Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
1616685494792.png

Naomba kuwapa pole Watanzania wenzangu kufuatia msiba huu mkubwa wa Taifa letu. Kifo cha Rais John J. P. Magufuli kumeacha ombwe na pia mafunzo kwa maisha yetu sote. Nimepokea kwa masikitiko makubwa msiba huu. Vyovyote vile ilivyo, kama nilivyowahi kusema huko nyuma hakuna ombwe la uongozi Tanzania.

Tumewahi kuondokewa na Waziri Mkuu akiwa madarakani, Makamu wa Rais, mawaziri n.k Huu ni wakati wa mapitio yetu. Taifa litaendelea kuwa salama na kwa pamoja katika maombolezo yetu tuondoe utata wowote ule; mama Samia Suluhu Hassan ameandaliwa na ndio sababu amekuwa makamu wa Rais mara hizi mbili chini ya Magufuli.

Taifa liko salama mikononi mwake na tumwombee hekima, ujasiri, na kuthubutu anapoliongoza kupitia maombolezo ya kitaifa na hatimaye kushika usukani wa taifa letu.

Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki mama Samia Suluhu Hassan

Amina.

WatanzaniaTukoPamoja.

2717933_tanzania-flag.jpg
 
Lakini ni mara ya kwanza tunaondokewa na Rais aliye kazini, Active President. Nyerere na Mkapa wamefariki wakiwa wastaafu. Kwa katiba yetu, Rais yuko tofauti sana na Makamu Rais, Waziri Mkuu, na wengine, ndio maana msiba wa Magufuli ni wa pekee.

Pia kutokana na staili yake ya kutawala, itakuwa ilileta mtikisiko mkubwa sana alipofariki, ni wazi alifariki siku kadhaa zilizopita. Alidhibiti kila kitu na wala hakupenda kufuata protokali. Hivyo kurejesha protokali vitakuwa moja ya majukumu makubwa ya anayefuata. Na kwamba nchi bado imetulia, katika mazingira haya, ni jambo la kumshukuru Mungu. Siyo automatic. Ni neema ya Mungu.
 
Mama yuko vizuri, pengine hatujamjua vizuri.

Tumpe muda na kumuunga mkono.

Jiwe msalimie Ben Saananne na Mawazo...
Sasa ni wakati wa kuukabili ukweli. Kwetu sisi wengine, inapendeza kupata hewa mpya ya ukweli, kuachana na UNAFIKI, PROPAGANDA, MAPAMBIO na ujinga mwingi unaotia kichefuchefu.
Tulimkosoa sana Kikwete. Hakuwaua au kuwakamata wapinzani au wakosoaji wake. Tunamiss sana uhuru wa kusema tunayofikiri bila kuwa na wasiwasi wa kushughulikiwa
 
Back
Top Bottom