OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,200
- 103,735
Freeman Mbowe na wenzake wameletwa tayari. Lakini ulinzi mkali umeimarishwa. Askari wengi. Pia kuna zuio la watu kuingia ndani ya mahakama. Wanasema ni mawakili 20 tu, wanahabari 10 (leo wameruhusiwa), ndugu 5, Viongozi 5, lakini simu marufuku.
Askari magereza wanalalamika kwamba jana tumefanya ujinga sana. Ujinga gani, tunawaukliza, wanasema tulikuwa tunatuma habari nje. Wanamueleza Benson Kigaila, NKM CHADEMA. Tumewaeleza kwamba, anayetakiwa kulalamika ni Jaji sio wao. Mahakama siyo gereza. Wajishikilie vizuri.
Mahakama imechelewa kwa dakika 40, yote hii ni kutokana na Jamhuri kutaka kuhodhi mamlaka ya mahakama, bila kujua kwamba wote hapa tuna interest na kesi hii, wao ni walalamikaji, sisi ni watuhumiwa. Kwanini watuzuie kuingia mahakamani na simu?
Watoto wote wa Freeman Mbowe, (Nicole na Dudley) pia wapo nje ya mahakama, pamoja na ndugu zao wengine.
Kama kawaida yao, makarao waliovalia kiraia, wamekaa kwenye siti karibu zote za mahakama, wamechukua nafasi kama kesi ni yao pekee yao.
Mambo ya ajabu yanafanyika
Lakini kitu cha muhimu hadi sasa ndugu zangu ni kwamba, kwa umoja wetu wote tupo nje ya mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa, Ubungo-Mawasiliano, tumeshawaelekeza MAWAKILI wetu wasomi kwamba "No ENTRANCE NO CASE"... And it's done, hii ni open court!
Updates
Jana Jaji Mustapha Siyani alisema watuhumiwa waletwe mapema, saa 3 asubuhi kesi ianze, lakini mpaka saa 5 na Dakika 24 sasa kesi haijaanza kwa sababu ya polisi kuzuia watu. Mawakili wetu walikwenda kumuona Jaji, wanatupa taarifa kwamba Jaji amekana kuzuia Jambo hilo mahakamani.
Updates
Wakili Msomi Kibatala ameandika Jaji ameruhusu watu waachwe huru
Mahakama Kuu ilipo kesi ya Ugaidi ya Mbowe, baada ya Polisi kuzuia watu kuingia Mahakamani na kuzuia simu, Jaji ameamuru kuwa na Polisi watoke na wasiwe na simu, Mawakili wa Mbowe wote wametoka Nje kwani hii ni kesi yenye maslahi ya UMMA! Mawakili wapo Nje na UMMA
JOPO la mawakili wa Freeman Mbowe na wenzake wote wametoka nje ya chumba cha mahakama muda huu, kupinga watu kuzuiwa kuingia mahakamani, na viongozi wa CHADEMA kuingia bila simu... Saa sita na dakika sita Mchana, saa za Afrika ya mashariki, Kesi imeshindwa kuendelea..
Kesi ya ugaidi inayomkabili Mhe Mbowe na wenzake3, imeshindwa kuendelea katika Mahakama kuu baada ya Polisi kufanya fujo na hivyo watuhumiwa wamerudishwa mahabusu muda huu
Freeman Mbowe na wenzake watatu wakitolewa nje ya chumba cha mahakama ikiwa ni zaidi ya saa moja tangu kesi hiyo ilipopangwa kusikilizwa.
Kesi imesitishwa na Washitakiwa wamepelekwa Mahabusu ndogo kusubiri Uwamzi wa Jaji. Kesi zinazofanyika Open Court, watu wanaruhusiwa kuingia. Lakini hii kesi Watu wamekatazwa kuingia na wachache waliongia hawakuruhusiwa kuingia na simu.
