Habari wadau!

Leo Makamu wa rais Zanziber kazindua mbio za mwenge wa uhuru wakiwa na kauli mbiu ya maendeleo ya Viwanda.

Naomba anaye fahamu umuhimu wa kukimbiza mwenge na matumizi ya zaidi ya bilioni 400.

Nini faida yake?

Kimsingi, Mwenge unatumia gharama kubwa mno, kiasi kwamba fedha hizo zingetumika kufanya shughuli za maendeleo, baadhi ya kero kwa wananchi ama zingekwisha au kupungua kwa kiasi kikubwa.

Inashangaza kuona kuwa Mwenge ule ulikabidhiwa katika eneo la shule ambayo haikuwa na madawati.

Njia nzima katika Wilaya ya Manyoni, Singida, tangu tumepokea Mwenge, shule zote njiani wanafunzi walikuwa wamejipanga barabarani, hawakusoma siku hiyo. Lakini hata Mwenge haukusimama njiani.

Wananchi wa Lusilile na vijiji jirani waliniambia kuwa kulikuwa na msako maalumu kwa wananchi watakaokiuka kuhudhuria mbio za Mwenge, hivyo walilazimika kujipanga barabarani tangu asubuhi na baadaye kupigwa na jua kali, njaa na kiu zao hadi Mwenge ulipopita.

Wapo waliolazimishwa kucheza ngoma ili ionekane wanaufurahia Mwenge. Kifupi, wapo wananchi ambao hawakufanya kazi za kujiingizia kipato ili kuheshimu amri ya kuhudhuria mbio za Mwenge

Hata hivyo, katika mbio za Mwenge, Mwenyekiti wa CCM na katibu wake, pamoja na viongozi wa Umoja wa vijana wa chama hicho (UVCCM) ni watu wa kuheshimiwa kuliko hata askari wa cheo cha juu.

Kuna bajeti ya kuweka mafuta gari ya Mwenyekiti wa CCM, Katibu wa CCM, wa UWT, na UVCCM, japo wanahadaa kuwa Mwenge ni wa kitaifa. Ni uongo, kuthibitisha hili, huwezi kuona popote risiti ya mafuta kwa magari ya wenyeviti wa mikoa wa TLP, NCCR, CUF, CHADEMA, NLD.

Kichefuchefu kingine ni kwamba kuna fungu la kununua nguo za mapokezi ya Mwenge, zipo tofauti kati ya ofisi ya mkuu wa mkoa, ofisi ya katibu tawala wa mkoa, ofisi ya mkuu wa wilaya Ofisi ya TAKUKURU, ofisi ya Usalama wa Taifa na viongozi wengine.

Pia unakuta kuna sare za mapokezi ya Mwenge zingine za kimbizia Mwenge. Fungu la suti hizo zilitosha kununua madawati kwa ajili ya darasa moja la shule waliyoenda kukabidhiana Mwenge ambayo haikuwa na madawati.

Mwenge unatembezwa na kaulimbiu za “kumulika wezi na wala rushwa,” nilishtuka zaidi tulipokuwa Manyoni Mjini, ukarabati wa mnara wa Mwenge, mnara ambao umejengwa miaka mingi huko nyuma, mnara ulipigwa rangi na kuandikwa kaulimbiu ya “Tumethubutu, tumeweza, na Tunasonga mbele” kwa gharama ya Sh. 2.5 milioni. Haiingii akilini. Watanzania tuache kuhalalisha wizi wa kimachomacho kama huu.

Mwenge ni nini? Kwanini unatumika kama alama katika mavazi na kadi za UVCCM? Mwenge una msafara mrefu kuliko hata msafara wa rais?

Katika msafara wa Mwenge, kuna kundi kubwa la askari polisi, sijui wote hao wanalinda nini? Hivi katika Tanzania nani anaweza kuwa na wazo la kuiba Mwenge? Na akiuiba ataufanyia nini?. Polisi wanaolinda Mwenge wapo makini zaidi kuliko hata wale wanaolinda benki.

Tunaambiwa wanaangalia usalama wa Mwenge, je Mwenge huwa unaugua? Mwenge unaweza kuwekewa sumu? Mwenge na TAKUKURU au uhamiaji zina uhusiano gani? Mwenge na mkuu wa Magereza, vina uhusiano gani? Mkuu wa gereza anahusika na wafungwa, je kwenye Mwenge kuna wafungwa? Mwenge na Uhamiaji lini na wapi? Mwenge na Jeshi la Wananchi ambalo jukumu lake ni kulinda mipaka, lini na wapi na kwa nini? Wote hawa wanalipwa pesa kuhalalisha mbio hizi.

Hivi hatuwezi kufungua shule mpaka Mwenge uje? Hatuwezi kupanda miti mpaka Mwenge uje? Hatuwezi kuzindua majengo mpaka Mwenge upite. Miaka zaidi 50 ya Uhuru tumegandamizwa kiakili na Mwenge, kwanini?

