Pages From My JF Diary π
Angalizo kwa watakatifu sitaki mnifokee maana nina nyuzi kibao za maisha na za mijadala ya kijami siwaoni ila hapa mtaanza ooh unapenda ngono
Kwenye jukwaa la chit chat kuna uzi unaitwa JF diary nimeweka nyuzi zangu nyingiiii kama unavutiwa kusoma maandiko yangu ila hili hakikubariki tafadhari tembelea huo uzi na uchague uzi mmoja utakaokuvutia usome kila la kheriππ
Twende nalooo sasa π
Ni vitu gani vikifanyika au ukifanyiwa au ukiona kwa mpenzi wako ukiwa kwa bed vinakukata stim
Au ni vitu gani vikifanyika au ukifanyiwa au kuona kwa bebe wako mizuka inapandaa midadii inakua on...
Mauaji, nini humfanya mtu aamue kumuua mtu mwingine?
Hivi karibuni tumeona visa vya mauaji vikiongezeka, hasa vile vinavyohusishwa na siasa hapa Tanzania.
Kuna maswali mengi yananijia kichwani
Je, haya mauaji hufanywa na mtu mmoja au huwa ni kundi la watu?
Ni nini hutokea kwenye akili ya mtu mpaka afikie hatua ya kumuua binadamu mwenzake?
Mimi binafsi damu inanitisha
Nikiona damu nyingi napata trauma kabisa
Sasa hawa wanaoua, tena kwa ukatili, huwa hawahisi chochote?
Anapomkata mtu, kumpiga risasi au kumchoma moto, halafu yule mtu anaomba msaada au huruma, kweli moyo hauwaumi...
Mara nyingi utasikia watu wakisema, Huyu anatumika na watu fulani, au Huyu anatumiwa tu.
Lakini swali linakuja, kutumika ni nini hasa?
Kipengele A:
Kutumika kwenye mahusiano
Kwenye mahusiano mtu anaweza kutumika kama chombo cha starehe
Yaani hakuna future yoyote, hakuna upendo wa kweli, ila upande mmoja anajua kabisa anachofanya Anaweza kuwa mwanaume au mwanamke
Ugumu unakuja kwa yule anayetumika
Mara nyingi si rahisi kugundua kwa sababu anakuwa amelewa mapenzi
Hisia zinakuwa zimemtawala kiasi kwamba haoni wala hasikii
Hata akionyeshwa na watu wa karibu kuwa anatumika...
Unaweza kutofautisha ukimya na ujeuri?
Kuna msemo unasema Silence is golden
Ni kweli, lakini not every silence is wisdom
Kuna watu wanaonekana ni wakimya, na kweli wanaweza kuwa wakimya kwa asili yao
Ila wakati mwingine sio ukimya tu, bali nyuma ya huo ukimya kuna jeuri, kiburi au dharau
Kwa mfano, huwezi ukasalimiwa halafu ukaamua kukaa kimya, au ukaulizwa jambo ukawa unamtazama mtu bila kujibu, halafu useme eti wewe ni mkimya
Kwa mtazamo wangu huo sio ukimya wa kawaida, huo ni silent disrespect
Kila kitu kina faida na hasara zake
Ukimya una faida nyingi unaweza kukuepusha na...
Hivi ni kweli ni rahisi kulalamika ukiwa nje ya mfumo eti kwa sababu wewe si mnufaika wa moja kwa moja?
Kwa mfano, unaweza kusema mtu fulani ni fisadi. Lakini je, ukipewa nafasi ya huyo mtu, una uhakika kwamba na wewe hutageuka kuwa fisadi?
Mfanoπ
Mtu asiye na kipato anaweza kuapa kwamba yeye hawezi kununua magari ya gharama kubwa kwa sababu anaona ni anasa na ni matumizi ya kupita kiasi
Lakini nadhani wakati huo anakuwa hana uwezo wa kifedha, hivyo huwaona wanaofanya hivyo kama wanafuja mali
Je, ikitokea siku pesa zikamjia, bado atabaki na msimamo huo, au atataka kubebwa...
Unataka au hutaki? π«£
Aliuliza hivi, Darling, itawezekana kweli huu siku upite hivi? π
Mi nikamwambia, Eeh, itawezekana Yes, wewe usijali, lala na utulie
Heh... gafla bin vuu, mkono wake nikausikia unapapasa kifua taratibu Nikamwambia, Hapana, nasikia kizunguzungu, nasikia kama homa hivi(sitaki nataka)
Akaamka taratibu, akachukua tauro, akaloweka kwenye maji, akaanza kunikanda kwenye paji la uso, akashuka mpaka kifuani, ananikanda taratibuπ
Kumbuka hapo tulikubaliana kua je inawezekanaπ
Basi bhana, sijui hata ilikuaje
Kulikua na moment fulani hiviπ
Alikua ananukia perfume fulani...
