ShesRise_1
JF-Expert Member
- Aug 21, 2025
- 17,478
- 41,419
Kwenye hii dunia vitu vingi vimeumbwa viwili viwili: binadamu, wanyama, wadudu
Hata kwenye tabia zipo nzuri na zipo mbaya
Watu wapo wema na wapo wabaya
Hapa sina maana ya muonekano wa mtu, I'm talking about character, kwa sababu tabia yako ndiyo itatuambia wewe ni nani, na tabia yangu ndiyo itawaambia mimi ni nani
Sasa je, tabia za nje zinatosha kumjua mtu kuwa ni mbaya au mwema?
Kwa mtazamo wangu jibu ni ndiyo, ila si mara zote tabia ya nje huonyesha kilichopo ndani
Kuna watu wanaonekana wema sana, lakini ndani wamejaa hila
Na kuna watu wanaonekana wakali au wagumu, lakini ndani wana mioyo safi sana
Lakini ukweli ni kwamba, actions speak louder than words
Mwisho wa siku tutakutambua kwa matendo yako
Sasa ni matendo gani ukiyaona kwa mtu unahitimisha kuwa huyu ni mtu mwema?
Kwangu mimi, mtu mwema nampima kwanza kwa upendo alionao kwa wengine
Mtu mwema mara nyingi habebi chuki wala roho mbaya kwa wengine
Mara nyingi watu wema huwa watulivu wanapoamua mambo, kwa sababu wanaamini wakifanya haraka wanaweza kusababisha matatizo au hasara kwa wengine
Watu wema hujali hisia za wengine Kama hawezi kukusaidia, mara nyingi hayupo tayari kukuumiza au kukupa matatizo
Mtu mwema hufurahia kuona wengine wakifanikiwa
Akiona mwenzake amepiga hatua hasemi
(Kwa nini yeye?)Badala yake anasema, Hongera🤗
Anaamini mafanikio ya mwingine hayapunguzi nafasi yake
Mtu mwema akimkosea mtu huwa yupo tayari kuomba msamaha
Na akikosolewa hasikii vibaya kila wakati, kwa sababu anajua hakuna binadamu mkamilifu
Kwa hiyo ukipata mtu wa aina hii kwenye maisha yako, usimchukulie poa
Watu wema ni wachache kuliko tunavyofikiri
Mara nyingi huwa ndiyo watu wanaokupa amani ya moyo wanakushauri kwa faida yako hata kama ukweli unauma wanakuombea mema hata ukiwa haupo nao, na wanabaki upande wako hata pale ambapo hawapati faida yoyote kutoka kwako
Ukiwa na mtu mwema karibu yako, mara nyingi unajikuta hata wewe unabadilika na kuwa mtu bora zaidi Positive people create positive lives
👇
Sasa twende kwa mtu mbaya...
Mtu mbaya mara nyingi hubeba chuki dhidi ya wengine
Moyo wake huwa kama umekufa ganzi, hana anachojali kuhusu wengine
Hata kama hana cha kukusaidia, atafanya juu chini akupe maumivu
Mtu mbaya marafiki zake ni unafiki, uchonganishi, umbeya, ubinafsi, chuki na husda
Mtu mbaya hataki kuona wenzake wakifanya vizuri
Anataka yeye ndiye awe top kwenye kila kitu
Akiona wenzie wanasifiwa, roho inamnyonga akiamini hawastahili
Hufurahia maanguko ya watu
Yule alikuwa anajidai, sasa amekuwa kama sisi kiko wapi🤣
Mtu mbaya hubeba chuki ambayo mwisho wa siku hummaliza yeye mwenyewe kidogo kidogo
Lakini pia ni hatari kua karibu yake maana chuki aliyoificha ndani akiitoa njee ni majanga
Anaweza kutabasamu mbele yako, lakini ndani anateseka kwa sababu tu huwezi kuanguka kama anavyotamani
Na kitu kingine nilichokiona, mtu mbaya huwa ni mgumu sana kufurahia mafanikio ya wengine
Kila zuri analigeuza baya kila mafanikio anaona kuna mchezo umefanyika utasikia
(hapa si bure kuna kitu)
Shida ya kuwa karibu na mtu wa aina hii ni kwamba taratibu utaanza kupoteza amani yako bila kujua
Atakuvuruga kisaikolojia, atakufanya uwaone wengine wabaya kama yeye, atakukatisha tamaa kila unapopiga hatua na wakati mwingine anaweza kuwa sababu ya wewe kuharibu mahusiano yako na watu wasiokuwa na kosa
Watu wabaya hua pia wanapenda wakikosana na watu na wewe eti ukosane nao pia hua wanapenda kurithisha uadui🤣🤣
Watu wa aina hii wakishindwa kukutumia, wanaanza kukuchafua Ndiyo maana kuna msemo unasema, show me your friends and I'll tell you who you are
Mara nyingi tabia huambukiza, hivyo ukikaa sana na mtu mwenye roho mbaya bila kuwa makini, unaweza kujikuta unaanza kufanana naye bila hata kugundua
Sasa hapo tumeona baadhi ya tabia za watu wema na watu wabaya na huo ni mtazamo wangu
Wewe ongezea...
Ni tabia gani ukiiona kwa mtu unaamini kabisa huyu ni mtu mwema?
Na ni tabia gani ukiiona unaona huyu ana roho mbaya?
Halafu ukijipima wewe mwenyewe, kwa tabia zako za ndani na nje unajiona upo upande gani?
