ShesRise_1
JF-Expert Member
- Aug 21, 2025
- 17,694
- 42,055
Mara nyingi utasikia watu wakisema, Huyu anatumika na watu fulani, au Huyu anatumiwa tu.
Lakini swali linakuja, kutumika ni nini hasa?
Kipengele A:
Kutumika kwenye mahusiano
Kwenye mahusiano mtu anaweza kutumika kama chombo cha starehe
Yaani hakuna future yoyote, hakuna upendo wa kweli, ila upande mmoja anajua kabisa anachofanya Anaweza kuwa mwanaume au mwanamke
Ugumu unakuja kwa yule anayetumika
Mara nyingi si rahisi kugundua kwa sababu anakuwa amelewa mapenzi
Hisia zinakuwa zimemtawala kiasi kwamba haoni wala hasikii
Hata akionyeshwa na watu wa karibu kuwa anatumika, mara nyingi haamini
Anaona anaonewa wivu, wanamchonganisha au hawataki kuona akifurahia mahusiano yake
Lakini siku akigundua ukweli, mara nyingi anakuwa tayari kapotezewa muda, kaumizwa na kuchezewa hisia
Ndipo huanza kurudisha kumbukumbu nyuma na kukumbuka vitu vidogo vidogo vilivyokuwa kama red flags, lakini kipindi kile hakuweza kuviona kwa sababu hisia zilikuwa zimemtawala
Kipengele B:
Kutumika kufanya uhalifu au kutimiza ajenda za wengine
Mtu anaweza pia kutumika kufanya uhalifu au kutimiza malengo ya watu wengine
Anaweza akawa anajua anachokifanya,
lakini pia anaweza akawa hatambui kabisa kuwa anatumika
Mimi naongelea zaidi yule anayetumika bila kujua
Mara nyingi watu wanaowatumia wenzao huwa smart sana
Wanajua namna ya kukufanya uwaamini
Wanaweza kukuonyesha upendo, kukujali, kukusaidia au kukupa nafasi mpaka uanze kuona hawawezi kuwa na nia mbaya(Fake treatment)
Watu wa pembeni wanaweza kuona mapema kwamba unatumika na wakajaribu kukuambia, lakini mara nyingi ni vigumu kuamini
Unaona kama wanakuhukumu vibaya au wanataka kukuchonganisha
Mpaka siku wale waliokuwa wanakutumia wanapomaliza kile walichokuwa wanakitaka, ndipo wanakuacha ukatupwa kama toilet paper hapo akili inarudi
Sasa hapo ndipo unaanza kukumbuka maneno ya watu waliokuwa wanakuonya, lakini yanakuwa hayana msaada tena()
Unaanza kuunganisha matukio na kukumbuka zile ishara ndogo ndogo ulizopuuzia, ukitambua kwamba zilikuwa ni red flags lakini lahaulaaa umechelewa tayari
Swali la mjadala
Kwa maoni yako, mtu anawezaje kugundua kuwa anatumika?
Ni dalili zipi ukiziona unaweza kusema
Hapa kuna kitu si sawa, nahisi natumika
Iwe kwenye:
1 Mahusiano
2 Kazi.
3 Siasa
4 Urafiki
5 Au maisha kwa ujumla
Karibuni tushirikishane mawazo na uzoefu
Huenda majibu yako yakamsaidia mtu kugundua mapema kuwa anatumika kabla hajachelewa
Midnight:02
ShesRise_1 🤚
Lakini swali linakuja, kutumika ni nini hasa?
Kipengele A:
Kutumika kwenye mahusiano
Kwenye mahusiano mtu anaweza kutumika kama chombo cha starehe
Yaani hakuna future yoyote, hakuna upendo wa kweli, ila upande mmoja anajua kabisa anachofanya Anaweza kuwa mwanaume au mwanamke
Ugumu unakuja kwa yule anayetumika
Mara nyingi si rahisi kugundua kwa sababu anakuwa amelewa mapenzi
Hisia zinakuwa zimemtawala kiasi kwamba haoni wala hasikii
Hata akionyeshwa na watu wa karibu kuwa anatumika, mara nyingi haamini
Anaona anaonewa wivu, wanamchonganisha au hawataki kuona akifurahia mahusiano yake
Lakini siku akigundua ukweli, mara nyingi anakuwa tayari kapotezewa muda, kaumizwa na kuchezewa hisia
Ndipo huanza kurudisha kumbukumbu nyuma na kukumbuka vitu vidogo vidogo vilivyokuwa kama red flags, lakini kipindi kile hakuweza kuviona kwa sababu hisia zilikuwa zimemtawala
Kipengele B:
Kutumika kufanya uhalifu au kutimiza ajenda za wengine
Mtu anaweza pia kutumika kufanya uhalifu au kutimiza malengo ya watu wengine
Anaweza akawa anajua anachokifanya,
lakini pia anaweza akawa hatambui kabisa kuwa anatumika
Mimi naongelea zaidi yule anayetumika bila kujua
Mara nyingi watu wanaowatumia wenzao huwa smart sana
Wanajua namna ya kukufanya uwaamini
Wanaweza kukuonyesha upendo, kukujali, kukusaidia au kukupa nafasi mpaka uanze kuona hawawezi kuwa na nia mbaya(Fake treatment)
Watu wa pembeni wanaweza kuona mapema kwamba unatumika na wakajaribu kukuambia, lakini mara nyingi ni vigumu kuamini
Unaona kama wanakuhukumu vibaya au wanataka kukuchonganisha
Mpaka siku wale waliokuwa wanakutumia wanapomaliza kile walichokuwa wanakitaka, ndipo wanakuacha ukatupwa kama toilet paper hapo akili inarudi
Sasa hapo ndipo unaanza kukumbuka maneno ya watu waliokuwa wanakuonya, lakini yanakuwa hayana msaada tena()
Unaanza kuunganisha matukio na kukumbuka zile ishara ndogo ndogo ulizopuuzia, ukitambua kwamba zilikuwa ni red flags lakini lahaulaaa umechelewa tayari
Swali la mjadala
Kwa maoni yako, mtu anawezaje kugundua kuwa anatumika?
Ni dalili zipi ukiziona unaweza kusema
Hapa kuna kitu si sawa, nahisi natumika
Iwe kwenye:
1 Mahusiano
2 Kazi.
3 Siasa
4 Urafiki
5 Au maisha kwa ujumla
Karibuni tushirikishane mawazo na uzoefu
Huenda majibu yako yakamsaidia mtu kugundua mapema kuwa anatumika kabla hajachelewa
Midnight:02
ShesRise_1 🤚