UPDATE: Kesi inaendelea baada ya pande zote kukutana
Baada ya kuzuiwa kwa Wananchi kuingia Mahakamani kusikiliza kesi ya Mhe. Mbowe na wenzake na kupelekea Mawakili upande wa tetezi kutoka nje ya ukumbi wa mahakama, hatimae Jaji ameamuru wananchi kuingia mahakamani baada ya majadiliano ya faragha kati ya pande zote mbili.
Upande wa Jamhuri wameshindwa kuileza Mahakama kifungu cha sheria kinachokataza wananchi kuingia na simu na kutoa taarifa juu ya kinaendelea katika kesi Na. 16/2021, Jaji akasema hakuna sheria wala kanuni inayokataza watu kuingia na simu mahakamani.
Kesi inaendelea.
Jaji anaingia.
Kesi inatajwa.
Watuhumiwa wanapandishwa kizimbani.
Upande wa Mawakili wa serikali wapo nane
Upande wa utetezi wakili Peter Kibalata anatambulisha Jopo lake la mawakili wa utetezi
Mawakili wa utetezi ni;
1. Jonathan Mndeme
2. Jeremiah Mtobesya
3. Gaston Garubindi
4. Alex Massaba
5. Michael Mwangasa
6. Maria Mushi
7. Evarista Kasanga
8. Khadija Aaron
9. Nashon Nkuungu
10. Bonifasia Mapunda
11. Boniface Mwabukusi
12. Peter Kibatala
Wakili wa Serikali: Kesi imekuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa
Jaji; Shahidi aliyebakiza sehemu ya ushahidi wake aje amalizie
Wakili wa serikali; Jana uliulizwa kuhusu noteBook kama nyenzo ambayo imetajwa kwenye PGO, ulipoulizwa kama umeileta ulisema hujaileta, kwanini?
Shahidi: Note Book niliyoulizwa ilikuwa ni nyezo maalum kwa matumizi ya polisi tu.
Wakili Kibatala; OBJECTION... huko anakujibu Shahidi kuhusu matumizi note Book PGO anajadili kitu ambacho jana mimi sikumuuliza yeye.
Wakili wa Serikali: Mimi nashangaa kama ama Object kuhusu majibu ya shahidi sababu ninachojua objection ingekuwa kwenye swali
Wakili Kibatala; hii notion ya kwamba Objection unatoa kwenye maswali tu sijui wakili anaitoa wapi, OBJECTION inaweza kuwa kotekote kwa swali na majibu.
Jaji: Jana mlimuuliza nini shahidi?
Kibatala: Naomba nipitie kidogo
Jaji: Sawa endelea ukiwa tayari niambie
Shahidi: Anayoosha mkono
Jaji: Shahidi unataka kufanya nini kuendelea kutoa ushahidi wakati tunasubiria?
Shahidi: Nataka kumsaidia mheshimiwa
Jaji; Hiyo siyo kazi yako
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji kama inawezekana nirahisishe mimi siendi mbali sana
Jaji: Hapana muache wakili ajiridhishe
Jaji: Wakati wakili Kibatala anaendelea ngoja niwaulize Mawakili wengine, Je, kuna kifungu cha sheria kinachovuka mipaka nini shahidi anaweza kujibu?
Wakili Mtobesya anasimama anasema sheria ya ushahidi inasema kwamba wakati shahidi anaongozwa baada ya maswali ya kudodoswa anatakiwa asitoke nje ya yale maswali ya dodoso, na kama mahakama itamruhusu basi mahakama itamruhusu mtoa dodoso arududie tena cross examination
Jaji: Sasa kuna tatizo kama mtaomba mbeleni?
Wakili Kibatala: Amemaliza kupata kifungu cha PGO 236 (3)9 anakisoma kuwa "Afisa wa polisi ambaye yupo kazini ambaye yupo mbali na kituo chake cha kazi anapomkamata mtuhumiwa anatakiwa kumtaarifu sababu za kumkamata Mtuhumiwa huyo, na kumuandika maelezo ya onyo katika notebook sehemu ya 10 inasema Afisa huyo wa Polisi atatakiwa kurekodi Jibu la mtuhumiwa huyo katika Notebook na atatikwa kutumia Notebook hiyo mahakamani
Jaji: Haya wakili wa serikali bado baada ya maelezo unataka kuendelea na swali lako?
