Kwenye maisha usiwe serious sana ishi Kama mwijaku furahia maisha fanya vitu ambavyo vinaonekana vya ajabu mtu mzima kuvifanya mfano kubebana mgongoni,.
Kuwa serious kwenye ishu ya posho tu maana usipokuwa serious kwenye hela unaweza kudhulumiwa usipate gawio.
Kula vinono na kunywa pombe...
Sijui shida ilikuwa nini yaani ukiwa unasafiri na bus haswa kwenda dar tuseme bus linaondoka saa 12 asubuhi basi usiku unapata mawenge usingizi hauji kabisa Ila siku hizi ukiwa na safari ya kesho saa 12 hupati mapepe wala wasiwasi wa kuachwa na gari unalala fresh tu hata ikibidi pombe...
Kwa mimi binafsi naona
1. Nikki Mbishi wa Tamaduni Muzik
2. Leonardo wa Cheka Tu
Wote ni wasomi wenye taaluma zao ambazo, zinahitajika kichwa Cha hesabu Nikki ana degree ya computer science huku Leonard yeye ana bachelor ya water resources engineering.
Kwenye interview zao utagundua wako smart...
Hatuko serious kwenye tasnia ya filamu yaani nchi yote hii wasanii wameshindwa kuja na idea ya movie ikachezwa mlima kilimanjaro au serenget au ngorongoro. Isiwe kipande tu iwe movie yote full mwanzo Mpaka mwisho ichezewe mlimani.
Mfano ni stand ya Mangaka iliyopo nanyumbu ni kali kuliko stand za songea, Mtwara, Lindi.. Serikali inakuwa inaonaje kuipa wilaya kipaumbele ilihali watu wengi wako mkoani na mzunguko uko mkoani.
Mungu ametuwekea mambo ya kutupa raha machache sana yaani ukifikiria raha ni kunywa pombe, kula chakula, kufanya mapenzi na kulala usingizi.ila cheki majanga yalivyo mengi magonjwa, majanga ya asili, umaskini, ajali n.k
At least kidogo tungekuwaga na uwezo wa kupaa Kama ndege yaani unaruka...
Swali fupi sana ila ni la msingi ambalo mtaalam wa afya yakupasa ulifanyie Utafiti uliandikie andiko.
Kwanini ukikaa bar unaweza kupiga safari lager zile kubwa za nusu lita hata 10 Sawa na lita 5 ila haiwezekani kukaa sehemu ukanywa maji Lita 5 labda unywe taratibu asubuhi Mpaka jioni.
Kwa...
Huwa nashangaa mtu anapata pesa anabaki na mawazo mengi kichwani yaani in short anaitesa pesa yake anaipa changamoto pesa yake kazi yake inakuwa ni kutatua tu matatizo mara ya wagonjwa mara ya madeni.
Sikatai kutumia pesa kwenye shida ila usijisahau babu kula kidogo sheikh kula kuku au safari...
Habari za hapa waungwana naombeni niongezeeni maarifa ya uendeshaji mzuri wa kibiashara case study ni hizi biashara zangu.
Nina jamaangu muaminifu sana kwenye maisha na ni mzawa wa hapa nilipo yeye ni fundi viatu sasa ana kijiwe chake sehemu nikaona ni center yaani tukiweka viatu vya mitumba...
Kwenye upande wa ufundi unaweza ukawa na vitu vifuatavyo mafundi wakaja kukodisha wakafanyie kazi kwa maana mafundi wengi tu nawajua wana ujuzi ila hawana vifaa.
TOOLBOX SET
GRANDER
MACHINE ZA KUPAKA RANGI
MACHINE ZA KUCHOMELEA
HAMER DRILL
MASHINE YA KUFYATUA MATOFALI
MATOROLI
MASHINE YA...
1.unaweza kuikodisha anytime
2.una weza kuzalisha tofali mwenyewe weekend ukapiga kazi mwenyewe au assume kila usiku wewe ukawa ukazalisha tofali 200 hata kama ni kwa msaada wa kibarua means Kwa week 1 una tofali 1400 ambazo ni zaidi ya million 1 na laki 4 ukitoa mchanga, maji na cement hapo...
unahitaji kufahamu sekta kubwa zaidi duniani. Itakusaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu mahali pa kuwekeza pesa zako. Inasaidia pia kujua ni viwanda gani vinakua na ambavyo vinatatizika.
1. Sekta ya Utengenezaji(manufacturing industry)
Sekta ya utengenezaji ni moja ya tasnia kongwe zaidi...
Kuna Wale Watu wa kujichanganya na watu wa namna zote wenye hela na wasio nazo, wanywa bia na wanywa gongo huwa wananifurahisha sana pale wanapopata hela yaani moyo hautulii mpaka hela iishe.
Na kati ya maskini na matajiri nimejifunza wanaoongoza Kwa dharau ni maskini hawahawa wanywa gongo...
Kosa moja tunalifanya waajiriwa ni kukurupa kujenga nyumba Kwa mikopo huku nyumba zenyewe hazimaliziki wakati pango la nyumba tu inaweza ikawa million Kwa mwaka na ukaimudu vizuri tu.
Sisemi kwamba watu wasijenge ila kuna ushauri mbalimbali humu ndani tumeona bin heri kujipata kwanza kwenye...
Inakuwa na mchanganyiko wa
Soseji
Mayai mawili ya kukaanga
Uyoga
Viazi vilivyokaangwa vikakauka vizuri ama chips
Nyanya kipande unaila ikiwa mbichi
Maharage yasiyokaangwa
steak ndogo ya kipande cha nyama sio mbaya sana
Mkate pia ukiweka slace mbili sio kesi.
Habari za asubuhi huku tukiendelea na vita lazima maisha yaendelee Tuamke kuinua uchumi unaoanguka nahitaji kujua kama umewahi kukutana na hii biashara ya kukodisha mtambo wa kuchanganya zege Tena Kwa mikoani huku kweli nitakuwa nimefanya uwekezaji wenye matokeo nikinunua hio mashine?
Kipaji Ni uwezo yaani watu wanakuwa na maslahi na kile ulichonacho wakati hamu ni mapendeleo ni hisia ama tamaa unayokuwa na shauku nayo juu ya kitu /jambo fulani linalokuvutia.
Ili kukitambua kipaji chako lazima uwe makini kwenye shughuli za kila siku au matendo unayoyatenda Kila siku yapi...
Kwa sababu uzuri mikoa hiyo iko karibu na Dar hivyo wageni wakishuka Dar ni rahisi kuifikia Kwa mfano likajengwa tower pale Kilwa kuna athari gani ilihali wageni wangependa pia kutembelea mji wa Kilwa ama Lindi pia panafikika kirahisi au mfano Singida na Dodoma iko karibu, kwanini tusijenge pia...
Jana hatari Sana wingi lilitanda Mida ya mchana saa Sita kukawa giza na hapo upepo mkali watu tumejificha zinapiga radi na kuvunja minazi. Wabishi wa kuhama mabondeni wamekubali jinsi maji baridi yanavyotisha wamehama wote wamerudi vijijini na huko mashambani wasio pata na waliopata wote...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.