Happy Tuesday 😊
ShesRise_1 ✋️
Hata kwenye tabia zipo nzuri na zipo mbaya
Watu wapo wema na wapo wabaya
Hapa sina maana ya muonekano wa mtu, I'm talking about character, kwa sababu tabia yako ndiyo itatuambia wewe ni nani, na tabia yangu ndiyo itawaambia mimi ni nani
Sasa je, tabia za nje zinatosha kumjua mtu kuwa ni mbaya au mwema?
Kwa mtazamo wangu jibu ni ndiyo, ila si mara zote tabia ya nje huonyesha kilichopo ndani
Kuna watu wanaonekana wema sana, lakini ndani wamejaa hila
Na kuna watu wanaonekana wakali au wagumu, lakini ndani wana mioyo safi sana
Lakini ukweli ni kwamba, actions speak louder than words
Mwisho wa siku tutakutambua kwa matendo yako
Sasa ni matendo gani ukiyaona kwa mtu unahitimisha kuwa huyu ni mtu mwema?
Kwangu mimi, mtu mwema nampima kwanza kwa upendo alionao kwa wengine
Mtu mwema mara nyingi habebi chuki wala roho mbaya kwa wengine
Mara nyingi watu wema huwa watulivu wanapoamua mambo, kwa sababu wanaamini wakifanya haraka wanaweza kusababisha matatizo au hasara kwa wengine
Watu wema hujali hisia za wengine Kama hawezi kukusaidia, mara nyingi hayupo tayari kukuumiza au kukupa matatizo
Mtu mwema hufurahia kuona wengine wakifanikiwa
Akiona mwenzake amepiga hatua hasemi
(Kwa nini yeye?)Badala yake anasema, Hongera🤗
Anaamini mafanikio ya mwingine hayapunguzi nafasi yake
Mtu mwema akimkosea mtu huwa yupo tayari kuomba msamaha
Na akikosolewa hasikii vibaya kila wakati, kwa sababu anajua hakuna binadamu mkamilifu
Kwa hiyo ukipata mtu wa aina hii kwenye maisha yako, usimchukulie poa
Watu wema ni wachache kuliko tunavyofikiri
Mara nyingi huwa ndiyo watu wanaokupa amani ya moyo wanakushauri kwa faida yako hata kama ukweli unauma wanakuombea mema hata ukiwa haupo nao, na wanabaki upande wako hata pale ambapo hawapati faida yoyote kutoka kwako
Ukiwa na mtu mwema karibu yako, mara nyingi unajikuta hata wewe unabadilika na kuwa mtu bora zaidi Positive people create positive lives
👇
Sasa twende kwa mtu mbaya...
Mtu mbaya mara nyingi hubeba chuki dhidi ya wengine
Moyo wake huwa kama umekufa ganzi, hana anachojali kuhusu wengine
Hata kama hana cha kukusaidia, atafanya juu chini akupe maumivu
Mtu mbaya marafiki zake ni unafiki, uchonganishi, umbeya, ubinafsi, chuki na husda
Mtu mbaya hataki kuona wenzake wakifanya vizuri
Anataka yeye ndiye awe top kwenye kila kitu
Akiona wenzie wanasifiwa, roho inamnyonga akiamini hawastahili
Hufurahia maanguko ya watu
Yule alikuwa anajidai, sasa amekuwa kama sisi kiko wapi🤣
Mtu mbaya hubeba chuki ambayo mwisho wa siku hummaliza yeye mwenyewe kidogo kidogo
Lakini pia ni hatari kua karibu yake maana chuki aliyoificha ndani akiitoa njee ni majanga
Anaweza kutabasamu mbele yako, lakini ndani anateseka kwa sababu tu huwezi kuanguka kama anavyotamani
Na kitu kingine nilichokiona, mtu mbaya huwa ni mgumu sana kufurahia mafanikio ya wengine
Kila zuri analigeuza baya kila mafanikio anaona kuna mchezo umefanyika utasikia
(hapa si bure kuna kitu)
Shida ya kuwa karibu na mtu wa aina hii ni kwamba taratibu utaanza kupoteza amani yako bila kujua
Atakuvuruga kisaikolojia, atakufanya uwaone wengine wabaya kama yeye, atakukatisha tamaa kila unapopiga hatua na wakati mwingine anaweza kuwa sababu ya wewe kuharibu mahusiano yako na watu wasiokuwa na kosa
Watu wabaya hua pia wanapenda wakikosana na watu na wewe eti ukosane nao pia hua wanapenda kurithisha uadui🤣🤣
Watu wa aina hii wakishindwa kukutumia, wanaanza kukuchafua Ndiyo maana kuna msemo unasema, show me your friends and I'll tell you who you are
Mara nyingi tabia huambukiza, hivyo ukikaa sana na mtu mwenye roho mbaya bila kuwa makini, unaweza kujikuta unaanza kufanana naye bila hata kugundua
Sasa hapo tumeona baadhi ya tabia za watu wema na watu wabaya na huo ni mtazamo wangu
Wewe ongezea...
Ni tabia gani ukiiona kwa mtu unaamini kabisa huyu ni mtu mwema?
Na ni tabia gani ukiiona unaona huyu ana roho mbaya?
Halafu ukijipima wewe mwenyewe, kwa tabia zako za ndani na nje unajiona upo upande gani?
Happy Tuesday 😊
ShesRise_1 ✋️