Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 8,940
- 6,854
Nimewasikia watu wakisema yafuatayo kuhusu Zanzibar:
1. Zanzibar inapaswa kupata uhuru kamili kutoka kwenye utawala wa Tanganyika.
2. Tanganyika ipate Katiba yake.
Ninachojiuliza ni kuwa Zanzibar itakuwaje nchi huru kamili ndani ya Muungano? Nchi zikiungana si kila moja zinapoteza sehemu ya uhuru wake na kuuweka kwenye Muungano wao? Watu wanasema kuwa lazima Zanzibar wawe na passport zao. Sawa, lakini hii si ina maana Zanzibar iwe na balozi zake na iwe na mamlaka kamili kuhusu uhamiaji? Ni nchi gani ambayo ni Federation ambayo constituent countries kila moja ina passport yake? Sijawahi kusikia passport za Scotland, Wales, Catalonia, Quebec n.k. Tukifikia hapo maana yake hamna Muungano.
Kuna watu wanakalamika kuhusu kodi kati ya Zanzibar na Tanzania Bara. Kuwa mtu ukinunua kitu Zanzibar,ukikileta bara unatozwa kodi tena. Si ndivyo ilivyo kati ya nchi mbili huru? Hivi wanadhani serikali huru ya Tanganyika itakubali vitu viingie kutoka Zanzibar bila kutozwa ushuru?
Mimi binafsi sioni mantik na logic ya kuwa na nchi mbili huru ndani ya Muungano. Kwa vyovyote vile patatakiwa kuwa na serikali ya Muungano ambayo itachangiwa na nchi hizo mbili. Ingawa uchumi wa Tanganyika ni mkubwa sana ukilinganisha na Zanzibar, sidhani kama serikali yake itakubali kuchangia zaidi ya mwenzao bila kupata upendeleo fulani.
Nimesikia tena kuwa wazanzibari wangependa kuwa na serikali ya mkataba kama vile ilivyo EU. Wanachosahau ni kuwa EU sio nchi. Na sisi tukiwa na mfumo kama huo ina maana hamna Muungano kama nchi. Itakuwa bora kama nchi hizo zitashirikiana katika jumuia za nchi rafiki kama EAC, SADC n.k. Kwa msingi huo Zanzibar hawatastahili upendeleo tofauti ya ule wanaopata Kenya, Uganda na Rwanda. Vile vile Tanganyika haitapata upendeleo Zanzibar. Hii hali itakuwa rahisi kwa Tanganyika maana hali ilivyo watanganyika hawapati upendeleo wowote wakiwa Zanzibar wakati wazanzibari wana haki sawa na watanganyika wakiwa Tanzania Bara.
Inazungumziwa kupotea kwa identity ya Zanzibar wakisahau kuwa watanganyika ndio hawana identity yeyote. Na maana ya Muungano wa nchi ni kuwa identity zetu zinakuwa chini ya identity ya umoja wetu. Mscot anajivunia uscotish wake lakini anajua akitoka nje ya UK , identity yake kubwa ni ya ubritish. Mzanzibari anayesema kuwa haikubali identity ya utanzania ni kuwa hautambui Muungano.
Kuna malalamiko kuhusu maamuzi kuhusu mambo ya Zanzibar kufanyika Dodoma lakini wanasahau wabunge wa Zanzibar wana uwezo wa kuzuia bajeti ya wizara isiyo ya Muungano ambayo shughuli zake zinahusu Tanzania Bara peke yake. Hamna mtu wa bara ana nafasi ya kufanya hivyo katika Bunge la Zanzibar.
Maoni yangu ni kuwa hii hatua ya Chadema ya ku "pander" kwa wazanzibari ni misguided unless kama lengo lao ni kuvunja Muungano. Kuwageuza watanganyika kuwa oppressors wakati ni wao wenyewe waliochinjana baada ya Mapinduzi na uhuru wao ulibinywa sana chini ya utawala wa Karume ni kutowatendea haki watanganyika ambao kwa kusema kweli wamekuwa wavumilivu sana.. Wengi wa wazanzibari walikimbilia bara kuepuka mkono wa chuma wa utawala ule. Na walipokelewa bara bila masharti yeyote.
Kwa mawazo yangu, kabla hata ya kuzungumzia Katiba mpya kuna haja ya kuwa na referendum kuhusu Muungano wenyewe. Na raia wa pande zote mbili waulizwe kama wanautaka au la ( watanganyika nao waulizwe ili kuondokana na dhana kuwa suala hili ni la wazanzibari peke yao). Baada ya hapo pande zote katika hii debate zieleze faida na hasara ambazo kila upande zinapata katika Muungano. Na zitakazopatikana baada ya kutengana. Kama upande mmoja utakataa basi tutengane kiungwana kama walivyofanya Czech Republic na Slovakia.
Pande zote mbili zikikubali ndio Katiba Mpya iandikwe ikiainisha ni aina gani ya Muungano tuwe nao na mgawanyo wa majukumu uwekwe wazi. Hii kuambiana kuwa tunaweza kuwa na Muungano wa nchi mbili zenye uhuru kamili ni kudanganyana. Tukiungana kila nchi itapoteza uhuru wake kwa kiasi fulani. Hatuwezi kula keki na tukabaki nayo. Ndio ukweli wenyewe.
