Void ab initio
JF-Expert Member
- Mar 1, 2015
- 5,703
- 5,635
Hakuna sure odds. Asidanganywe mtu.Wakuu habari za mchana,
Hopefully wote tuko poa, tunaumiza vichwa jinsi ya kumpasua mhindi. Sasa kuna jambo moja limenigusa nimeona ngoja nilizungumze hapa. Nafkiri dhima kuu ya muanzilishi wa Uzi huu ilikua ni kushirikishana mawazo na maarifa mbalimbali katika kuweka mikeka ili tuweze kutoboa na nafkiri watu wengi pia wamewahi kufaidika humu kutokana na codes zilizotumwa na wengine humu.
Sasa, kuna tabia ilizuka ya baadhi ya members kuna kwenye Uzi wetu huu na kuleta mambo ya biashara za kuuza codes, ila wameona haitoshi mtu anakufuata kabisa inbox. Eti mkuu, kuna jamaa anauza sure odds laki mbili, unaonaje tukichanga ili tununue? For real? Kweli tumefikia huko? Hivi nitakua mpumbavu kiasi gani eti nitoe pesa kwaajili ya kununua sure odds wakati najua kabisa kwamba betting is probability? Naomba wenye hizi tabia mjiheshimu aisee. Sisi wote nia ni kumuumiza kanji ila wenzetu mmgeuka mnataka kutuumiza sisi wenzenu. Hizo mambo hazifai, wewe kama una source yako unanunua baki nayo huko, sisi tutaendelea kushare codes na insha'Allah one day tutatusua tu, pelekeni upumbavu wenu hukooo kwa washamba wa kubet!