Thesis
JF-Expert Member
- Aug 30, 2017
- 1,805
- 3,087
Mkuu bi Hadija hakuwa mchafu bali ni mwanamke aliyekuwa amefiwa na mume. Kwa kawaida mwanamke aliyeolewa akiwa bikra kisha mumewe akafa na yeye akabaki bila kuzini huyo bado ni msafi. Hata huyo anayesema ameoa bikra ukweli ni kwamba ameoa mwanamke mzinzi kwasababu walifanya tendo kabla ya ndoa, hao wote ni wazinzi. Kitendo cha kukubali kutoa uchi kabla ya ndoa ni uzinzi, hilo lipo wazi, kwasababu hata joka jeusi kama asingemuo huyo dada it means bikra yake ingekuwa ishavinjwa na kuolewa bado.Mungu anavyose Msikurubie Zinaaa ....Namaanisha Wanaume wazini sanaaaa...alafu Waoe bikra wapate Vizazi vyema?...
Mtume Muhammad hakuoa Bikra..bi hadija...Je kizazi chake Ni kichafu..?
Mwenyezi Mungu anatutaka tuombe Atupe watoto walio pious ...TUMUOMBE Atupe wake na Waume wake walio wema..
Na Huyu Huyu Mungu anasema mzinifu awe na mzinifu mwenzake..
Lakini watu wanataka kumjua Mungu kwenye maswala ya kugegeda tu... ukiamua kumjua Mungu na kumfuata fuata yote aelekezayo.....
Mnasema wanawake wanajaa makanisani Kutafuta Mungu awape awaume...JE HILI NI KOSA?...Huko kanisani wanatakiwa waende watakatifu?
Jamani, tuseme ukweli, usafi wa ndoa ni wa wote wawili. Nakubaliana na mleta mada kuwa ndoa nyingi kwa sasa ni za washirika na sio wanandoa, ndio maana wanawake hawako tayari ku Sacrifice baadhi ya vitu kwa ajili ya ndoa zao na kadhalika wanaume. Wengi tunaishi kishirika na sio kindoa kwasababu ya uchafu wetu tulionao. Ukweli ni kwamba uzinzi ni uchafu mkubwa sana unachafua hadi kizazi tulichonacho, ni bahati mbaya Mambo haya ni ya kiroho sana watu wengi hawajui. "Kwa waislam Quran ipo wazi kabisa, mwanaume mzinzi humuoa mwanamke mzinzi na kadhalika mwanamke mzinzi huolewa na mwanaume mzinifu", haya maneno ni kweli, kale la laana ka uzinzi kanakuwa ndani yenu hata kama mlikutana wote mkiwa mabikra lkn mkafanya tendo kabla ya ndoa yenu, hakika nyinyi ni wazinzi na hukuna tofauti na wazinzi wengine, hivyo hako katabia kanakuwa kapo ndani yenu