ShesRise_1
JF-Expert Member
- Aug 21, 2025
- 17,287
- 40,946
Hivi ni kweli ni rahisi kulalamika ukiwa nje ya mfumo eti kwa sababu wewe si mnufaika wa moja kwa moja?
Kwa mfano, unaweza kusema mtu fulani ni fisadi. Lakini je, ukipewa nafasi ya huyo mtu, una uhakika kwamba na wewe hutageuka kuwa fisadi?
Mfano👇
Mtu asiye na kipato anaweza kuapa kwamba yeye hawezi kununua magari ya gharama kubwa kwa sababu anaona ni anasa na ni matumizi ya kupita kiasi
Lakini nadhani wakati huo anakuwa hana uwezo wa kifedha, hivyo huwaona wanaofanya hivyo kama wanafuja mali
Je, ikitokea siku pesa zikamjia, bado atabaki na msimamo huo, au atataka kubebwa kichwani na hataki hata kukanyaga ardhi?
Hii ina maana gani?
Je, mara nyingi watu hulalamika kwa sababu wako nje ya mfumo na hawanufaiki nao?
Mwisho kabisa, kama ni kweli kwamba binadamu anaweza kubadilika anapoingia kwenye mfumo wa madaraka au kunufaika nao, ni mfumo gani imara unapaswa kuwekwa ili kuzuia tabia ya (kulamba asali? )
Kama tatizo ni mfumo Je
Mfumo gani unaweza kuwafanya viongozi wasijisahau wanapopewa madaraka na wasije wakafanya yale yale waliyokuwa wanawakosoa waliowatangulia?
NB: Sina chama chochote
Lakini napenda nchi yenye ustawi bora
ShesRise_1 🤚
Kwa mfano, unaweza kusema mtu fulani ni fisadi. Lakini je, ukipewa nafasi ya huyo mtu, una uhakika kwamba na wewe hutageuka kuwa fisadi?
Mfano👇
Mtu asiye na kipato anaweza kuapa kwamba yeye hawezi kununua magari ya gharama kubwa kwa sababu anaona ni anasa na ni matumizi ya kupita kiasi
Lakini nadhani wakati huo anakuwa hana uwezo wa kifedha, hivyo huwaona wanaofanya hivyo kama wanafuja mali
Je, ikitokea siku pesa zikamjia, bado atabaki na msimamo huo, au atataka kubebwa kichwani na hataki hata kukanyaga ardhi?
Hii ina maana gani?
Je, mara nyingi watu hulalamika kwa sababu wako nje ya mfumo na hawanufaiki nao?
Mwisho kabisa, kama ni kweli kwamba binadamu anaweza kubadilika anapoingia kwenye mfumo wa madaraka au kunufaika nao, ni mfumo gani imara unapaswa kuwekwa ili kuzuia tabia ya (kulamba asali? )
Kama tatizo ni mfumo Je
Mfumo gani unaweza kuwafanya viongozi wasijisahau wanapopewa madaraka na wasije wakafanya yale yale waliyokuwa wanawakosoa waliowatangulia?
NB: Sina chama chochote
Lakini napenda nchi yenye ustawi bora
ShesRise_1 🤚