Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Samia Suluhu Hassan amepunguza tozo za miamala ya simu ili zisiwaathiri vijana wengi waliojiajiri kwenye huduma za fedha kwa njia ya simu. Amewataka Watanzania kutochukulia tozo kama uhasama, bali njia ya kuboresha maisha yao.
Rais Samia Suluhu...
Uliwadharau Watanzania na ukatoa kauli za kebehi kuwa hii ni sheria ya bunge hivyo kila mtanzania anatakiwa kulipa tozo za kizalendo ili kujenga shule, zahanati na vituo vya afya.
Watanzania wakakuona hufai maana ulibuni chanzo cha mapato kisichofaa na kinachowanyonya watanzania wanyonge. Maana...
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Agosti 31, 2021 ametia saini mabadiliko ya tozo za miamala ambapo serikali imepunguza 30% na makampuni ya simu Kupunguza 10% kutoka kwenye gharama za awali za ufanyaji wa miamala.
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesaini marekebisho ya Kanuni za Tozo za Miamala ya kutuma na kutoa Fedha na kupunguza viwango vya tozo kwa 30%
Pia Serikali imejadiliana na watoa huduma za simu ambao nao wameridhia kupunguza viwango vya tozo wanazotoza kati ya mtandao na mtandao mwingine kwa...
Ukifuatilia jinsi wabunge wanvyo mjadili mtu unashindwa kuelewa hawa wawakilishi walitumwa nini huko bungeni.
Swala la tozo linaumiza mwananchi Hakuna hata wa kuligusia lakini ukisikia wanavyomjadili Silaa na Gwajima utafikiri ndo hayo waliomba kura wakayajadili huko bungeni.
WanaJF,
Kutokana na kauli ya msemaji ww serikali aliyoitoa juzi, Leo ndo siku ya tamko rasmi juu ya mustakabali wa tozo za miamala.
Je, mpaka muda huu, kunaueyote ambaye amepata update ya tamko tajwa atujuze?
Watanzania sasa wamemuelewa Mama na kukubali kulipa Tozo na kodi kwa moyo mmoja. Katika mitandao malalamiko hayo yamepungua, na leo kulikuwa na Thread moja tu ya kulalamikia kuchelewa kwa muamala kwa ajili ya Tozo na si lalamiko la tozo. Ni suala la utendaji tu
Hii imetokana na watanzania...
Ni wakati mgumu sana kwa wafanya biashara; purchasing power ya wananchi imeshuka mno.
Pesa inaenda moja moja serikalini bila kupitia kwa wafanya biashara
Tozo ni laana kali Sana. Wachumi fanyani kazi yenu la sivyo kila kitu itasimama. Hakuna tena kuzungusha hela ni kulipa Tozo tu.
Wenye...
Mama Samia kwa nini mnafanya hivi, mbona hii sio fair? Ni wapi tumekukosea?
Kabla nilitegemea ulipoingia ungepunguza ukali wa maisha Ila ukali ndio unazidi.
Mama Samia mbona hakuna aliyekataa kulipa Kodi?
Ndani ya miezi minne kufanya haya mabadiliko makubwa hivi huoni ni kama unatutesa sana...
Haongei sana bali Anatekeleza sana!
Hana papara Ila anafanya kila kitu Kwa ustadi mkubwa. Sio mtu wa kupanic Ila anaamini kwenye anachofanya
Amewekeza sana kwenye kupanga mikakati kabambe na kuhakikisha inatekelezwa ipasavyo Kwa utekelezaji madhubuti wa Serikali
Nimefuatilia katika hili suala...
Awamu ya kwanza ya Vituo vya Afya 90 kati ya 207 katika Tarafa zisizo na Vituo vya Afya, ambazo zimepokea fedha Mil. 250 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje (OPD), Jengo la Maabara na Kichomea Taka hii hapa.
Watanzania waelewe, serikali haina vyanzo vingine vya mapato zaidi ya kodi ya Watanzania.
Watanzania tunataka maendeleo,barabara nzuri,reli,umeme, shule,hospitali, miji iliyopangika,maji, serikali yenye ufanisi,ulinzi na usalama,lakini ili upate vitu hivyo lazima ugharamikie kwa tozo na kodi...
Ni kilio kilio cha tozo, makato, kila mahali.
Ila watanzania wenzangu tukiendelea kusikilizia maumivu haya makali kabisa, embu kwa pamoja tujiulize maswali tafakuri yafuatayo
Je, makato na tozi za zamani katika miamala ya simu, vilienda wapi? Je, tulishawahi kufanyiwa press conference ya...
ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe Mkoa wa Kagera, Dk. Benson Bagonza ametoji maswali nane juu ya tozo za miamala ya simu na majengo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kagera … (endelea).
Tangu kuanza kwa tozo hizo, zimeibua mjadala kwa wananchi huku Serikali...
Nachukua fulsa hii kumpongeza mama kwa kazi kubwa anazo zifanya kwa taifa hili tena ukizingatia amepokea kijiti kama mpira wa krosi ya kubabatizwa, lakini anajaribu kuutuliza mpira utulie hili aweze kuucheza.
Nikirudi katika mada
Hili lilionekana zaidi ile siku alipokuwa akihojiwa na Idhaa ya...
Watanzania muda tulio nao kwa sasa na matatizo tunayo pambana nayo liwe fundisho.
Mwaka 2020 October tukubali kuwa tulichezewa sana na tukakubali na matokeo yake ndiyo haya sasa.
Bunge lililopatikana ni matokeo ya sisi kukubali kudanganywa kwa maneno mazuri lakini sasa tunaonja shubiri...
Tanzania nchi yenye kila aina ya raslimali nchi yenye nguvu kazi ya kutosha watu mil.60
Nchi yenye ardhi nzuri kwa kilimo na makazi lakini wananchi wake ni masikini wa kutupwa wamerundikiwa furushi la tozo kila mwananchi kalibeba furushi
Ili tuyaepuke hayo maisha ni muhimu katiba mpya...
Ndugu zangu Watanzania tumekosea wapi mbona siku hadi siku mambo yanazidi kuwa tight sana mtaani huku. No pesa ukitumia ka hela kako kidogo unakutana na makato ya ajabu,ukiweka Vocha usalimie ndugu & jamaa napo tabu.
Day after day wanakuja na mbinu mpya sio kwa ajili ya kumpa ahueni Mtanzania...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.