Wakili wa Serikali: basi naomba nisiulize tena kuhusiana na PGO naliondoa swali langu tafadhali
Wakili wa Serikali: Kingai Jana uliulizwa kuhusiana na Notebook uliyotakiwa kuleta mahakamani na ukasema hujaileta, kwanini?
Shahidi: siyo lazima kuileta mahakamani
Wakili wa Serikali: Elezea sababu ya kutokuleta mahakamani
Shahidi: ile ni facility ya polisi ya kufanya kazi, kuna vitu anaandika ni siri ya police anaweza kusoma kujikumbusha. laikini siyo lazima kuileta Mahakamani
Wakili wa Serikali: Jana uliulizwa kuhusu facility zilizokwepo wakati unamchukua maelezo mtuhumiwa wa pili, Je ulikuwa unamaanisha facilities gani?
Shahidi: kama vile viti, meza na karatasi
Wakili wa Serikali: Elezea za kwanini hukutumia
Shahidi: Nilieleza kuwa palikuwa na upelelezi unaendelea na mazingira ya kutofanya kazi ile Moshi
Wakili wa Serikali: Jana uliulizwa kuhusu Afya ya Mtuhumiwa wa pili kuhusu tatizo lake la Afya, Kwanini hukumpeleka hospitali kulijua zaidi?
Shahidi: Mtuhumiwa alinieleza alikuwa na tatizo la Afya lakini wakati namuhoji alikuwa amepona na alirejea nyumbani kwake chalinze na kufungia banda la chipsi la Biashara alipotoka kupona
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu kumkuta na silaha ukasema hukumuonya, Sasa kwanini hukuonya kwa kesi ya kukutwa na silaha?
Shahidi: Niliamini kwa sababu nimemuonya kwa Kesi kubwa ya kula njama za kutenda matendo ya kigaidi hayo mengine yangeingia ndani
Wakili wa Serikali: uliulizwa hapa kuhusiana na yule askari anayeitwa Goodluck kuhusu kufika kituo cha Polisi Mbweni, elezea alifika kwa kazi gani?
Shahidi: Kwa ajili ya kazi za kiupelelezi wakili wa Serikali: pia uliiulizwa kuhusiana na Detention Register na hukuleta hapa Mahakamani, Elezea kwanini hukuleta Detention Register
Shahidi: Mheshimiwa jaji mimi siyo custodian wa Detention kama Dention Register itahitajika basi custodian watakuja kutoa ushahidi
Wakili wa Serikali: uliukizwa kuhusu kuwatumia Adam na Mohammed kuhusu kumtafuta Moses Lijenje na kama wasingekwepo Ungetumia Njia zingine, ieleze Mahakama ni njia gani ungetumia? Shahidi: tunatumia taarifa za wasiri wetu, katika hili tuliwatumia wote, na hata hivyo hatukumpata
Wakili wa Serikali: Ni hayo Mheshimiwa Jaji JAJI: kuna lolote kwa upande wa Utetezi? wakili Peter Kibatala: Hapana mheshimiwa Jaji JAJI: kuna lolote kwa upande wa Serikali?
Wakili wa Serikali: Ni huyu SHAHIDI pekee tuliyekuwa naye leo, naomba ahirisho la kuendelea kesho, sababu mashahidi wengine wapo nje ya Dar es Salaam, na ikukupendeza Mheshimiwa Jaji leo tulichelewa kuanza kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu, kesho tunaomba kuanza saa nne kamili.
JAJI: Utetezi...?
Wakili Peter Kibatala: Hatuna pingamizi kwa Maombi waliyoleta wenzetu.
