhe. Lissu pamoja na watu wengine.
Tunaendelea kufuatilia kinachoendelea Karatu.
Samwel Welwel
===
Jeshi la Polisi wilaya ya Karatu wameamuru kufungwa kwa ofisi ya Chadema wilaya ya Karatu na kuwakamata watu wengine wakiwemo viongozi wa Chadema wa wilaya hiyo.
1. Joseph Mtui
2. John Malle
3. Fabiola Niima
4. Daniel Mnyampanda
5. Eliya Kibola, Katibu wa Chadema wilaya ya Karatu
6. Valerian Qurama
7. Samwel Welwel, Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Karatu
Taarifa zaidi kukujia hapahapa jukwaani.
UPDATE:
Waliokamatwa Karatu hadi sasa ni
- Makamu Mwenyekiti CHADEMA Tundu Lissu
- Walinzi wote wa Tundu Lissu
- Katibu wa BAWACHA Catherine Ruge
- Mzee Hashim, Mwenyekiti Wa Baraza La Wazee CHADEMA Taifa
- Suzan Kiwanga na
- Mwandishi wa Jambo TV (Oscar).
Polisi wanaendelea kuwatafuta wengine walio ambatana na Tundu Lissu Wilayani Karatu
====
Leo Septemba 10, 2023 Majira ya saa nne asubuhi Jeshi la Polisi wilaya ya Karatu lilifika Hotel ya Ngorongoro iliyopo Karatu na kuizingira, Polisi hao wakiwa na mitutu ya bunduki pamoja na mabomu. Jeshi hilo liliwaeleza wahudumu wa hotel hiyo kuwa wanataka kujua chumba alicholala Makamu Mwenyekiti wa Chama Bara Mhe. Tundu Lissu wakaelezwa na kwenda kwenye chumba hicho.
Baada ya purukushani ya Jeshi la Polisi na walinzi wa Mhe. Lissu, Jeshi hilo lilingia kwa nguvu katika chumba alichofikia Mhe. Lissu na kuondoka nae bila kueleza wanaenda nae wapi.
Baadae wengine waliokamatwa na Jeshi hilo ni Mhe. Susan Kiwanga, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. Catherine Ruge Katibu Bawacha Taifa, Mhe. Twaha Mwaipaya, walinzi wa Mhe. Lissu pamoja na watu wengine.
Tunaendelea kufuatilia kinachoendelea Karatu.
Samwel Welwel
===
Jeshi la Polisi wilaya ya Karatu wameamuru kufungwa kwa ofisi ya Chadema wilaya ya Karatu na kuwakamata watu wengine wakiwemo viongozi wa Chadema wa wilaya hiyo.
1. Joseph Mtui
2. John Malle
3. Fabiola Niima
4. Daniel Mnyampanda
5. Eliya Kibola, Katibu wa Chadema wilaya ya Karatu
6. Valerian Qurama
7. Samwel Welwel, Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Karatu