Kampeni zinaenda kwa ngazi shehe. Mwanzo ilikuwa ngazi ya kanda, sasa ni ngazi ya majimbo. Kwa maana hiyo Dar bado sheikh. Tuliza mzuka, Tundu Lissu atakuponesha hicho kiharusi, au Stroke kwa lugha ya mabeberu
Kurudia rudia mikoa ni ishara ya kukosa mikakati ya kueleweka ,

Chadema wako very disorganized.

Lakini ukiwaambia ukweli watakataa, jambo ambalo tena nalo ni baya kukataa criticism.
 
Lakini tuache utani Lissu ni mtambo mgumu sana, suluba zote hizo haonyeshi hata kuchoka.
Mikutano haina burudani zaidi ya yeye kuwa burudani hapohapo msemaji mwanzo mwisho

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app

Lissu ni mpango wa Mungu

binadamu wa kawaida hawezi kufanya anayofanya lisu,hata jiwe ameshachemka

kichinjio changu nakipeleka kukinoa kwa maombi kuanzia jumapili hii hadi uchaguzi nichinje kimtelezo
 
Lakini tuache utani Lissu ni mtambo mgumu sana, suluba zote hizo haonyeshi hata kuchoka.
Mikutano haina burudani zaidi ya yeye kuwa burudani hapohapo msemaji mwanzo mwisho

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
Mimi nilijiapiza huyu hamalizi kampeni. Kwanza ametoka kuugua na kushinda ndani muda mrefu, watu wa aina hii huwa hawana kinga imara. Pili amelemaa, sikujua Kama angehimili kampeni kiasi hiki.
 
Mimi nilijiapiza huyu hamalizi kampeni. Kwanza ametoka kuugua na kushinda ndani muda mrefu, watu wa aina hii huwa hawana kinga imara. Pili amelemaa, sikujua Kama angehimili kampeni kiasi hiki.
Kiukweli hata mm nilipoona chopa imeletewa figisu nikajua huyu kwisha habari yake. Kumbe loooh!!!
 
Yes, Tundu Lissu umebakiza mikoa ya Dar, Pwani, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Manyara na Tanga. Najua mikoa yote ya kusini kwako itakuwa ni mtelezo maana utaungana na chama mshirika cha ACT Wazalendo katika kuipasua pasua CCM. Hapa Dar napo utaenda vizuri kufagia upepo alioacha Magufuli ambao nao hauvumi tena.

Najua bado pia Hai, Moshi mjini, Same na Mwanga bila kusahau Tukuyu, Kyela na Chunya.

Tukazane tumalize nchi maana muda nao unaenda sana hasa ukizingatia tuna siku 10 tu za kumaliza kampeni. Tunataka tufike mpaka Mafia hatuachi kitu.

Kila lakheri na Mungu akuepushie nongwa.
Kuna uwezekano akafunika mikoa yote,
Halafu kabakiza mikoa 6 tuu maana Pwani alishaenda siku ya kwanza labda Bagamoyo na rufiji
 
Mimi nilijiapiza huyu hamalizi kampeni. Kwanza ametoka kuugua na kushinda ndani muda mrefu, watu wa aina hii huwa hawana kinga imara. Pili amelemaa, sikujua Kama angehimili kampeni kiasi hiki.
Hata mimi sikutegemea anaweza kufanya kampeni akiwa amesimama.
Mambo ya ajabu aliyonayo Lissu.
1. Haonyeshi kujisikitikia
2. Tangu akiwa hosp alijaa tabasamu
3. Hakukatishwa tamaa kwa jaribio la mauaji

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
MAMBO MATATU YA KUOGOPESHA NA YA KUTISHA KUTOKA KWA TUNDU LISSU:

1. Aliamriwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi aende akaripoti kituo cha Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, lakini hakwenda na wakamuacha.

2. Aliandikiwa barua ya kuripoti Police Central Dar es salaam, akawajibu barua ya kuitwa Polisi siyo barua ya kirafiki, ni amri ya kisheria na inatakiwa iandike kosa nililofanya. Kwa hiyo hakwenda, na wakagairi kumuita wakamuacha.

3. Alikuwa anaenda Kibaha, Polisi Mkoa wa Pwani wakazuia njia, akasema haondoki na atalala hapo hapo, na wao wakasema watakesha naye. Lakini ilipofika saa 2 usiku, wakafungua njia, wakamuacha akaendelea na ratiba zake.

Haya mambo hata Mo-Dewji na Pesa zake hawezi kufanya, vipi kuhusu mimi na wewe? Dadeki.
 
