Battle Confusion ni nini?

Battle Confusion ni nini?

Fundi Mchundo

Platinum Member
Joined
Nov 9, 2007
Posts
12,408
Reaction score
10,601
Leo katika mahojiano ya mtuhumiwa mmoja kwenye kesi ya ugaidi inayovuma limetumika neno "Battle Confusion". Mtuhumiwa ambae alikuwa Komandoo alisema alipotoka Congo kwenye misheni aliambiwa ana " Battle Confusion" na kuondolewa kwenye kazi yake ya uanajeshi. Hili neno sijawahi kusikia ila nadhani linatokana na literal translation ya " kuchanganyikiwa vitani".

Ninachojua ni kuwa watu wengi ambao wamepitia katika matukio yenye taharuki kubwa kama vita huwa wanaugua kitu kinaitwa " Post Traumatic Stress Disorder ( PTSD)". Hali hii imewatokea sana askari waliopigana Afghanistan, Iraq na sehemu nyingine. Ni hali inatakiwa matunzo bora na tiba, sio kufukuzwa kazi. Kwa vile inaelekea tuna askari wengi wanaorudi kutoka kwenye misheni inabidi jeshi letu liupe uzito suala hili.

Amandla..
 
Leo katika mahojiano ya mtuhumiwa mmoja kwenye kesi ya ugaidi inayovuma limetumika neno "Battle Confusion". Mtuhumiwa ambae alikuwa Komandoo alisema alipotoka Congo kwenye misheni aliambiwa ana " Battle Confusion" na kuondolewa kwenye kazi yake ya uanajeshi. Hili neno sijawahi kusikia ila nadhani linatokana na literal translation ya " kuchanganyikiwa vitani".
Kundolewa Kazini nadhani ni njia pekee iwapo mtu hawezi kufanya kazi yake ipasavyo kama mwanzo..
Ninachojua ni kuwa watu wengi ambao wamepitia katika matukio yenye taharuki kubwa kama vita huwa wanaugua kitu kinaitwa " Post Traumatic Stress Disorder ( PTSD)". Hali hii imewatokea sana askari waliopigana Afghanistan, Iraq na sehemu nyingine. Ni hali inatakiwa matunzo bora na tiba, sio kufukuzwa kazi. Kwa vile inaelekea tuna askari wengi wanaorudi kutoka kwenye misheni inabidi jeshi letu likipe uzito suala hili.

Amandla..
Nadhani kuondolewa sio kufukuzwa.., unaweza kupangiwa kazi nyingine au kupumzishwa..., kuna kazi nyingine kuzifanya unaweza ukawa hatari kwako na kwa wengine wanaokuzunguka...
 
Kundolewa Kazini nadhani ni njia pekee iwapo mtu hawezi kufanya kazi yake ipasavyo kama mwanzo..

Nadhani kuondolewa sio kufukuzwa.., unaweza kupangiwa kazi nyingine au kupumzishwa..., kuna kazi nyingine kuzifanya unaweza ukawa hatari kwako na kwa wengine wanaokuzunguka...

Kwa msamiati wa kwetu kuachishwa ni kama kufukuzwa. Kwa maelezo yake ni kuwa alikuwa anapata matatizo anaposikia milio ya mizinga na bunduki kwa hiyo angeweza kuhamishiwa sehemu ambayo hatasikia milio hiyo. Aidha, anatakiwa kupewa huduma za therapy kwa maisha yake yote ili aweze kumudu athari nyingine zinazotokana na PTSD. Bahati mbaya jamii yetu kwenye matatizo ya akili tuko nyuma sana. Sio jeshini tuu, hata uraiani.

Huyu anaonekana ameweza kumudu maisha uraiani lakini wengine huwa wanaweza kufanya matendo ya ajabu sana. Wengine kwa kuamini kuwa bado wako vitani hutoa uhai wa wenzao. Sio kitu cha masihara. Hasa ukizingatia wanapata matatizo yao wakiwa wanapigania taifa lao. Wanastahili shukrani na pongezi, sio kuning'inizwa kama popo na kuchomwa kwa bisibisi.

Amandla...
 
Zamaini iliitwa na wanajeshi shell shock, kwasasa wataalamu wanaiita PTSD.

Vita sio mchezo, ni rahisi kutoa amri ukiwa ofisini lakini kwa makanda walipo mstari wa mbele ni balaa tupu.

Sijapenda walivyotendewa wale wanajeshi, naamini hata wenzao huko kambini hawajapenda pia.
 
