Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,568
Mke wa Ashraf Hakimi amempeleka mahakamani ili kupata talaka na alitaka Mahakama iwagawanyishe mali.
Baada ya Talaka kufanikiwa na kukubaliana kugawana mali, ikagundulika kuwa Ashraf Hakimi hakuwa na mali yoyote na hata akaunti zake benki hazikuwa na pesa yoyote.
Inaelezwa kuwa mahakama imebaini Ashraf Hakimi alishaweka mali zake zote kwa jina la mama yake muda mrefu uliopita.
==============
Aliyekuwa Mke wa Mchezaji wa Klabu ya PSG 🇨🇵, Achraf Hakimi 🇲🇦 aitwaye Hiba Abouk 🇪🇦 baada ya kuachana na Hakimi March 27,2023 alienda Mahakamani na kuwasilisha kesi ya kudai talaka huku akitaka agawiwe nusu ya mali ya Hakimi.
Baada ya Mahakama kufanya tathimini za mali za Achraf ilibaini kuwa aliyekuwa Mume wake hamiliki chochote kwani mali yake yote imesajiliwa kwa majina ya Mama yake
Hakimi anapokea Euro Milioni Moja (zaidi ya Shilingi Bilioni 2.56 kama Mshahara ndani ya PSG kila mwezi lakini 80% (zaidi ya Shilingi Bilioni 1.64) pesa hizo huwekwa kwenye akaunti ya mama yake Bi. Fatima.
"Hana mali, magari, nyumba, vito au hata nguo kwa jina lake.Wakati wowote na akitaka chochote huwa anaulizia kwa Mama yake ambaye huwa anamnunulia"
Mahakama ilitoa taarifa hiyo.
Inakadiriwa Kuwa Hakimi Achraf ana Utajiri wa Euro Milioni 17 ambazo ni zaidi ya Shilingi Bilioni 45 ila Mali zote zinamilikiwa na Mama yake, Bi Fatima.