Zamani mbio za mwenge wa Uhuru zilikuwa zikikimbizwa maeneo ya mjini na vijijini kuelekea kuzindua miradi mbalimbali kwa miguu kila wanapoingia maeneo hayo,leo lengo lao lipo vile vile ila tofauti ni kuwa mbio hizi siku hizi ni mwendo wa gari mwanzo mwisho. Hata ile fursa wananchi walikuwa wakiipata ya kuukimbiza na kuushika mwenge wao imepotea,labda tatizo nini linalosababisha mabadiliko hayo!?
 
mwenge una uhusiano na nguvu za giza, kwenye ule moshi huwa kuna madawa ya kuwapumbaza wa tanzania sasa wakitumia meli au ndege moshi utapotea bure!
 
mwenge wa uhuru unafaa kuwekwa makumbusho ni upumbafu karne hii bajet ya mwenge ni mabilion kisha unaenda kufungua tundu za choo cha tope huko vijijini ambapo kinakuwa na gharama ya kununua kuku mmoja sokoni !!! what kind of nonesense is this?

instead zile bajeti wangezielekeza kila mkoa, kila mwaka,
mfano mwaka huu itajenga shule kibiti......
mwaka ujao itajenga muundo mbinu somanga....
unaofwatia inamalzia jengo la tra kule chattle.....
kuliko huu unyumbu unaofanywa sasa ,ni ufujaji wa pesa za watanzania,maana hauna faida zaidi ya hasara,ni ukosefu wa akili na maarifa kuendelea tumia mabilion kuhangaika na hiyo tochi...


MY TAKE MATUMIZI YA BAJETI YA MWENGE YABADILISHWE, NA YAELKEKEZWE KWENYE MAMBO MBALIMBALI HASA VIJIJINI IJENGE SHULE MAHOSPITALI MIUNDOMBINU MADAWATI NK.............




1B.jpg



hawa watu woote hapa wanalipwa

halafu siku hizi nasikia waalimu wanakatwa pesa kwa lazima kuchangia mwenge woyiii
 
Wananchi walishirikishwa kuushika lakini hivi sasa wanashirikishwa kuchangia,kuushika ni kwa wateule wachache,kuna haja ya mbio hizi kuendelezwa?
 
Kama swali mlivyoona hapo juu mimi nmeshidwa kujibu naomba mwenye kuweza kujibu ili na mimi nipate faida ya kufahamu mwenge unafaida gani.

Asante
 
Salam,

Nikikwambia nimekuchukia na kukukasirikia Kama ninavyouchukia mwenge.... Jihadhari sana.. Naweza kukudhuru.

Nisiwe mnafiki Lile dude ninalichukia.
 
Wote tunajuwa kwamba binge ndicho chombo cha kuweza kufanya maamzi makubwa hapa nchini, lakini kwa bahati mbaya bunge letu limeshindwa kufanya hivo.

wabunge walipaswa kwa Pauli Moja kupitisha hseria itakayozifuta mbio za mwenge hapa nchini kwani hazina Tija kwa taifa Bali zinaligharimu taifa letu.

kwa kuwa wameshindwa na wameishia kuwa mbumbu natamani magufuli angepitisha amri ya Kuwalazimisha wabunge wawe wanakatwa fedha kutoka kwenye posho za vikao na miashahara yao ya kila mwezi.

nawasilisha
 
Mwenge upo mkoa wa mwanza na Leo unaingia wilaya ya Ilemela
Hakuna huduma ya daladala kuanzia eneo la National kuelekea buswelu na maeneo ya jirani
Taabu yote hii ni kwa sababu ya mwenge
Wanafunzi na watu wengine wakiwemo wanaCCM wamejazana barabarani kusubiri mwenge
Wanafunzi hawasomi Leo kisa mwenge huu ni upuuzi kuvunja ratiba za maana kisa kusubiri moto tu
Nimepita karibu na shule flani wamejaa kina mama,migambo,police na wanafunzi ambao ndo mtaji wa CCM wanasubiri mwenge
Mwanajeshi anawaamrisha mgambo kwa matusi wakae vizuri wote katika gari nkaamini kweli kazi ya jeshi ni utumwa
Tangu nazaliwa hadi sasa sijui faida ya huu mwenge kwenye nchi hii anejua aniambie
Au ndo unatumika kupumbaza watu??
 
