Wataalam wa Afya wanasema hali hiyo ya kukosa wagonjwa wapta tangu Novemba 2022 imewafanya kushindwa kutoa chanjo aina tatu za majaribio zilizotua nchini humo hivi karibuni.
Maambukizi ya ugonjwa huo kupitia Kirusi cha ‘Sudan strain’ yamesababisha vifo vya watu 55 tangu mlipuko ulivyoanza...
Mkuu wa wilaya ya ikungi Mhe. Jerry C. Muro amezindua zoezi la chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa hatari wa kupooza (POLIO) linalolenga kutoa chanjo kwa watoto 97, 575 katika wilaya ya Ikungi
Mhe. Muro amesema hayo wakati akizindua zoezi la chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa hatari wa polio...
Malawi imeanza kampeni kubwa ya chanjo ya watoto wachanga dhidi ya Malaria ambayo ni kampeni ya kwanza kabisa duniani, mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Dk Neema Kimambo amesema.
Chanjo ya RTS,S, kama inavyojulikana, imekuwa katika majaribio nchini Malawi, Ghana na Kenya katika...
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema hadi sasa idadi ya waliochanja chanjo ya Uviko-19 katika mkoa huo ni milioni 3.4.
Makalla ameyaeleza hayo leo Jumamosi Novemba 27, 2022 baada ya matembezi ya hiari yaliyoandaliwa na Huduma za Afya Aga Khan Tanzania (AKHS, T) kwa kushirikiana...
Serikali imetahadharisha matumizi mabaya ya dawa za antibiotiki ambazo zinasababisha usugu wa vimelea dhidi ya dawa, ikionya hatari ya kutokea madhara makubwa hasa kifo kwa watumiaji.
Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Tumaini Nagu amesema jijini Dar es Salaam kuwa takwimu zinaonesha asilimia 92...
Nimekwenda ofisi kama tatu za watu binafsi nimeshindwa kupata huduma kwa kutumia kitambulisho cha passport eti hakitambuliki. Yaani kitabu hakitambuliki?
Ni kweli karne ya 22 kuna baadhi ya ofisi hazitambui kama passport ya kusafiria ni kitambulisho.
Wananiambia hicho hakitambuliki sisi hapa...
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema Novemba 26, 2022 watazindua upya utoaji wa chanjo ya Saratani ya Mlango wa kizazi nchini kwa wasichana ili kuwakinga dhidi ya aina hii ya saratani.
“Tulianzisha sisi chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana (HPV vaccine), ikaanza...
kuna msemo kuwa muda ni mwalimu mkuu. Kila jambo wewe lipe muda ukweli utajulikana tu.
Makandokando ya chanzo za covid yaanza kujitokeza. Mkurugenzi wa Kampuni ya Pfizer akihojiwa na kamati ya Umoja wa Ulaya amekiri kua wao kama Pfizer hawakua na ushahidi wowote wa kisayansi kuthibitisha kama...
Hatua hiyo inafuatia ufanisi hafifu wa chanjo zilizotumika awali kushindwa kufanya kazi kama ilivyotarajiwa kutokana na kutofautiana na aina Kirusi kilichopo nchini humo.
Uganda inakabiliwa na Kirusi cha Sudan wakati chanjo zilizoingizwa nchini humo zilikuwa za Kirusi cha Zaire. Mkurugenzi Mkuu...
KIFADURO
Kifaduro ni ugonjwa unaoambukiza, husababishwa na vimelea vya bakteria wanaoitwa Bordetella pertussis. Huenezwa kwa njia ya hewa na huwapata hasa watoto wenye umri wa chini ya mwaka mmoja.
Ugonjwa huu huathiri mfumo wa upumuaji wa mtoto. Huambatana na dalili za homa, mafua au kuziba...
Habari wanajukwaa,
Nakuja kwenu wanajamvi kuuliza kama ni sahihi mtu kulazimishwa kuchanjwa hasa hii chanjo ya korona. Nijuavyo mimi mtu anatakiwa aelimishwe kisha ahiari pasipo shuruti.
Lakini Hali ni tofauti mkoani RUKWA wilaya ya NKASI kwani kinachoendelea sio uelimishaji wala uhamasishaji...
Magonjwa ya kuhara husababishwa na vimelea vya aina mbalimbali.
Vimelea vya Rotavirus huchangia kwa kiwango kikubwa katika magonjwa ya kuhara kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano. Kwa Mujibu wa Takwimu za WHO, zaidi ya Watoto 525,000 Duniani wenye Umri chini ya Miaka 5 hupoteza...
Huko Marekani, madhara ya chanjo ya COVID 19 yameanza kujitokeza baada ya kusababisha matatizo makubwa ya moyo kwa watoto na watu wazima chini ya miaka 40.
Magonjwa ya moyo sasa yameanza kua ya kawaida kwa watoto wadogo ambao hawakua nayo kabla ya chanjo ya covid.
Dr. Marty Makary, Profesa wa...
Kifua kikuu ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vya bakteria na huenezwa kwa njia ya hewa. Mtu mwenye maambukizi ya kifua kikuu akikohoa, kupiga chafya au kutema mate ovyo husambaza vijidudu hivyo hewani, huweza kumwambukiza mtu mwingine.
Siku hii huadhimishwa Machi 24 kila mwaka ili kuongeza...
Kwa wale waliomdhihaki Magufuli kuhusu chanjo ya Corona (planndemic disease) hii inawahusu,mkaleta ujuaji mkajidai mmesoma mnajua sana kuliko Rais wa nchi mwenye taarifa lukuki 🥺
⚫Poleni sana
Magonjwa ya ajabu ajabu yanapiga watu huko, infertility, heart attacks,blood pressure.
"Msidhani kua...
Tetanus (Pepopunda) ni ugonjwa unaosababishwa na sumu inayotokana na maambukizi ya bakteria wanaoitwa Clostridium tetani ambao hupatikana kwa wingi kwenye ardhi, vumbi na vinyesi vya wanyama.
Vimelea hivi huingia mwilini kupitia sehemu za ngozi ya mwili iliyo wazi, kitendo chochote kinacho...
Habari, wakuu.
Nimepata chanjo ya corona tarehe 15 mwezi huu pale hospitali ya bukoba government hospital. Sasa nimpewa cheti cha kawaida ambacho sio cha kidigitali.. nimeambiwa mtandao unasumbua hvo nsubirie kidogo ntatumiwa sms ya uthibitisho kuwa nimechanja pamoja na link ya kudownload hicho...
Majaribio yaliyofanyika kwa zaidi ya watoto 400 wa Afrika Magharibi ya chanjo hiyo yanaonyesha kuwa inatoa ulinzi wa hadi 80% kwa hadi miaka 2, dhidi ya #Malaria inayogharimu maisha ya takriban watoto 500,000 wa Kusini Mwa Jangwa la Sahara kila mwaka
Chanjo hiyo imetengenezwa na Wanasayansi...
Chuo kikuu cha Oxford kimekamilisha jaribio la kwanza la uchunguzi wa kitabibu kuhusu ufanisi wa chanjo mpya ya ugonjwa wa Malaria iliyopewa jina la R21/Matrix-M.
Kwa mujibu wa chapisho la uchunguzi huu lilolotolewa kwenye Jarida la The Lancet, chanjo hii inaweza kutengeneza kingamwili zenye...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.