Katika dunia tunayoishi leo, si rahisi kupata msaada wa kweli wa kihisia kutoka kwa watu
Mara nyingi mtu anapokuwa na changamoto hutamani kuonewa huruma kuambiwa maneno ya faraja, kushikwa mkono, kusaidiwa kifedha au hata kusaidiwa kwa vitendo
Kwa kawaida, msaada huo unaweza kuupata kutoka kwa mtaalamu wa saikolojia, rafiki wa karibu, mpenzi au ndugu
Lakini ukweli ni kwamba hata hao tunaowategemea wana maisha yao na mizigo yao ya kihisia
Wanaweza kuwa wanapitia matatizo makubwa kuliko hata yako
Hali hiyo inaweza kufanya ushindwe kupata kile ulichokitarajia kutoka kwao, na wakati...
SIRIπ€
Ukisikia neno siri unaelewa nini?
Kila mtu ana siri zake asizopenda zifahamike hadharani
Zinaweza kuwa siri nzuri au siri mbaya
Utasikia mtu akisema, Mimi siri zangu nitakufa nazo.
Mara nyingi hii humaanisha kuna mambo aliyoyafanya au anayoyajua ambayo hataki yawekwe wazi kwa sababu yanaweza kuleta aibu, fedheha au madhara kwake
Ndiyo maana anaamua kuzilinda kwa namna yoyote ile zisifahamike.
Umewahi kusikia neno siri za serikali? Au mtu akisema, Mimi nina siri za mtu fulani
Mimi naamini siri zinatofautiana kwa uzito
Ukisikia mtu anakuambia,
Nakueleza ila iwe siri yako...
Kila mwanaume kamili angependa awe na ndugu, kaka, baba au rafiki kama TL.
Na kila mwanamke angependa kuwa na mwanaume, kaka au baba mwenye msimamo kama TL.
Picha Mpya ya Mwanaume
Tundu Antiphas Mughwai Lissuπͺ
Binadamu tuna ndoto, malengo na matamanio mengi kuhusu maisha Tunapanga kuwa na nyumba nzuri, gari, ardhi, biashara na mafanikio mengine mengi
Lakini umewahi kujiuliza kuhusu mwisho wa safari yako?
Umewahi kutamani kifo chako kiwe cha aina fulani?
Mara nyingi husikia watu wakisema,
Yule amekufa kifo kibaya
inasikitisha sanaπ₯²
Hapo unajiuliza, kama kuna kifo kibaya, je, kuna kifo kizuri?
Labda kile kisichoambatana na maumivu makali, mateso ya muda mrefu au taabu nyingi
Je, hicho ndicho kifo kizuri?
Pia, kwa nini kuzungumzia kifo huonekana kama...
Umewahi kuwa in love na mtu lakini ukashindwa kabisa kumwambia? β€οΈ
Ni nini kilikufanya ushindwe kufunguka?
Kwa sisi baby girls, mara nyingi tunaamini ni bora kubaki kimya kuliko kuonekana tunajishusha au kukosa maadili
Au kuhofia tutaonekanaje kwa muhusika na watu wengine
Ndiyo maana wengi huchagua kuficha hisia zao, wakibaki kuonyesha ishara tu huku wakigugumia moyoni
Kama mwanaume hajajiongeza, basi ndiyo hivyo tenaπ€
Kwa wanaume, huonekana ni rahisi zaidi kutupia ndoano, ingawa wapo pia ambao ni madomo zege
Na hawa madomo zege hua wananishangaza hivi nyie wanaume kuna ugumu...
Hivi unajua unaweza kuwa na furaha lakini usisikie utamu?
Au ukasikia utamu lakini huna furaha?
For me, furaha naiona kama ile hali ya moyo kuwa na utulivu na kujisikia vibe fulani hivi yaani ndiyo naiona ni furaha
Then raha, naona kama ni ile hali ya kuhisi uko sawa, huna matatizo
Exp: Labda huumwi, huna msongo wa mawazo, huna madeni, huuguzi
Yaani huna changamoto zinazoweza kukunyima raha
Mimi hutafsiri hivyo
Then utamuuuπ
mimi nauelewa kama ladha nzuri hivi ya kitu
Exp: ukilamba asali utasema, utasema hii asali ni tamu sana!
Kula au kufanya kitu kitamu unaweza ukahisi utamu...
Nimetoka kuoga wakati napaka Lotion nilikua mbele ya kioo gafla nikajiona kwenye kio nikiwa mtupu
Hapo hapo nikajiuliza hivi ingekuaje kama tungekua tunatembea utupu bila nguo hivi maisha yangekuaje?
Nikajiuliza pia hivi ni nani alipata wazo la kuvaa nguo
Aliwaza nini ?
Ni baridi kali ilimsukuma?
Au jua kali kupita kiasi?
Au aibu ?
Kama ni aibu alijuaje hii ni aibu ?
Maana kwa viumbe hai nadhani mwanadamu ndio anavaa nguo
Mada yangu naigawanya sehemu mbili wewe mdau utajibu upande unaopenda
π
Mtazamo wa kidini
Kwa mujibu wa Biblia, baada ya Adamu na Hawa...