Kitu ambacho sijapenda ni namna walivyopata torture na Policcm
Hawa jamaa ni wapumbavu na kufanya vitu unprofessional

Mateso Kama Yale yanamfanya mtu apandwe wazimu na ukichaa akafanya jambo baya ila bahati Huyo commando mvumilivu Sana aliamua kutii Sheria bila shuruti ila ningekua Mimi ningewavunja viuno hawo vilaza

Nimekumbuka filamu ya Rambo first blood sehemu ya kwanza
Jamaa katoka zake Vietnam jungle kadata na serikali imemtelekeza wakatokea kenge wakaanza kumharasy nadhani walipata majibu

Hawa Polisi wetu wajifunze kufanya Kazi Kwa weledi
Wanaboa!
 
Leo katika mahojiano ya mtuhumiwa mmoja kwenye kesi ya ugaidi inayovuma limetumika neno "Battle Confusion". Mtuhumiwa ambae alikuwa Komandoo alisema alipotoka Congo kwenye misheni aliambiwa ana " Battle Confusion" na kuondolewa kwenye kazi yake ya uanajeshi. Hili neno sijawahi kusikia ila nadhani linatokana na literal translation ya " kuchanganyikiwa vitani".

Ninachojua ni kuwa watu wengi ambao wamepitia katika matukio yenye taharuki kubwa kama vita huwa wanaugua kitu kinaitwa " Post Traumatic Stress Disorder ( PTSD)". Hali hii imewatokea sana askari waliopigana Afghanistan, Iraq na sehemu nyingine. Ni hali inatakiwa matunzo bora na tiba, sio kufukuzwa kazi. Kwa vile inaelekea tuna askari wengi wanaorudi kutoka kwenye misheni inabidi jeshi letu liupe uzito suala hili.

Amandla..
Dah... Tutakoma na misamiati, battle confusion inatokea vitani na ni hali ya kupita tu, maana yaake ni kama kupoteza uelekeo hivi, yaani kama kuzima data afu inarudi, sasa hadi huku mtaani tena khaaa!!!!!
 
Dah... Tutakoma na misamiati, battle confusion inatokea vitani na ni hali ya kupita tu, maana yaake ni kama kupoteza uelekeo hivi, yaani kama kuzima data afu inarudi, sasa hadi huku mtaani tena khaaa!!!!!
Imetajwa Mahakamani na mtuhumiwa kesi ya ugaidi. Amesema aliachishwa uanajeshi na wakubwa wake na sababu waliyompa ni kuwa anaugua "battle confusion". Tunajifunza mengi kwenye hii kesi.

Amandla...
 
Leo katika mahojiano ya mtuhumiwa mmoja kwenye kesi ya ugaidi inayovuma limetumika neno "Battle Confusion". Mtuhumiwa ambae alikuwa Komandoo alisema alipotoka Congo kwenye misheni aliambiwa ana " Battle Confusion" na kuondolewa kwenye kazi yake ya uanajeshi. Hili neno sijawahi kusikia ila nadhani linatokana na literal translation ya " kuchanganyikiwa vitani".

Ninachojua ni kuwa watu wengi ambao wamepitia katika matukio yenye taharuki kubwa kama vita huwa wanaugua kitu kinaitwa " Post Traumatic Stress Disorder ( PTSD)". Hali hii imewatokea sana askari waliopigana Afghanistan, Iraq na sehemu nyingine. Ni hali inatakiwa matunzo bora na tiba, sio kufukuzwa kazi. Kwa vile inaelekea tuna askari wengi wanaorudi kutoka kwenye misheni inabidi jeshi letu liupe uzito suala hili.

Amandla..
Fact
 
Kitu ambacho sijapenda ni namna walivyopata torture na Policcm
Hawa jamaa ni wapumbavu na kufanya vitu unprofessional

Mateso Kama Yale yanamfanya mtu apandwe wazimu na ukichaa akafanya jambo baya ila bahati Huyo commando mvumilivu Sana aliamua kutii Sheria bila shuruti ila ningekua Mimi ningewavunja viuno hawo vilaza

Nimekumbuka filamu ya Rambo first blood sehemu ya kwanza
Jamaa katoka zake Vietnam jungle kadata na serikali imemtelekeza wakatokea kenge wakaanza kumharasy nadhani walipata majibu

Hawa Polisi wetu wajifunze kufanya Kazi Kwa weledi
Wanaboa!
🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom