BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,379
- 8,124
Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, Julai 11, 2023, Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa, Sensa ya Elimu na Utamaduni Zanzibar, Dk Omar Adam amesema hatua hiyo inalenga kulinda silika na tamaduni za Kizanzibari.
Amesema katazo hilo ni kwa mujibu wa sheria namba saba ya mwaka 2015 inayolenga kulinda utamaduni, mila na desturi za Mzanzibari bila kuathiri mambo mengine.
“Zanzibar hairuhusu mwanaume kusuka nywele faini ya kusuka nywele kwa Zanzibar ni Sh1 milioni au miezi sita jela au vyote kwa pamoja,” amesema.
Amesema hakuna kibali wala kulipia ili uruhusiwe kusuka nywele kwa mwanamme kama ambavyo awali ilisambaa kwennye mitandao ya kijamii.
“Sheria ilikuwa haijaanza kutekelezwa kwa kutoa faini lakini imeshatokea kama mara tatu mtu anakamatwa na kupewa onyo na wengine wapo wamejirekebisha na wengine wanaendelea kujirekebisha,” amesema
Hata hivyo, amesema katazo hilo haliwahusu Wamaasai kwasababu wanatambua kwamba huo ndio utamaduni wao kwamba mwanaume anasuka na mwanamke ananyoa au naye anasuka.
Kuhusu suala la kuathiri utalii wa Zanzibar, Katibu huyo amesema haliwezi kuathiri kwa sababu utafiti alioufanya kwanza watalii wengi hawasuki huo ni utamaduni ambao umetokea huku.
Kuhusu wasanii, amesema iwapo kuna msanii anataka kufanya shughuli zake wanaweza kukutana naye wakazungumza akavaa kofia mpaka anapokwenda kwenye maonyesho yake.
“Tunachosema suala la ushirikiano wa Muungano kisiwei kichaka cha kuharibu tamaduni silka na atamaduni za Kizanzibar ni akam ilivyo bangi hatuwezi kuruhusu kwamba ziendeel huku asili tuliochiwa na wazee wetu inapotea na katika sula hili tumejipanga tutakuwa wakali sana” alisema
Amesema watapitia hata kwenye shule kutoa elimu hiyo kwa walimu na wanafunzi ili kuwadhibiti wnafunzi wenye tabia hizo.
Sio mara ya kwanza kwa Zanzibar kutoa makatazo kama hayo, mwaka 2021 aliyekuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Lela Musa alipiga marufuku kuvaa nguo fupi (nusu uchi) kwa watalii ili kulinda utamaduni wa Zanzibar
Agizo hilo lilitolewa, huku ikielezwa iwapo wakibainika wameevaa nguo zisizo na stara atakamatwa anayewatembeza na kutozwa faini, hata hivyo jambo hilo utekelzaji wake haukuzingatiwa.
Pia, Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Rashidi Msaraka aliwahi kupiga marufuku vijana wanaonyoa viduku ambapo aliwahi kuwakamata na kuchukua mkasi kuwanyoa, hata hivyo nalo halikuwa na mwendelezo wake.
MWANANCHI
Waziri Maulid Mwita aomba radhi na kutengua kauli ya katibu mtendaji wa baraza la sanaa juu ya kulipa 1,000,000 kupata kibali cha mwanaume kusuka
Waziri Tabia amesema Katibu Mtendaji huyo aliteleza, na kwamba Zanzibar inasimamia sheria inayotaka kulinda mila na utamaduni wa Mzanzibar na ipo kanuni inayoeleza katika mipaka ya Zanzibar wanaume wa Kizanzibar kusuka ni kinyume na mila, utamaduni na desturi na yeyeote atakayekiuka hayo atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kutozwa faini ama kifungo cha miezi 6.
Zaidi soma: Waziri Maulid Mwita aomba radhi na kutengua kauli ya katibu mtendaji wa baraza la sanaa juu ya kulipa 1,000,000 kupata kibali cha mwanaume kusuka
Mada zinazohusiana
- Kwanini wanaume wanasuka nywele?
- Ni desturi kwa Waswahili kusuka nywele bila kujali jinsia zao, kwanini Zanzibar wanakataza wanaume kusuka?
- Zanzibari kukataza wanaume kusuka sio jambo la kimaadili ila ni chanzo kipya cha uchumi
Vitu vingine vilivyowahi kupigwa marufuku Zanzibar