Hakika Mwenge sasa unaunguza wazalendo, unanyonya wanyonge, unanyanyasa walipakodi. Unamaliza fedha lukuki bila kuwa na tija. Rais anayebana matumizi ya hovyo amebariki ukimbizwe. Ajabu.

Ni vyema Mwenge nao ukafutwa na kuzikwa kabisa, kwani nalo ni jibu, tena limekomaa, tayari kwa kutumbuliwa
Hiyo budget ya mwenge sio kweli haiwezifika 400bn

Ukiondoa mtazamo wa kupinga kila kitu hebu Fanya zoezi kufuatilia miradi itakayofunguliwa mwenge ukipita mkoan kwako
 
Nashangaa sijawahi kusikia serikali imekosa pesa ya kukimbizia Mwenge. Ila linapoibuka swala kama la kutoa ajira utasikia serikali haina pesa...
Hizi pesa za kukimbizia Mwenge huwa zinatoka kwenye vyanzo vipi ambavyo huwa havikauki? Na kwa nini bunge lisipitishe sheria ya kufuta mbio za Mwenge? Maana kwa karne hii umeshakuwa irrelevant.. Kama ni uhuru tulisha upata zaidi ya miaka hamsini iliyopita and by the way sasa kila nchi iko huru so hakuna haja ya kuendelea na sherehe zisizo na tija...
 
Waulize wafanyakazi wa serikali kinachowakuta kwenye halmashauri zao.
Huwa wanachangishwa kias Fulani, pia kila taasisi hujitegemea kushiriki mbio hizo. Mengine sijui
 
Zamani mbio za mwenge wa Uhuru zilikuwa zikikimbizwa maeneo ya mjini na vijijini kuelekea kuzindua miradi mbalimbali kwa miguu kila wanapoingia maeneo hayo,leo lengo lao lipo vile vile ila tofauti ni kuwa mbio hizi siku hizi ni mwendo wa gari mwanzo mwisho. Hata ile fursa wananchi walikuwa wakiipata ya kuukimbiza na kuushika mwenge wao imepotea,labda tatizo nini linalosababisha mabadiliko hayo!?
 
mwenge una uhusiano na nguvu za giza, kwenye ule moshi huwa kuna madawa ya kuwapumbaza wa tanzania sasa wakitumia meli au ndege moshi utapotea bure!
 
mwenge wa uhuru unafaa kuwekwa makumbusho ni upumbafu karne hii bajet ya mwenge ni mabilion kisha unaenda kufungua tundu za choo cha tope huko vijijini ambapo kinakuwa na gharama ya kununua kuku mmoja sokoni !!! what kind of nonesense is this?

instead zile bajeti wangezielekeza kila mkoa, kila mwaka,
mfano mwaka huu itajenga shule kibiti......
mwaka ujao itajenga muundo mbinu somanga....
unaofwatia inamalzia jengo la tra kule chattle.....
kuliko huu unyumbu unaofanywa sasa ,ni ufujaji wa pesa za watanzania,maana hauna faida zaidi ya hasara,ni ukosefu wa akili na maarifa kuendelea tumia mabilion kuhangaika na hiyo tochi...


MY TAKE MATUMIZI YA BAJETI YA MWENGE YABADILISHWE, NA YAELKEKEZWE KWENYE MAMBO MBALIMBALI HASA VIJIJINI IJENGE SHULE MAHOSPITALI MIUNDOMBINU MADAWATI NK.............




1B.jpg



hawa watu woote hapa wanalipwa

halafu siku hizi nasikia waalimu wanakatwa pesa kwa lazima kuchangia mwenge woyiii
 
Wananchi walishirikishwa kuushika lakini hivi sasa wanashirikishwa kuchangia,kuushika ni kwa wateule wachache,kuna haja ya mbio hizi kuendelezwa?
 
Kama swali mlivyoona hapo juu mimi nmeshidwa kujibu naomba mwenye kuweza kujibu ili na mimi nipate faida ya kufahamu mwenge unafaida gani.

Asante
 
Salam,

Nikikwambia nimekuchukia na kukukasirikia Kama ninavyouchukia mwenge.... Jihadhari sana.. Naweza kukudhuru.

Nisiwe mnafiki Lile dude ninalichukia.
 
Wote tunajuwa kwamba binge ndicho chombo cha kuweza kufanya maamzi makubwa hapa nchini, lakini kwa bahati mbaya bunge letu limeshindwa kufanya hivo.

wabunge walipaswa kwa Pauli Moja kupitisha hseria itakayozifuta mbio za mwenge hapa nchini kwani hazina Tija kwa taifa Bali zinaligharimu taifa letu.

kwa kuwa wameshindwa na wameishia kuwa mbumbu natamani magufuli angepitisha amri ya Kuwalazimisha wabunge wawe wanakatwa fedha kutoka kwenye posho za vikao na miashahara yao ya kila mwezi.

nawasilisha
 
Back
Top Bottom