Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,305
- 10,582
- Thread starter
- #21
Ukweli mchungu huu,sasa umepata mchumba unaambiwa mahari sh.mil.2 au 3 halafu kabla hujatoa unamuuliza mshenga kuwa awaulize wazazi wa binti kuwa binti yao ni BIKRA...povu litakalokuja utafikiri limetoka sayari ya Jupiter
Kimsingi Mwanaume akioa anayohaki na wajibu wa kuuliza habari ya Ubikra kwa mwanamke amuoaye. Mwanaume anayohaki ya kumwacha mwanamke kwa kigezo cha kutokukuta bikra kwa mwanamke.
Hata huko kanisani mchungaji hapaswi kuiita ndoa takatifu afungishapo ndoa ikiwa anajua fika waoanaji walitenda kosa la kitandani.
Hivi unadhani ile habari ya nani Baba kamili wa Patrick ingekuwa tatizo endapo Bwana Peter angemuoa Muna akiwa Bikra. Mambo mengine ni kujitakia tuu.