Poleni sana, siku mwenge ukipelekwa museum na ccm nao wataufuata huko

Psalm 133:1 "Behold, how good and how pleasant it is for brethren to dwell together in unity."
 
Kwa muda mrefu wapinzani wamekuwa wakishauri mbio za mwenge zizitishwe kwani kwa sasa hazina ulazima sana na pia itasaidia kuokoa fedha zinazotengwa kwa ajili ya kugharamia shughuli za kukimbiza mwenge nchi nzima.

Wapinzani na wadau wengine badala yake walishauri mwenge huo uwekwe katika Jumba la Makumbusho kwa ajili ya kumbukumbu ya vizazi vijavyo.

Hata hivyo,ushauri huu siku zote umekuwa ukigonga mwamba na mbio hizi zimeendelea mpaka sasa.

Lakini pamoja na yote haya naomba niwe wa kwanza kutoa angalizo kuwa mbio hizi zinaweza kufutwa /kusitishwa wakati wowote ule iwapo madai ya kuporomoka kwa uchumi ni yana ukweli japo watawala wamekuwa wakipinga hoja hizi.


Hata leo mheshimiwa anaweza kabisa(natabiri) kuzifuta mbio hizi na kutangaza leo ndio siku ya mwisho ya kuadhimisha kilele cha mbio za mwenge.Kama sio leo basi inaweza kuwa siku nyingine.

Siku wakifikia uamuzi huo watakuja na sababu zao lakini kamwe hawawezi kutaja sababu zilizowahi kutolewa na wapinzani au kama kweli hali ya uchumi ndio itakuwa chanzo.

Tunaweza kuambiwa tu sasa ni wakati wa kufanya kazi au ikatolewa /zikatolewa sababu nyingine zozote zile.

Time will tell.
 
Kinachokera ni mambo yao wayaanzishe na Mwenge unabajeti yake lakini wafanyakazi ambao hatuna maana kwa serikali hii ndio tunaobanwa eti tutoe pesa za Mwenge kama wamekata increment, kupandisha madaraja na mambo mengine basi msisumbue wafanyakazi na wafanyabiashara
 
- "Mimi nawashangaa sana watu wanaotaka Mwenge ufutwe, sijui wanatoka sayari gani?

- Mimi siwezi kukubali Mwenge ufutwe, najua na Dkt. Shein hawezi kukubali mwenge ufutwe katika kipindi chake. Naomba muwazomee na muwasute hao wanaosema Mwenge ufutwe.

- Kufuta Mwenge wa Uhuru ni sawa na kufuta historia na alama za nchi yetu.

- Katika kipindi cha uongozi wangu na uongozi wa Dkt. Shein Mwenge utaendelea kuwepo na utaendelea kukimbizwa nchini Kote." Kauli ya Rais Magufuli.

Note:

Yeah hayo ni mawazo yake hakuna anaepinga mawazo ya mtu mwingine.Hata hao wanaosema mwenge haufai ni mawazo yao sioni sababu ya kutokwa na povu.Kila mtanzania anayomawazo pia tujiulize toka mwenge umeanza kukimbizwa umeliingizia taifa bei gani? Kama hakuna je'faida ya mwenge ipo wapi? Nadhani wazo la kuanzisha mwenge lilifanikiwa hapo nyuma lakini kwa dunia ya leo gharama za maisha zimezidi kuongezeka zaidi na uwendeshaji wa mwenge umekua na gharama kubwa sana.Niishauri Serikali kama mtanzania mwenge uwepo kama kawa ila uwashwe kwa siku moja kila mwezi papohapo ulipo kuliko kukimbizwa nchi nzima, pesa yake ya bajeti ya mwenge walipiwe matibabu maskini wenzetu waliopo mahospitalini kwani mwenge umekua chumaulete kwa taifa badala ya faida leo mashuleni vyoo, maabara pamoja na ofisi za walimu ni shida lakini bajeti ya mwenge ipo.
 
Back
Top Bottom