Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,266
- 9,715
Ndugu zangu Watanzania,
Jumamosi ya wiki hii ya Tarehe 27 januari 2024 Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan, mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nuru ya wanyonge na nyota ya matumaini atakuwa anasherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza umri wa miaka 64 tangia alipozaliwa.
Hii ni kwa kuwa Mama yetu Mpendwa alizaliwa Siku ya JUMATANO ya Tarehe 27 januari 1960,mwaka mmoja kabla ya kupata uhuru wa Tanganyika na takribani Miaka minne kabla ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar pamoja na kuzaliwa kwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hii ikiwa na maana kubwa sana kwetu watanzania,kwa kuwa tunaongozwa na kiongozi ambaye anafahamu kwa undani na kwa kina na kwa marefu na kwa ufahamu mpana na uelewa wa hali ya juu sana juu ya wapi nchi yetu imetoka,imepita wapi,imepitia mangapi ,ipo wapi na inapaswa ielekee wapi.
Hii ndio sababu Rais wetu mpendwa Mama Samia amejaa Upendo , uzalendo na uchungu mkubwa sana katika kifua chake juu ya Taifa letu. Ndio maana tunaona namna alivyo na maono makubwa sana juu ya wapi Taifa letu linapaswa kuelekea na kupita. Ndiyo maana hakuna kishindo kinachoweza mtikisa wala mtetemesha wala kumkwamisha katika kuongoza Taifa letu.
Rais Samia anatimiza miaka hiyo huku Taifa likiwa salama katika mikono yake,. wananchi wakiwa na imani kubwa kwake,amani, utulivu na usalama vikiwa vimetamalaki huku kukiwa na umoja, mshikamano,upendo na umoja wa kitaifa. Anatimiza miaka hiyo huku tukiwa tumepiga hatua na kupata maendeleo katika kila sekta,huku tukizungumza lugha moja pasipo ubaguzi wa aina yoyote ile.
Kwa hakika maisha ya Rais Samia hapa Duniani na hapa Nchini yamekuwa neema na baraka kwa watu wengi.maisha yake yameleta nuru, tabasamu na matumaini kwa mamilioni ya watanzania.kwa kuwa ni wakati huu wa uongozi wake ambapo watoto kutoka kaya maskini na za kipato cha chini wana uhakika wa asilimia zote kutimiza ndoto zao za kielimu, kwa kuwa Elimu ni bure mpaka kidato cha sita,huku mikopo kwa Elimu ya juu ikiwa inapatikana na kutolewa kwa wanafunzi wote wenye sifa na kustahili.
Ni wakati wake ambapo sasa kilimo kina thamani na ni shughuli inayolipa na siyo shughuli au kazi ya watu wa kipato cha chini pekee,ni wakati wake ambapo watu wanaona Secta ya afya ilivyofanyiwa mapinduzi makubwa sana.
Ambapo sasa tunatoa hadi madaktari bingwa na bobevu kwenda kutoa huduma za upasuaji wa moyo nchini zambia.Hii ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa katika Secta hii ,Ambapo kwa sasa hospitali ya Apollo ya india ni kama ipo hapa hapa nchini.
Ni chini ya uongozi wake ambapo tumepata mafanikio kila sehemu alipooweka mikono yake,ni kicheko kila sehemu alipopeleka jicho lake,ni matumaini kila sehemu alipoweka neno,ni tabasamu kila eneo alipotoa maagizo,ni furaha kwa Taifa lote kila limtizamapo na ni tabasamu kwa Taifa lote katika nyuso za watanzania.
Kazi iendelee ,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Jumamosi ya wiki hii ya Tarehe 27 januari 2024 Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan, mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nuru ya wanyonge na nyota ya matumaini atakuwa anasherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza umri wa miaka 64 tangia alipozaliwa.
Hii ni kwa kuwa Mama yetu Mpendwa alizaliwa Siku ya JUMATANO ya Tarehe 27 januari 1960,mwaka mmoja kabla ya kupata uhuru wa Tanganyika na takribani Miaka minne kabla ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar pamoja na kuzaliwa kwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hii ikiwa na maana kubwa sana kwetu watanzania,kwa kuwa tunaongozwa na kiongozi ambaye anafahamu kwa undani na kwa kina na kwa marefu na kwa ufahamu mpana na uelewa wa hali ya juu sana juu ya wapi nchi yetu imetoka,imepita wapi,imepitia mangapi ,ipo wapi na inapaswa ielekee wapi.
Hii ndio sababu Rais wetu mpendwa Mama Samia amejaa Upendo , uzalendo na uchungu mkubwa sana katika kifua chake juu ya Taifa letu. Ndio maana tunaona namna alivyo na maono makubwa sana juu ya wapi Taifa letu linapaswa kuelekea na kupita. Ndiyo maana hakuna kishindo kinachoweza mtikisa wala mtetemesha wala kumkwamisha katika kuongoza Taifa letu.
Rais Samia anatimiza miaka hiyo huku Taifa likiwa salama katika mikono yake,. wananchi wakiwa na imani kubwa kwake,amani, utulivu na usalama vikiwa vimetamalaki huku kukiwa na umoja, mshikamano,upendo na umoja wa kitaifa. Anatimiza miaka hiyo huku tukiwa tumepiga hatua na kupata maendeleo katika kila sekta,huku tukizungumza lugha moja pasipo ubaguzi wa aina yoyote ile.
Kwa hakika maisha ya Rais Samia hapa Duniani na hapa Nchini yamekuwa neema na baraka kwa watu wengi.maisha yake yameleta nuru, tabasamu na matumaini kwa mamilioni ya watanzania.kwa kuwa ni wakati huu wa uongozi wake ambapo watoto kutoka kaya maskini na za kipato cha chini wana uhakika wa asilimia zote kutimiza ndoto zao za kielimu, kwa kuwa Elimu ni bure mpaka kidato cha sita,huku mikopo kwa Elimu ya juu ikiwa inapatikana na kutolewa kwa wanafunzi wote wenye sifa na kustahili.
Ni wakati wake ambapo sasa kilimo kina thamani na ni shughuli inayolipa na siyo shughuli au kazi ya watu wa kipato cha chini pekee,ni wakati wake ambapo watu wanaona Secta ya afya ilivyofanyiwa mapinduzi makubwa sana.
Ambapo sasa tunatoa hadi madaktari bingwa na bobevu kwenda kutoa huduma za upasuaji wa moyo nchini zambia.Hii ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa katika Secta hii ,Ambapo kwa sasa hospitali ya Apollo ya india ni kama ipo hapa hapa nchini.
Ni chini ya uongozi wake ambapo tumepata mafanikio kila sehemu alipooweka mikono yake,ni kicheko kila sehemu alipopeleka jicho lake,ni matumaini kila sehemu alipoweka neno,ni tabasamu kila eneo alipotoa maagizo,ni furaha kwa Taifa lote kila limtizamapo na ni tabasamu kwa Taifa lote katika nyuso za watanzania.
Kazi iendelee ,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.