#COVID19 Marekani: Chanjo ya Covid 19 imesababisha madhara makubwa ya moyo kwa watoto na watu wazima chini ya miaka 40,

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Huko Marekani, madhara ya chanjo ya COVID 19 yameanza kujitokeza baada ya kusababisha matatizo makubwa ya moyo kwa watoto na watu wazima chini ya miaka 40.

Magonjwa ya moyo sasa yameanza kua ya kawaida kwa watoto wadogo ambao hawakua nayo kabla ya chanjo ya covid.

Dr. Marty Makary, Profesa wa John Hopkins university na mtaalamu wa upasuaji wa moyo mwezi March 2022 aliionya CDC madhara ya kuwachanja watoto wadogo lakini akapuuzwa, sasa ukweli umejitokeza kwamba chanjo ya covid ni hatari kwa watoto na watu wazima chini ya miaka 40.

Dr. Makary anasema CDC walipuuza ushauri wa watu lakini huko umoja wa Ulaya walishtuka mapema wakapiga marufuku chanjo ya Moderna kwa watu chini ya miaka 40 kwa sababu ilionekana ina madhara makubwa zaidi kwenye moyo kuliko chanjo nyingine.

Dr. Makary anasema CDC ilichokifanya ni kudanganya umma usalama wa chanjo kinyume na ukweli wake kwamba chanjo hazikua salama kama zilivyokua zinatangazwa.

Dr. Anasema kilichofanyika ni kuonyesha madhara makubwa ya maambukizi ya covid kinyume na uhalisia na pia kuonyesha faida nyingi za chanjo kinyume na uhalisia hivyo kupelekea watu kuogopa na kwenda kuchanja.


Dr. Makary anasema mtoto mdogo wa miaka 14 amepata madhara ya chanjo sasa ya moyo ni ngumu kufika miaka 50, hivyo mustakabali wa maisha ya watoto ni muhimu kuliko faida za chanjo.

Msikilize hapa akiongea Fox News.
 
Nikisikia izo habar nashtuka sana coz 😭 wife alichanjaaa nilimuishia asichanje ila ni vile tu ni mtumish ndo hakua na namna ila Mungu amuepushe na ayo majanga
 
Back
Top Bottom