Jaji anasema, kama ilivyoombwa na Wakili wa serikali na kuungwa Mkono kwa niaba ya Mawakili wote wa washtakiwa nahairishs kesi mpaka kesho Asubuhi kuendelea na shauri
Jaji anasimama anatoka mahakamani baada ya Polisi kuamrisha... Na watuhumiwa wanaondolewa mahakamani kurejeshwa rumande.
Kwa hisani ya Martin MM - Twitter
---- MWISHO-----
Askari magereza wanalalamika kwamba jana tumefanya ujinga sana. Ujinga gani, tunawaukliza, wanasema tulikuwa tunatuma habari nje. Wanamueleza Benson Kigaila, NKM CHADEMA. Tumewaeleza kwamba, anayetakiwa kulalamika ni Jaji sio wao. Mahakama siyo gereza. Wajishikilie vizuri.
Mahakama imechelewa kwa dakika 40, yote hii ni kutokana na Jamhuri kutaka kuhodhi mamlaka ya mahakama, bila kujua kwamba wote hapa tuna interest na kesi hii, wao ni walalamikaji, sisi ni watuhumiwa. Kwanini watuzuie kuingia mahakamani na simu?
Watoto wote wa Freeman Mbowe, (Nicole na Dudley) pia wapo nje ya mahakama, pamoja na ndugu zao wengine.
Kama kawaida yao, makarao waliovalia kiraia, wamekaa kwenye siti karibu zote za mahakama, wamechukua nafasi kama kesi ni yao pekee yao.
Mambo ya ajabu yanafanyika
Lakini kitu cha muhimu hadi sasa ndugu zangu ni kwamba, kwa umoja wetu wote tupo nje ya mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa, Ubungo-Mawasiliano, tumeshawaelekeza MAWAKILI wetu wasomi kwamba "No ENTRANCE NO CASE"... And it's done, hii ni open court!
Updates
Jana Jaji Mustapha Siyani alisema watuhumiwa waletwe mapema, saa 3 asubuhi kesi ianze, lakini mpaka saa 5 na Dakika 24 sasa kesi haijaanza kwa sababu ya polisi kuzuia watu. Mawakili wetu walikwenda kumuona Jaji, wanatupa taarifa kwamba Jaji amekana kuzuia Jambo hilo mahakamani.
Updates
Wakili Msomi Kibatala ameandika Jaji ameruhusu watu waachwe huru
Mahakama Kuu ilipo kesi ya Ugaidi ya Mbowe, baada ya Polisi kuzuia watu kuingia Mahakamani na kuzuia simu, Jaji ameamuru kuwa na Polisi watoke na wasiwe na simu, Mawakili wa Mbowe wote wametoka Nje kwani hii ni kesi yenye maslahi ya UMMA! Mawakili wapo Nje na UMMA
Kesi ya ugaidi inayomkabili Mhe Mbowe na wenzake3, imeshindwa kuendelea katika Mahakama kuu baada ya Polisi kufanya fujo na hivyo watuhumiwa wamerudishwa mahabusu muda huu
Kesi imesitishwa na Washitakiwa wamepelekwa Mahabusu ndogo kusubiri Uwamzi wa Jaji. Kesi zinazofanyika Open Court, watu wanaruhusiwa kuingia. Lakini hii kesi Watu wamekatazwa kuingia na wachache waliongia hawakuruhusiwa kuingia na simu.
UPDATE: Kesi inaendelea baada ya pande zote kukutana
Baada ya kuzuiwa kwa Wananchi kuingia Mahakamani kusikiliza kesi ya Mhe. Mbowe na wenzake na kupelekea Mawakili upande wa tetezi kutoka nje ya ukumbi wa mahakama, hatimae Jaji ameamuru wananchi kuingia mahakamani baada ya majadiliano ya faragha kati ya pande zote mbili.
