Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Kupitia mtandao wa X, GODBLESS LEMA ameandika kuwa wameamua kusitisha safari ya kutembelea wahanga wa mafuriko kateshi wilayani Hanang kutokana na vikwazo vikali wanavyokutana navyo tokea waanze safari ya kuelekea huko

---
Tumekatisha safari ya kuelekea Katesh- Hanang kuona waanga wa mafuriko kutokana na vikwazo vingi tulivyo kutana navyo kuanzia tunaingia Mkoa wa Manyara na zaidi vikwazo vikali tulipotaka kusalimia wagonjwa Hospital ya Rufaa Mkoa wa Manyara.Tunaendelea kuwapa pole sana wakazi wote wa Mkoa wa Manyara.Tutaongea na vyombo vya habari kwa taarifa ya kina zaidi.

Lema.png

Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe. Freeman Mbowe pamoja na viongozi wa Kanda ya Kaskazini wamefika kituo cha Polisi mkoa wa Manyara kilichopo Babati mjini. Mwenyekiti na ujumbe wake wamepitia kituoni hapo na kupokelewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara kamanda George Katabazi wakiwa njiani kuelekea wilaya ya Hanang.
Pia soma > Manyara UPDATE: Waliofariki kwa Mafuriko Wilayani Hanang wafikia 63


UBAGUZI KATIKA MAAFA YA MANYARA NI AIBU KWA TAIFA!

Ndugu Watanzania!

Kuna taarifa kuwa Jeshi la Polisi katika Mkoa wa Manyara limemzuia Mhe. Freeman Mbowe kufika eneo la maafa likisingizia kuwa limepata maagizo ya kutoka juu. Sisi Askofu tunaamini kuwa hakuna maagizo yeyote kutoka zaidi ya hofu za wanasiasa wa Manyara. Sisi hatuamini kama Rais Samia au Waziri Mkuu Majaliwa na wao wanaweza kutoa amri hizo.

Sisi Askofu tunatoa wito kwa Waziri mwenye dhamana kutoka kueleza umma nini kimetokea hadi Jeshi la Polisi likazuia Mhe Mbowe kufika Manyara. Mbona jana alikuwepo msibani kwa Askofu Kweka? Je, kwa nini Mbowe azuiwe kuwatembelea hao wahanga wakati wengine ni wafuasi wake? Je, Jeshi la Polisi halijui kama Mbowe ni kiongozi wa kitaifa katika nchi hii? Askofu au Sheikh akitaka kutembelea Manyara atazuiwa? Je, UN wakitaka kwenda huko pia watazuiwa? Taharuki ya nini kwenye maafa?

Hivi ni taifa gani hili ambalo watu hubaguana hata katika maafa kama hayo? Je, serikali iko tayari kupokea misaada ya kutoka nje ya nchi wakati inakataa misaada kutoka kwa wananchi wake wengine kama viongozi wa upinzani?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula

Dar es Salaam, 7 Desemba 2023; 9:30 alasiri
 
Kupitia mtandao wa X, GODBLESS LEMA ameandika kuwa wameamua kusitisha safari ya kutembelea wahanga wa mafuriko kateshi wilayani Hanang kutokana na vikwazo vikali wanavyokutana navyo tokea waanze safari ya kuelekea huko

---
Tumekatisha safari ya kuelekea Katesh- Hanang kuona waanga wa mafuriko kutokana na vikwazo vingi tulivyo kutana navyo kuanzia tunaingia Mkoa wa Manyara na zaidi vikwazo vikali tulipotaka kusalimia wagonjwa Hospital ya Rufaa Mkoa wa Manyara.Tunaendelea kuwapa pole sana wakazi wote wa Mkoa wa Manyara.Tutaongea na vyombo vya habari kwa taarifa ya kina zaidi.

CCM wamejimilikisha mpaka maafa. Tukisema wao ndo chanzo cha maafa wasikatae. Miongoni mwa waliopatwa na maafa wamo wanachama wa vyama tofauti. Unamzuiaje kiongozi wa Chama kwenda kuona Watanzania wenzake? Hapo wanataka wakiitisha kimkutano waseme ni CCM pekee ilikuja kuwaona.
 
Screenshot_2023-12-07-13-27-17-1.png


Kama tulivyotarajia tangu awali , Serikali ya Tanzania imekizuia Chama cha Demokrasia na Maendeleo , kuwafariji watu wa Hanang , ambako viongozi wake wamekatazwa hata kutembelea Wagonjwa hospitalini .

Hapa ndipo siasa za kishamba za ccm zilipofikia .

Screenshot_2023-12-07-15-04-47-1.png
 
Masela wa matukio wanajua mkuu wa nchi alipanga tarehe hiyo nao wakapanga tarehe hiyo makusudi ili watafute sababu na huruma chadema kwa sasa hakuna mikakati!
 
Kama tulivyotarajia tangu awali , Serikali ya Tanzania imekizuia Chama cha Demokrasia na Maendeleo , kuwafariji watu wa Hanang , ambako viongozi wake wamekatazwa hata kutembelea Wagonjwa hospitalini .

Hapa ndipo siasa za kishamba za ccm zilipofikia .

View attachment 2835675
Acheni visingizio, mmekosa michango ya kupeleka!!

Mkaweka picha ya Mfalme Mbowe kama yeye ndo kafa kwenye mafuriko
 
Back
Top Bottom