Amandla...
1. Zanzibar inapaswa kupata uhuru kamili kutoka kwenye utawala wa Tanganyika.
2. Tanganyika ipate Katiba yake.
Ninachojiuliza ni kuwa Zanzibar itakuwaje nchi huru kamili ndani ya Muungano? Nchi zikiungana si kila moja zinapoteza sehemu ya uhuru wake na kuuweka kwenye Muungano wao? Watu wanasema kuwa lazima Zanzibar wawe na passport zao. Sawa, lakini hii si ina maana Zanzibar iwe na balozi zake na iwe na mamlaka kamili kuhusu uhamiaji? Ni nchi gani ambayo ni Federation ambayo constituent countries kila moja ina passport yake? Sijawahi kusikia passport za Scotland, Wales, Catalonia, Quebec n.k. Tukifikia hapo maana yake hamna Muungano.
Kuna watu wanakalamika kuhusu kodi kati ya Zanzibar na Tanzania Bara. Kuwa mtu ukinunua kitu Zanzibar,ukikileta bara unatozwa kodi tena. Si ndivyo ilivyo kati ya nchi mbili huru? Hivi wanadhani serikali huru ya Tanganyika itakubali vitu viingie kutoka Zanzibar bila kutozwa ushuru?
Mimi binafsi sioni mantik na logic ya kuwa na nchi mbili huru ndani ya Muungano. Kwa vyovyote vile patatakiwa kuwa na serikali ya Muungano ambayo itachangiwa na nchi hizo mbili. Ingawa uchumi wa Tanganyika ni mkubwa sana ukilinganisha na Zanzibar, sidhani kama serikali yake itakubali kuchangia zaidi ya mwenzao bila kupata upendeleo fulani.
Nimesikia tena kuwa wazanzibari wangependa kuwa na serikali ya mkataba kama vile ilivyo EU. Wanachosahau ni kuwa EU sio nchi. Na sisi tukiwa na mfumo kama huo ina maana hamna Muungano kama nchi. Itakuwa bora kama nchi hizo zitashirikiana katika jumuia za nchi rafiki kama EAC, SADC n.k. Kwa msingi huo Zanzibar hawatastahili upendeleo tofauti ya ule wanaopata Kenya, Uganda na Rwanda. Vile vile Tanganyika haitapata upendeleo Zanzibar. Hii hali itakuwa rahisi kwa Tanganyika maana hali ilivyo watanganyika hawapati upendeleo wowote wakiwa Zanzibar wakati wazanzibari wana haki sawa na watanganyika wakiwa Tanzania Bara.
Inazungumziwa kupotea kwa identity ya Zanzibar wakisahau kuwa watanganyika ndio hawana identity yeyote. Na maana ya Muungano wa nchi ni kuwa identity zetu zinakuwa chini ya identity ya umoja wetu. Mscot anajivunia uscotish wake lakini anajua akitoka nje ya UK , identity yake kubwa ni ya ubritish. Mzanzibari anayesema kuwa haikubali identity ya utanzania ni kuwa hautambui Muungano.
Kuna malalamiko kuhusu maamuzi kuhusu mambo ya Zanzibar kufanyika Dodoma lakini wanasahau wabunge wa Zanzibar wana uwezo wa kuzuia bajeti ya wizara isiyo ya Muungano ambayo shughuli zake zinahusu Tanzania Bara peke yake. Hamna mtu wa bara ana nafasi ya kufanya hivyo katika Bunge la Zanzibar.
Maoni yangu ni kuwa hii hatua ya Chadema ya ku "pander" kwa wazanzibari ni misguided unless kama lengo lao ni kuvunja Muungano. Kuwageuza watanganyika kuwa oppressors wakati ni wao wenyewe waliochinjana baada ya Mapinduzi na uhuru wao ulibinywa sana chini ya utawala wa Karume ni kutowatendea haki watanganyika ambao kwa kusema kweli wamekuwa wavumilivu sana.. Wengi wa wazanzibari walikimbilia bara kuepuka mkono wa chuma wa utawala ule. Na walipokelewa bara bila masharti yeyote.
Kwa mawazo yangu, kabla hata ya kuzungumzia Katiba mpya kuna haja ya kuwa na referendum kuhusu Muungano wenyewe. Na raia wa pande zote mbili waulizwe kama wanautaka au la ( watanganyika nao waulizwe ili kuondokana na dhana kuwa suala hili ni la wazanzibari peke yao). Baada ya hapo pande zote katika hii debate zieleze faida na hasara ambazo kila upande zinapata katika Muungano. Na zitakazopatikana baada ya kutengana. Kama upande mmoja utakataa basi tutengane kiungwana kama walivyofanya Czech Republic na Slovakia.
Pande zote mbili zikikubali ndio Katiba Mpya iandikwe ikiainisha ni aina gani ya Muungano tuwe nao na mgawanyo wa majukumu uwekwe wazi. Hii kuambiana kuwa tunaweza kuwa na Muungano wa nchi mbili zenye uhuru kamili ni kudanganyana. Tukiungana kila nchi itapoteza uhuru wake kwa kiasi fulani. Hatuwezi kula keki na tukabaki nayo. Ndio ukweli wenyewe.
Amandla...