Upande wa Jamhuri wameshindwa kuileza Mahakama kifungu cha sheria kinachokataza wananchi kuingia na simu na kutoa taarifa juu ya kinaendelea katika kesi Na. 16/2021, Jaji akasema hakuna sheria wala kanuni inayokataza watu kuingia na simu mahakamani.
Kesi inaendelea.
Jaji anaingia.
Kesi inatajwa.
Watuhumiwa wanapandishwa kizimbani.
Upande wa Mawakili wa serikali wapo nane
Upande wa utetezi wakili Peter Kibalata anatambulisha Jopo lake la mawakili wa utetezi
Mawakili wa utetezi ni;
1. Jonathan Mndeme
2. Jeremiah Mtobesya
3. Gaston Garubindi
4. Alex Massaba
5. Michael Mwangasa
6. Maria Mushi
7. Evarista Kasanga
8. Khadija Aaron
9. Nashon Nkuungu
10. Bonifasia Mapunda
11. Boniface Mwabukusi
12. Peter Kibatala
Wakili wa Serikali: Kesi imekuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa
Jaji; Shahidi aliyebakiza sehemu ya ushahidi wake aje amalizie
Wakili wa serikali; Jana uliulizwa kuhusu noteBook kama nyenzo ambayo imetajwa kwenye PGO, ulipoulizwa kama umeileta ulisema hujaileta, kwanini?
Shahidi: Note Book niliyoulizwa ilikuwa ni nyezo maalum kwa matumizi ya polisi tu.
Wakili Kibatala; OBJECTION... huko anakujibu Shahidi kuhusu matumizi note Book PGO anajadili kitu ambacho jana mimi sikumuuliza yeye.
Wakili wa Serikali: Mimi nashangaa kama ama Object kuhusu majibu ya shahidi sababu ninachojua objection ingekuwa kwenye swali
Wakili Kibatala; hii notion ya kwamba Objection unatoa kwenye maswali tu sijui wakili anaitoa wapi, OBJECTION inaweza kuwa kotekote kwa swali na majibu.
Jaji: Jana mlimuuliza nini shahidi?
Kibatala: Naomba nipitie kidogo
Jaji: Sawa endelea ukiwa tayari niambie
Shahidi: Anayoosha mkono
Jaji: Shahidi unataka kufanya nini kuendelea kutoa ushahidi wakati tunasubiria?
Shahidi: Nataka kumsaidia mheshimiwa
Jaji; Hiyo siyo kazi yako
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji kama inawezekana nirahisishe mimi siendi mbali sana
Jaji: Hapana muache wakili ajiridhishe
Jaji: Wakati wakili Kibatala anaendelea ngoja niwaulize Mawakili wengine, Je, kuna kifungu cha sheria kinachovuka mipaka nini shahidi anaweza kujibu?
Wakili Mtobesya anasimama anasema sheria ya ushahidi inasema kwamba wakati shahidi anaongozwa baada ya maswali ya kudodoswa anatakiwa asitoke nje ya yale maswali ya dodoso, na kama mahakama itamruhusu basi mahakama itamruhusu mtoa dodoso arududie tena cross examination
Jaji: Sasa kuna tatizo kama mtaomba mbeleni?
Wakili Kibatala: Amemaliza kupata kifungu cha PGO 236 (3)9 anakisoma kuwa "Afisa wa polisi ambaye yupo kazini ambaye yupo mbali na kituo chake cha kazi anapomkamata mtuhumiwa anatakiwa kumtaarifu sababu za kumkamata Mtuhumiwa huyo, na kumuandika maelezo ya onyo katika notebook sehemu ya 10 inasema Afisa huyo wa Polisi atatakiwa kurekodi Jibu la mtuhumiwa huyo katika Notebook na atatikwa kutumia Notebook hiyo mahakamani
Jaji: Haya wakili wa serikali bado baada ya maelezo unataka kuendelea na swali lako?
