Jokajeusi

JF-Expert Member
Jun 1, 2018
6,305
10,582
Bikra ni alama ya uaminifu na baraka kwa kizazi chako

Habarini Wakuu.

Naweza kuwa tofauti na wengi, Naweza nisiungwe mkono na wengi hasa wale waliooa na walioolewa. Lakini ninachojaribu kueleza hapa ni suala lenye manufaa kwa familia, jamii, taifa na dunia kwa ujumla. ni suala litakalo iweka dunia salama hasa katika kipengele cha mahusiano ndani ya ndoa.

Haijalishi tulikosea wapi na kujikwaa wapi. Makosa tuliyoyafanya tuhakikishe hayajitokezi kwa wana na binti zetu. Ili familia zetu ziweze kuwa bora na zenye baraka kwa Mungu.

Bikra ni alama aliyopewa mwanamke kuthibitisha kuwa hajaguswa na mwanaume. Kwa nini Mwanamke apewe alama hii? Nitakupa mfano, Ukienda kununua kitu dukani kuna alama fulani huwekwa katika kitu husika ikiashiria kitu hicho ni kipya. Ndivyo ilivyo kwa mwanamke, bikra ni uthibitisho namba moja kuonyesha mwanamke husika ni kigoli, mwanawali na ambaye hajaguswa. Mwanaume hajapewa alama hii kwani yeye hayupo kwaajili ya mwanamke bali mwanamke kwaajili ya mwanaume. Hivyo ni kusema mwanaume ndiye mwenye wajibu wakumtafuta mwanamke kama bidhaa yenye thamani kushinda zote duniani.

Ili ndoa zetu zidumu lazima jambo hili lizingatiwe. Watu wengi wanachukulia ni jambo jepesi lakini athari zake zinaonekana. Usishangae kusikia watu kudhihakiana kwa majina elfu. Mara kibamia, sijui Bwawa haya yote ni matokeo ya kuoa wanawake wasio bikra.

Tuje kwenye maandiko;
Kumbukumbu la torati 22:
13 Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,
14 kisha akamshitaki mambo ya aibu kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia sikuona kwake alama za ubikira;
15 ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni;
16 na baba yake yule kijana awaambie wazee, Mwanamume huyu nilimpa binti yangu awe mkewe, naye amchukia;
17 angalieni, amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue yale mavazi mbele ya wazee wa mji.
18 Basi wazee wa mji ule na wamtwae yule mtu mume na kumrudi,
19 wamtoze shekeli mia za fedha, wampe babaye yule kijana, kwa kuwa amemzulia jina baya mwanamwali wa Israeli; naye awe mkewe; hana ruhusa ya kumwacha siku zake zote.
20 Lakini likiwa ni kweli neno hili, la kutoonekana kwake yule kijana alama za ubikira;
21 na wamtoe nje yule kijana mlangoni pa nyumba ya baba yake, na waume wa mji wake wampige kwa mawe hata afe; kwa vile alivyofanya upumbavu katika Israeli, kwa kufanya ukahaba katika nyumba ya baba yake; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.

Aya hizo zinaonyesha jinsi gani Bikra ilivyomuhimu kwa watu makini. Mwanamke asiye na alama za ubikira humdhalilisha Baba yake kwani inatafsirika alifanya ukahaba katika nyumba ya baba yake. Au huenda Baba yake ndiye aliyembikiri.
Pia hufanya familia husika kuonekana ni familia ya kikahaba na uzinifu jambo ambalo ni aibu kwa familia na ukoo kwa ujumla.

Aya hizo pia zinaonyesha kuwa mwanaume anayohaki ya kudai bikira kwa mke wake endapo hajaikuta. Jambo ambalo kwa ulimwengu wa sasa wanawake wengi wasingeolewa na kuishia kuwa makahaba wa mjini.

mambo ya walawi 21
13 Naye atamwoa mwanamke katika ubikira wake.
14 Asitwae mjane, wala mwanamke aliyeachwa na mumewe, wala mwanamke mwenye unajisi, wala kahaba; lakini atamwoa mwanamwali katika watu wake mwenyewe.
15 Naye asiwatie unajisi kizazi chake katika watu wake; kwa kuwa mimi ndimi Bwana nimtakasaye.

Aya hizo zinamhusu mtu yeyote makini, mwenye kumcha Mungu, anayetaka utakatifu na anayetaka ukoo na kizazi chake kiwe kitakatifu.

Ili familia isiwe najisi basi lazima mwanaume aoe mwanamke Bikra, Asioe mjane au mwanamke aliyeachwa na mtu mwingine au kuokota wanawake kwenye mabaa. Lengo ni kutokitia kizazi chake unajisi.

