Ningependa kujua kama kuna nchi nyingine ambayo inawajengea/inawapa nyumba viongozi wake wakuu wakitoka madarakani?
Na inawapa magari mapya ambayo kila baada ya miaka mitano wanapewa mengine mapya ( sijui tamati ya yale ya awali). Uhuru amepewa nyumba?
Amandla...
Hivi karibuni tumefahamishwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema ameenda Marekani kuhudhuria Forum ya International Democrat Union (IDU) kinachofanyika Washington.
Na hivi karibuni amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Democrat Union of Africa. IDU na DUA ni ushirika wa vyama vya siasa vyenye mlengo...
Nimeona mahali mtu aliyetambulishwa kama Katibu wa CHADEMA Handeni, Kombo Matulu akihimiza wananchi wakampigie kura mgombea wa CUF.
Inaelekea CHADEMA wamebadilisha msimamo wao kuhusu kutoshiriki katika katika uchaguzi wowote mpaka Katiba mpya itakapopatikana.
Amandla.
Marekani wana taasisi mbili ambazo naamini zingetusaidia sana kama tungeziiga. Ya kwanza ni ya National Economic Council ambayo kazi yake ni kumshauri rais wao kuhusu uchumi wa nchi yao na muelekeo wa uchumi wa dunia. Ofisi hii ni ya wachumi waliobobea.
Ya pili ni Congressional Budget Office...
Hii sakata ya Halima na wenzake inatoa fursa kwa Chadema kujisahihisha. Kuna uwezekano mkubwa kuwa Halima aliamua kufanya alichofanya baada ya kuhisi kuwa kuna orodha mbadala ilitayarishwa tofauti na ile ambayo yeye na wenzake waliona kuwa ni ya haki. Wasiwasi huo usingekuwa bure kwa sababu...
Mara kadhaa nimesoma kuwa wakili walimuomba Jaji awasomee alichoandika. Hivi Mahakama haina stenographers ambao kazi yao ni kuweka kumbukumbu ya kinachoendelea?
Kama hiyo inashindikana, kwa nini wasirekodi kwa kutumia voice au video recorder? Mimi naona kumtegemea Jaji sio sahihi. Yeye...
Hivi serikali ikifuta kesi ya Mbowe peke yake Chadema watafanya nini? Watamshauri Mwenyekiti kiti wao asikubali kutoka mpaka wakina Adamoo nao waachiwe? Au watasema atoke ili awaongoze kupambania uhuru wa wanachama wenzake ambao bado wako mahabusu?
Amandla...
Leo katika mahojiano ya mtuhumiwa mmoja kwenye kesi ya ugaidi inayovuma limetumika neno "Battle Confusion". Mtuhumiwa ambae alikuwa Komandoo alisema alipotoka Congo kwenye misheni aliambiwa ana " Battle Confusion" na kuondolewa kwenye kazi yake ya uanajeshi. Hili neno sijawahi kusikia ila...
Nimewasikia watu wakisema yafuatayo kuhusu Zanzibar:
1. Zanzibar inapaswa kupata uhuru kamili kutoka kwenye utawala wa Tanganyika.
2. Tanganyika ipate Katiba yake.
Ninachojiuliza ni kuwa Zanzibar itakuwaje nchi huru kamili ndani ya Muungano? Nchi zikiungana si kila moja zinapoteza sehemu ya...
Tangu CHADEMA wameanza kampeni zao za Chadema digitali hadi ya Katiba Mpya huyu Mheshimiwa sijamsikia. Viongozi na wanachama wenzake wanawekwa ndani lakini yuko kimya.
Mwenyekiti wake anafunguliwa mashtaka ya ugaidi bado yuko kimya. Lakini wakati haya yanaendelea anafungua mashindano ya Aida...
Chief Patrick Kunambi mmoja wa waasisi wa TANU amefariki dunia. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu sehemu pema peponi na awape faraja wote aliowaacha.
Amandla.....
Ni mara nyingi huwa tunajisahau na kudhani kuwa vita ya kumkomboa mwafrika ilipiganwa (?) na mtu mweusi peke yake. Tunawasahau wakina Ruth First, Joe Slovo, Athol Fugard, Nadine Gordimer na wengine ambao walisimama kidete kumpigania mtu mweusi Afrika ya Kusini. Leo mmoja wao, Helen Suzman (...
Wakati sisi wamisheni tunajiandaa kusheherekea Krismas na wenzetu kusheherekea Iddi hivi karibuni, ni wangapi katika sisi tunaojivunia weusi wetu tutakaosheherekea Kwanzaa? Hasa wenzetu mlio kwa Obama!
Kwa wale wasiojua Kwanzaa ni nini, waangalie hapa The Official Kwanzaa Web Site - Kwanzaa...
Tutabaki na nini? Hivi hao watalii tunaotegemea kukaa kwenye hiyo Hoteli Sunrise watatoka wapi baada ya sisi kubomoa majengo yote ya kale?
Mji wa Dar es Salaam unasikitisha kwa kasi ya kubomea majengo ya zamani na kujenga maghorofa bila kuangalia infrastructure iliyokuwepo!
Lesser Flamingoes...
Ni mara chache watanzania tunapata nafasi ya kushangilia mwana riadha wetu. Jana kwa kushika nafasi ya nne huko Stuttgart umenifanya nipate faraja. Pengine hao viongozi wetu wangewatilia maanani mnaoshindana aibu iliyotukuta Beijing isingetupata. Hongera sana, binti wa Kitanzania. Usikate tamaa...
Katika nchi tuliyokuwa na upungufu wa role models ni vizuri kusoma kuwa bado kuna wazaliwa wa nchi yetu hawajakata tamaa na wanajaribu kuleta tofauti katika maisha ya muafrika. Mzungu, ndio, lakini ni muafrika kamili!
Hii inawezekana imeishatoka kule kwenye mambo ya dini. Ninachojiuliza ni vitu viwili:
1) Mbona hatusikii watu wakigombania kuuguza?
2) Huyo Mungu atakuadhibu kutokana na utakavyozikwa(ambacho kiko nje ya uwezo wako maana ndio yameisha kukuta) na siyo ulivyoishi?
Mimi naona ni aibu kubwa...
Hivi kweli nchi yenye watu zaidi ya milioni moja( sawasawa na Mauritius) inaweza kujisifia kuongeza export kutoka dola milioni tatu kwa mwezi hadi milioni tisa na nusu? Na hii ikafanywa kichwa cha habari! Tutafika kweli?
By THISDAY REPORTER
Dar es Salaam
THE Chief Secretary, Philemon Luhanjo, has intervened to help convince Mlimani Holdings Limited carry on with the multi-billion shillings Mlimani City project whose progress has been proceeding at a snails pace.
Documentary evidence availed to THISDAY...
Kutokana na ramani nyingi ( mfano ni hiyo hapo juu) mpaka huu uko ukingoni mwa ziwa Nyasa/Malawi na ziwa lote ni la Malawi.Ina maana kuwa wavuvi na boti zetu zinaposafiri mno zinaingia bila kibali katika nchi nyingine? Au wametuazima kwa muda? Mbona hali ni tofauti kwenye maziwa Tanganyika na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.