Wakili wa Serikali: basi naomba nisiulize tena kuhusiana na PGO naliondoa swali langu tafadhali
Wakili wa Serikali: Kingai Jana uliulizwa kuhusiana na Notebook uliyotakiwa kuleta mahakamani na ukasema hujaileta, kwanini?
Shahidi: siyo lazima kuileta mahakamani
Wakili wa Serikali: Elezea sababu ya kutokuleta mahakamani
Shahidi: ile ni facility ya polisi ya kufanya kazi, kuna vitu anaandika ni siri ya police anaweza kusoma kujikumbusha. laikini siyo lazima kuileta Mahakamani
Wakili wa Serikali: Jana uliulizwa kuhusu facility zilizokwepo wakati unamchukua maelezo mtuhumiwa wa pili, Je ulikuwa unamaanisha facilities gani?
Shahidi: kama vile viti, meza na karatasi
Wakili wa Serikali: Elezea za kwanini hukutumia
Shahidi: Nilieleza kuwa palikuwa na upelelezi unaendelea na mazingira ya kutofanya kazi ile Moshi
Wakili wa Serikali: Jana uliulizwa kuhusu Afya ya Mtuhumiwa wa pili kuhusu tatizo lake la Afya, Kwanini hukumpeleka hospitali kulijua zaidi?
Shahidi: Mtuhumiwa alinieleza alikuwa na tatizo la Afya lakini wakati namuhoji alikuwa amepona na alirejea nyumbani kwake chalinze na kufungia banda la chipsi la Biashara alipotoka kupona
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu kumkuta na silaha ukasema hukumuonya, Sasa kwanini hukuonya kwa kesi ya kukutwa na silaha?
Shahidi: Niliamini kwa sababu nimemuonya kwa Kesi kubwa ya kula njama za kutenda matendo ya kigaidi hayo mengine yangeingia ndani
Wakili wa Serikali: uliulizwa hapa kuhusiana na yule askari anayeitwa Goodluck kuhusu kufika kituo cha Polisi Mbweni, elezea alifika kwa kazi gani?
Shahidi: Kwa ajili ya kazi za kiupelelezi wakili wa Serikali: pia uliiulizwa kuhusiana na Detention Register na hukuleta hapa Mahakamani, Elezea kwanini hukuleta Detention Register
Shahidi: Mheshimiwa jaji mimi siyo custodian wa Detention kama Dention Register itahitajika basi custodian watakuja kutoa ushahidi
Wakili wa Serikali: uliukizwa kuhusu kuwatumia Adam na Mohammed kuhusu kumtafuta Moses Lijenje na kama wasingekwepo Ungetumia Njia zingine, ieleze Mahakama ni njia gani ungetumia? Shahidi: tunatumia taarifa za wasiri wetu, katika hili tuliwatumia wote, na hata hivyo hatukumpata
Wakili wa Serikali: Ni hayo Mheshimiwa Jaji JAJI: kuna lolote kwa upande wa Utetezi? wakili Peter Kibatala: Hapana mheshimiwa Jaji JAJI: kuna lolote kwa upande wa Serikali?
Wakili wa Serikali: Ni huyu SHAHIDI pekee tuliyekuwa naye leo, naomba ahirisho la kuendelea kesho, sababu mashahidi wengine wapo nje ya Dar es Salaam, na ikukupendeza Mheshimiwa Jaji leo tulichelewa kuanza kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu, kesho tunaomba kuanza saa nne kamili.
JAJI: Utetezi...?
Wakili Peter Kibatala: Hatuna pingamizi kwa Maombi waliyoleta wenzetu.
Jaji anasema, kama ilivyoombwa na Wakili wa serikali na kuungwa Mkono kwa niaba ya Mawakili wote wa washtakiwa nahairishs kesi mpaka kesho Asubuhi kuendelea na shauri
Jaji anasimama anatoka mahakamani baada ya Polisi kuamrisha... Na watuhumiwa wanaondolewa mahakamani kurejeshwa rumande.
Kwa hisani ya Martin MM - Twitter
---- MWISHO-----