RockCarnegie
JF-Expert Member
- Jan 17, 2019
- 963
- 1,927
Mwanzoni ilionekana kama ni masihara kwa viongozi wa serikali ya awamu ya tano ya Chama cha Mapinduzi kujitokeza hadharani na kudai kuwa wao ni Mawe, Vichaa, Malaika na hata wengine kusema wao ni Mungu!
Nimeona pia clip ikionyesha Spika Ndugai akisema yeye ni miongoni wa walio na mafaili hosptali ya wagonjwa wa akili, Milembe!
Kauli na vitendo vya viongozi wa serikali ya awamu ya tano visivyozingatia sheria na taratibu za nchi huenda ni matokeo ya kuwa na viongozi wagonjwa wa afya ya akili!
Swali la kujiuliza ni kwa nini Chama cha Mapinduzi ambcho ndicho mdhamini wa hawa viongozi kiliamua kutuletea vichaa hawa!? Je ni makusudi au ni bahati mbaya!?
Viongozi pia ni taswira ya njinsi wananchi walivyo! Kama tuliona watu walio wagonjwa wa akili wanafaa kutuongoza, na tunaendelea kuwavumilia, basi Watanzania asilimia kubwa ni wagonjwa wa akili hata kama hatuna mafaili Milembe!
Haiwezekani kuwa na Spika wa Bunge anayepatwa na taharuki anaposikia Chama fulani kimefanya maamuzi dhidi wanachama wake, ama Rais anayelalamika kukimbizwa Mabeberu kila kukicha! Yawezekana kweli Milembe ina mafaili ya hawa Wazalendo!
Tuchapeni kazi kwa tahadhari, kakorona kanaual!
Nimeona pia clip ikionyesha Spika Ndugai akisema yeye ni miongoni wa walio na mafaili hosptali ya wagonjwa wa akili, Milembe!
Kauli na vitendo vya viongozi wa serikali ya awamu ya tano visivyozingatia sheria na taratibu za nchi huenda ni matokeo ya kuwa na viongozi wagonjwa wa afya ya akili!
Swali la kujiuliza ni kwa nini Chama cha Mapinduzi ambcho ndicho mdhamini wa hawa viongozi kiliamua kutuletea vichaa hawa!? Je ni makusudi au ni bahati mbaya!?
Viongozi pia ni taswira ya njinsi wananchi walivyo! Kama tuliona watu walio wagonjwa wa akili wanafaa kutuongoza, na tunaendelea kuwavumilia, basi Watanzania asilimia kubwa ni wagonjwa wa akili hata kama hatuna mafaili Milembe!
Haiwezekani kuwa na Spika wa Bunge anayepatwa na taharuki anaposikia Chama fulani kimefanya maamuzi dhidi wanachama wake, ama Rais anayelalamika kukimbizwa Mabeberu kila kukicha! Yawezekana kweli Milembe ina mafaili ya hawa Wazalendo!
Tuchapeni kazi kwa tahadhari, kakorona kanaual!