Priceless soul
JF-Expert Member
- Jul 4, 2017
- 1,484
- 1,727
USIONE SIFA,KWANI MAMA AKO ALITOLEWA BIKRA NA BABAAKO?Wakuu Kwema!
Mara kwa mara nimekuwa nikihamasisha vijana humu kuwa wasioe wanawake wasio na bikra kwani hao sio wake zao. Pia mwanamke usikubali kuolewa na mwanaume ambaye hajaitoa bikra yako, huyo sio mumeo.
Huyo sio mkeo kama hukukuta bikra na wala hukuitoa. Huyo ni mke wa uzinzi, na lazima upate matokeo ya uzinzi,
Mwanamke uliyemkuta bikra na ukaitoa ndiye mkeo, huyo ndio mliwekeana agano la kuwa mwili mmoja na roho moja na yeye na sio mwanamke ambaye hukuikuta bikra yake.
Mwanamke kama hukuitoa bikra yake ni lazima akumbuke wanaume wake wa zamani, ni lazima awe mzinzi na malaya. Usioe! Usikubali kujidharau wewe kama mwanaume kwa kuoa mtu ambaye sio mke wako, huko ni kufanya uzinzi.
Leo nitanukuu aya za mke wa ujana wako ambaye sharti awe na bikra, bikra ndio ujana au usichana wa mwanamke, bila bikra mwanamke ni mtu mzima, hawi tena msichana(kijana wa kike) yaani ni kusema umeoa mzee wakati wasichana wapo.
Katika nukuu hii nimekoleza sehemu muhimu
Malaki 2:14- 16
14Mnauliza, “Mbona sasa hazikubali?” Mwenyezi-Mungu hazikubali kwa sababu anajua wazi kuwa umeivunja ahadi yako kwa mke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.
15Je, Mungu hakuwafanya nyote wawili muwe mwili mmoja na roho moja? Je, alikusudia nini alipofanya hayo? Yamkini alikusudia tuzae watoto ambao watamcha yeye. Kwa hiyo, hakikisheni kuwa hakuna hata mmoja wenu anayekosa uaminifu kwa mkewe.
16Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema: “Ninachukia talaka. Ninachukia mmoja wenu anapomtendea mkewe ukatili huo. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja wenu anayekosa uaminifu kwa mkewe.”
Mambo ya msingi
1. Usipooa mwanamke asiye na bikra Mungu hasikii maombi yako, na ukitoa bikra usimuoe mwanamke uliyembikiri pia hasikii maombi yako.
2. Mwanaume ukimtoa bikra mwanamke mnakuwa mwili mmoja na roho moja. Lakini usipotoa bikra hamuwi wamoja na ndio maana ndoa za siku hizi zinaumiza pande zote mbili
3. Mungu anachukia talaka kwa mke uliyemtoa bikra.
Kiufupi ni kuwa Mungu hamtambui mkeo kama hukumkuta na bikra, anaona mnafanya zinaa.
Usioe mwanamke asiye na Bikra, usiolewe na mwanaume ambaye hakukutoa bikra.
Jokajeusi
NINACHOJUA MKE MWEMA ANATOKA KWA MUNGU,
NA NDOA NJEMA PIA,INALINDWA NA MUNGU,NA SIO NA BIKRA.
(HIZO FIKRA ZAKO NA MAWAZO YAKO SIO SHERIA WALA PENDEKEZO)
#MJUE SANA MUNGU,ILI UWE NA AMANI#
[JAMAA ANGU AMETOKEA FAMILIA AMBAYO MAMAKE AMEKUWA NA WATOTO WAWILI KABLA YA KUOELEA NA BABA ALIYEISHI NAE MIAKA 40,LAKINI HYO,FAMILIA IMEKUWA MFANO MWEMA KAMA FAMILIA ILIYOBARIKIWA NA MUNGU,KWANI MTOTO WAO WA MWISHO ANA MASTERS, NA NDUGU ZAKE WATATU WALISHAWAH KUWA T.O KWA KILA MMOJA,MMOJA ALIKUWA T.O PRIMARY,MWENGINE ADVANCE NA MMOJA ALIBAKI LECTURE(UDSM) KWA GPA KALI...WAKIKE N MWANAMITINDO
U.K.
JITAHIDI KUMJUA MUNGU ILI UWE NA AMANI,MAANA INAONYESHA HUNA AMANI NA MOYO KWA KITU ULICHOFANYIWA NA MWANAMKE ASIYEBIKIRA KABLA YA KUMPATA HUYO,NA HIYO IMEKUPELEKEA KUCHUKIA WOTE....
NB: JE,UTAMUOZA MWANAO ALIYETOLEWA BIKRA NA MTU TOFAUTI KABLA YA KUOLEWA ?
#MJUE SANA MUNGU,UWE NA AMANI.