Kutokana na shetani kutamalaki, watu siku hizi huokota okota tuu wanawake popote. Wengine huokotana Baa na kwenye kumbi za starehe. Wengine huenda kabisa kwenye madanguro na kujichukulia wake ilimradi tuu. Watu wa namna hii hukutwa na madhila makubwa ndani ya ndoa. Kama si kuzaa watoto mashoga,basi ni wasagaji. Kama si wasagaji hupata watoto malaya na makahaba. Ni rahisi watoto kuzalia nyumbani kwani Baba na mama ni wale wale tuu.

Hapo hapo utasikia mwanaume anakibamia au hana nguvu za kiume. Au mke wangu ana K kubwa au sio mtamu. Ulijuaje mkeo sio mtamu kama hukuwahi onja vya nje.

Mwenye jukumu la kulinda bikra ya mtoto ni nani?
Jibu ni moja, Ni mzazi.
Wazazi ndio watu pekee wenye jukumu la kuilinda bikra ya mtoto wao. Changamoto inatokea pale endapo Mama hakuweza kulinda bikra yake sembuse ya mtoto. Baba naye aliuziwa mbuzi kwenye gunia hawezi kuwa na muda huo.

Lutu alikuwa ni mzazi wa kiume lakini aliweza kujua kuwa mabinti zake ni bikra. Utajiuliza alijuaje. Ni rahisi kwa Baba mwenye kujali familia yake kujua kinachoendelea kwa watoto wake. Lakini wababa wazembe na wanaoaibisha ubaba wao huuliza maswali yakijinga kama Mimi ni Baba nitawezaje kulinda bikra ya binti yangu. Jibu ni kuwa huwezi ikiwa mwenyewe ulichukua mtu asiye na bikra.

Kwa upande wa wachungaji, maaskofu na mapastor. Hii kwao ni moja ya sheria kubwa na muhimu. Mchungaji hawezi kukamilika ikiwa amechukua vitu vya mtumba. Ndio maana baadhi ya Wachungaji wa siku hizi wapo wapo tuu. Hawana tofauti na watu wa mitaani.
mambo ya walawi 21
13 Naye atamwoa mwanamke katika ubikira wake.
14 Asitwae mjane, wala mwanamke aliyeachwa na mumewe, wala mwanamke mwenye unajisi, wala kahaba; lakini atamwoa mwanamwali katika watu wake mwenyewe.
15 Naye asiwatie unajisi kizazi chake katika watu wake; kwa kuwa mimi ndimi Bwana nimtakasaye.

Nawasilisha.

Nakaribisha hoja na mapovu yenye hoja pia. Hoja zijikite kwenye maandiko ya kwenye biblia.

==============

Kwa nini maaskofu/ wachungaji hawaoi bikra; Je, wameasi kanuni zao?


===============

Somo Muhimu la Kuhusu Bikra


===========

Mwanamke Bikra ndiye Mke bora



=========

Bikra ni kapu la ndoa


===============

Madhara makuu ya kuoa mwanamke asiye na bikra



================

Kuoa mwanamke bikra sio kinga ya mkeo kutokukusaliti



 
Kuna watu wameolewa wakiwa na watoto lkn mpaka leo wanaheshimu ndoa zao, hapo utasema mwanaume ameoa laana..? Jibu ni hapana. kila mwanaume anatamani aoe bikra lkn unaweza kuta huyo huyo mwanaume ametoa bikra zaid ya 10 na bado akaoa malaya.
 
ni shajikatia tamaa kupata bikra naelekea uzeeni. uanzishwe utaratibu wa kununua bikra angalau na sisi tuambulie. wenzetu wazungu wanauza original anapita dactari kukagua una uziwa


Hahahaaaaa!!! Mkuu nimecheka sana
 
Mademu wa humu watakuambia hivi

""Kama unataka bikra Zaa wakwako""".

Ili hali kuna mdada humu katoa uzi Yupo bikra bado na anamiaka 32
..hapo utagundua kua wao walitolewa Wakiwa sekondar .

Maisha uchaguzi buaaana!!


Kweli Mkuu Maisha uchaguzi.

Si mbaya mara moja moja kuelezea mambo ya moto kama haya
 
yetooooo!!!!!!!


Ndio hivyo Dadaangu, kama wewe ulikosea jitahidi kwa wanao. Kwani unashindwa kumwambia mtoto wako wa kike kila baada ya muda fulani nitakuwa nakukagua kama umeanza mchezo mbaya au laa. Wazazi wanachakujibu kuhusu hizi ishu.

Embu fikiria Lutu ni mzazi wa kiume lakini anauhakika kabisa mabinti zake wako sildi. je wewe utashindwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…