Kwenye hii dunia vitu vingi vimeumbwa viwili viwili: binadamu, wanyama, wadudu
Hata kwenye tabia zipo nzuri na zipo mbaya
Watu wapo wema na wapo wabaya
Hapa sina maana ya muonekano wa mtu, I'm talking about character, kwa sababu tabia yako ndiyo itatuambia wewe ni nani, na tabia yangu ndiyo itawaambia mimi ni nani
Sasa je, tabia za nje zinatosha kumjua mtu kuwa ni mbaya au mwema?
Kwa mtazamo wangu jibu ni ndiyo, ila si mara zote tabia ya nje huonyesha kilichopo ndani
Kuna watu wanaonekana wema sana, lakini ndani wamejaa hila
Na kuna watu wanaonekana wakali au wagumu, lakini ndani...
Hivi hii slogan ya nazaa watoto waje kunisaidia imekaaje?
Baadhi ya wazazi, hasa wale wa ukanda wa pwani nilikokulia mimi, utashangaa mzazi anazaa watoto wengi ambao wakati mwingine unaona kabisa uwezo wa kuwalea hana
Ukimuuliza utasikia anasema:
Tajiri na mali zake, maskini na wanawe
Hapo ndipo huwa nashindwa kuelewaπ€
Tajiri ambaye ana uhakika wa chakula bora, elimu bora na matibabu bora mara nyingi unamkuta anazaa watoto wachache
Lakini wewe mwenye kipato kidogo unazaa watoto weeeengi, halafu sababu yako kubwa ni kwamba watakuja kunisaidia baadaye
Hivi kweli hii ni sawa?
Yaani...
Ni nani unaye crush naye hapa jukwaani? π
Hapa jukwaani pamekuwa sehemu ya enjoyment kwa baadhi ya watu, darasa kwa wengine, na sehemu ya kujifunza, kubadilishana mawazo na kufahamiana.
Sasa tuambie ni nani unaye crush naye hapa jukwaani?
Sisemi lazima iwe crush ya kimapenzi No
Inaweza kuwa ni kwa sababu unapenda namna anavyoandika, madini anayotoa, ucheshi wake, namna anavyojenga hoja, au hata comments zake zinavyokuvutia.
Mimi nina crushes wangu wengi tu hapa jukwaani π
Na wewe je, taja wako ni nani, na ni kitu gani hasa kinakufanya umpende au um-appreciate?
ShesRise_1 π€
Shida siyo kudaiwa tu, shida ni unadaiwa na nani?
Mimi roho yangu ni ndogo sana Hata nikidaiwa 50,000 tu siwezi kulala usingizi mpaka nilipe
Nakosa amani kabisa
Twende kwenye mada
Madeni yanaweza kumharibu na kumuathiri mdaiwa kwa kiwango kikubwa kuliko tunavyofikiria, hasa pale anapogundua uwezo wake wa kulipa umekuwa mdogo
Hali inakuwa mbaya zaidi kama anaanza kupokea presha kutoka kwa anayemdai
Yaani kuna watu wanadai vibaya π€£
Baadhi ya madhara ambayo mdaiwa anaweza kuyapata ni:
Kukosa utulivu
Kila akikumbuka ana deni, mood inabadilika
Kutumia muda mwingi kuwaza namna ya...
Natoa angalizo kwa wale wa unashinda JF full-time
Huu ni kama ushauri tu kwamba hii mada inakuhusu isome yote ili uanze leo kupigana na hiyo tabia isiyopendeza ya kufatilia ni nani anaingia online sa ngapi na anatoka saa ngapi
Sisi wengine kuandika ni moja wapo ya enjoyment π
Na hii platform sio kama hizo zingine za kupost makalio au kutafuta attention hapa tulio wengi hatufahamiani
na hii inatupa uhuru wa ku share kujifunza kupiga story na kufurahia maisha kwa mtindo huo
kwa wale wote wanaovutiwa na nyuzi zangu guys nipo in love kwenu π₯° nawapenda sanaππ
Twende zetu sasa π
Mapigano...
Mara nyingi tunasikia baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania zikijinasibu kuwa zinafuata mfumo wa demokrasia
Lakini swali langu ni hili: Je, demokrasia inaonekana kwa vitendo, au ipo kwenye maandishi tu?
Kwa uelewa wangu, demokrasia ya kweli ni pamoja na:
Wananchi kuwa huru kutoa maoni yao bila kubughudhiwa, ilimradi maoni hayo ni ya kujenga na yana tija
Sheria kufanya kazi bila kupindishwa(Mahakama huru)
Wananchi kupiga kura kuchagua viongozi wanaowataka(haki ya msingi)
Sasa mimi najiuliza hapa Tanzania kuna demokrasia?
Kama ndiyo, ni mambo gani yanakufanya uamini kuwa demokrasia ipo...