Haya ni baadhi ya tathmini yangu
1.Hajaweka sera za Chadema zikaeleweka kwa wananchi hadi sasa
2.Anajinadi yeye zaidi sio chama au wabunge na madiwani
3.Anamzungumzia zaidi Dr Magufuli badala ya kuelezea atakachofanya yeye na chama chake wakishika dola
4.Anachukua vitu vingi humu jamii forums na kuviundia hotuba kwa asilimia 90 ya hotuba zake source ni jamii forums
5.Mahudhurio kwenye mikutano yake bado ni changamoto ni madogo
6.Anapokelewa kwa mbwembwe anapowasili kwa mapikipiki nk lakini ikifika wakati wa kuondoka anaondoka peke yake kama mwanga na wenye pilipiki wakimfikisha tu wanambwaga wala hawakai mkutano
7. Kwa kukosa viongozi wa dini kwa kutomuunga mkono kila anakoenda anazunguka na Askofu Mwamakula mjanja wa Dar es saalam kumsaidia kupiga dua hewa walau ionekane viongozi wa dini wako naye
8.Mikutano yake anaigeuza kama darasa badala ya kampeni analigeuza darasa la historia alizosoma HGL na sheria alizosoma chuo kikuu
9.Hoja ya maendeleo ya watu na sio vitu hadi sasa imemshinda kuitetea kwenye kampeni
10.Hafichi chuki yake kwa watu wa kanda ziwa
11.Hadi sasa hana uhusiano mzuri na vyombo vya ulinzi,vyombo vya habari,tume ya uchaguzi
12.Hana hela na kitendo cha kuchangisha kinawaudhi wanaotakiwa kuchanga .Hasira zao wengi wanazionyesha kuondoka mkutanoni mapema
13.Hana nyota ya mvuto hata akipita njiani na magari yake watu hawaoni kama kuna mtu mgombea uraisi anapita
14.Hajui kupanga point anapoongea.Hana mpangilio unaoeleweka na hivyo kusababisha akimaliza kuhutubia hujui hata aliongelea nini
15.Hana support ya watu wazima kwenye chama mikutano yake haijai watu wa aina zote ina na wa jinsia zote wengi unakuta ni vijana tena wa kiume ukiona mwanamke ni wa kumulika na tochi na watu wazima kuwaona ni shida ni mmoja mmoja tu
17.Kitengo cha uchakachuaji picha cha Chadema kimeharibu credibility ya Mikutano kiasi kuwa picha na video zao wanazorusha haziko credible tena hasa za mahudhurio na haziaminiwi
18.Hajali muda.Wa kufika anapotakiwa kwenye mkutano wa kampeni wala wa kuondoka
19.Hajali maamuzi ya chama chake mfano chama chake kupitia vikao vyake vya kamati kuu na mkutano mkuu vilimteua mgombea uraisi wa Chadema zanzibar yeye kufika zanzibar akaanza kumnadi Maalim SEIF
20.Majukwaa anayotumia sio presidential materia yanadhalilisha hadhi ya ugombea uraisi vijukwaa utafikiri meza ya muuza mitumba
21.Sound system iko very poor
22.Bado watu hajawakuna vizuri ana kazi kubwa ya kuwafanya wapokee hotuba zake he is not a good public speaker .Anaweza eleweka zaidi bungeni,mahakamani na kwa wasomi zaidi.Huku chini hakuwezi

Mengine ongezeni nyie
Vijana ndio wapiga kura, wanafuata sera siyo fiesta. Tukutane 28. Nyie jipangeni kuchakachua.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Zile siku 7 zilikuwa na athari sana aisee
Momentum ilikua kubwa mnoo nadhani kma wasingemfungia angemfuta kabisa Magufuli kwenye ramani kwa knockout blow.

Kikubwa hapa wabadili ratiba mfano sikuona haja ya kurudi Dodoma ilihali eneo kma Mtwara na Lindi ambako kuna kura za hasira hajafika.

Alafu vyama ambavyo havifanyi kampeni vingepigwa fine. Maana unakuta akitaka kwenda wanadai kuna mgombea wa NRA ilihali hana mkutano!!

Hivi vyama vingefutwa vibakie walau vitano tu.
 
Momentum ilikua kubwa mnoo nadhani kma wasingemfungia angemfuta kabisa Magufuli kwenye ramani kwa knockout blow.

Kikubwa hapa wabadili ratiba mfano sikuona haja ya kurudi Dodoma ilihali eneo kma Mtwara na Lindi ambako kuna kura za hasira hajafika.

Alafu vyama ambavyo havifanyi kampeni vingepigwa fine. Maana unakuta akitaka kwenda wanadai kuna mgombea wa NRA ilihali hana mkutano!!

Hivi vyama vingefutwa vibakie walau vitano tu.
Kweli kabisa
 
Back
Top Bottom