Waziri Mwigulu Nchemba: Rais Samia Suluhu Hassan amepunguza tozo za miamala ya simu ili zisiwaathiri vijana wengi waliojiajiri kwenye huduma za fedha

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,792
4,448
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Samia Suluhu Hassan amepunguza tozo za miamala ya simu ili zisiwaathiri vijana wengi waliojiajiri kwenye huduma za fedha kwa njia ya simu. Amewataka Watanzania kutochukulia tozo kama uhasama, bali njia ya kuboresha maisha yao.

Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza fedha zote zitakazokusanywa kwenye tozo za miamala ya simu kuanzia leo Septemba Mosi zielekezwe kwenye sekta ya elimu (kujenga/kukarabati madarasa na madawati) ili kupanua fursa ya elimu kwa watoto wengi zaidi.

Nchemba.jpg
 
Leo nimepigiwa simu na Voda kwa namba yao ya 100,wamenishawishi kufanya miamala kwani tozo imeshapunguzwa!
Naona kuna kila dalili miamala imepungua sana!
 
Leo nimepigiwa simu na Voda kwa namba yao ya 100,wamenishawishi kufanya miamala kwani tozo imeshapunguzwa!
Naona kuna kila dalili miamala imepungua sana!
Yani Voda wakutafute kwa ile namba ya Customer care? Daaah 😂😂😂😂
 
Yani Voda wakutafute kwa ile namba ya Customer care? Daaah 😂😂😂😂
Mkuu unabisha?Hebu uliza,najua kuna mwingine limemtokea!Hata mimi nimepata mshtuko kuona namba 100,nikajua labda kuna kabahati nasibu nimeshinda huko voda kumbe wananibia nifanye miamala!
 
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Samia Suluhu Hassan amepunguza tozo za miamala ya simu ili zisiwaathiri vijana wengi waliojiajiri kwenye huduma za fedha kwa njia ya simu. Amewataka Watanzania kutochukulia tozo kama uhasama, bali njia ya kuboresha maisha yao...
Kwani mwanzo Mwigulu ulivyopanga viwango hivyo hukujua kama vitaathiri ajira ya vijana wengi waliojiajiri kwenye vibanda vya simu??

Halafu hayo madai yako kuwa Rais Samia ndiyo amepunguza hivyo viwango nalo ni la uongo!

Ukweli ni kuwa, bila wananchi kupaza sauti kwa kutumia mitandao ya kijamii, kamwe viwango hivyo visingepunguzwa!

Bravo watanzania kwa kukataa tozo hizo za dhuluma na uonevu
 
Na wakenya wanataka kuitumia voda kuingiza bosi wao ili aajiri wakenya wenzake.
 
Mwanzoni si walisema kamati ikishakaa watapeleka bungeni tena na sio yeye Samia au mimi nilielewa vingine
Kuna mahala sijui hapoko sawa ktk kuelewa kwetu maana hata mimi nilisikia na kuelewa hivyo, tumwombe sana Mungu ktk kuvuka hapa tulipo pafikia.
 
Back
Top Bottom