Ni desturi kwa Waswahili kusuka nywele bila kujali jinsia zao, kwanini Zanzibar wanakataza wanaume kusuka?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,224
12,729
IMG_20230718_102124.jpg
Nimesikia Zanzibar mwanaume ukikutwa umesuka nywele unapigwa faini. Wanadai ili kulinda maadili na utamaduni wa Mzanzibari. Lakini wakati huo huo utamaduni wa Mzanzibar, kama ulivyo kwa Waswahili wote ilikuwa ni ruhusa kwa mwanaume na mwanamke kusuka nywele. Naona hawa wanaodai kulinda utamaduni huwa wanajisemea tu, hawajui hata maadili na utamaduni wao ulikuwa namna gani.


Kutoka kitabu Safari za Waswahili.

Khabari za nywele zao waanaume na wanawake.

"Wanawaume wengine wanasuka na wengine wananyoa, na kusuka kwao kwanza huosha nywele na majani ya mkunungu na maji yaliyo moto kidogo. Na majani yake yanateleza sana maji yake. Akesha osha kichwa, huleta udongo mwekundu, khalafu huzisuka zile nywele, na kupaka udongo juu yake. akesha suka hutia mafuta ya nyonyo kichwani. Huo ndio msuko wa waanaume.

Wa kadhalika wanawake wanafanya kama hivyo. Mwanamke hanyoi nywele zake, ila anayetoka katika uzazi, baada ya kwisha kuzaa kwa siku arbaini, hunyoa nywele zake, ama kama hukazaa hazinyoi. Walakini wanawake namna wanayosuka nyingine na wanaume namna nyingine, bali wote wanatia udongo mwekundu kichwani na mafuta ya nyonyo.

Wanawake wanasukwa na wanawake wenzao, na wanaume kadhalika, walakini khabari ya kusuka wanaume yalikuwa zamani, sasa mno wananyoa. Na wanawake misuko ya kizamani wameiwacha, wanasuka namna ya sasa. Kadhalika udongo mwekundu hawaatamii sana."

Pia soma:
Baraza la Sanaa Zanzibar: Wanaume Wanaosukwa kama Wanawake kukamatwa, faini ni Tsh. Milioni 1 au kifungo cha Miezi 6

Kwa marufuku nyingine Zanzibar soma:

Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya Wahanga na kuzaa gharika

 
Ile ni nchi ya kiislam, uislam wameufanya kuwa ni mila, desturi na utamaduni wao. Hawataki uislam wao uchanganywe na desturi zingine
 
Vp na wale maasai kule kuna baadhi wanasuka na ni utamaduni wao je hiko kikombe watakiepuka!?
 
Back
Top Bottom