Status
Not open for further replies.
Natumia nafasi hii kama ilivyoelezwa kwenye katiba ya jamhuri wa muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kifungu cha 18, kipengele cha kwanza ambayo inasomeka hivi nanukuu:
18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
Mwisho wa kunukuu.

Natumia haki yangu ya kikatiba kama inavyoeleza hapo juu kumshauri rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ambaye ni ndugu John Magufuli, kuendelea kudumisha, kuimarisha na kujenga umoja wa kitaifa katika taifa ambalo watanzania sote tulizoea kuishi kwa upendo kama ndugu kwa kuvumiliana na kusikilizana hivyo kushiriki katika umoja wetu huo ulioasisiwa na Mwalimu Nyerere katika ujenzi wa taifa letu pendwa vizuri.

Siku zinavyozidi kwenda mbele inedhihirika wazi ule umoja wa kitaifa unasambaratika kwa spidi kali sana na kupotea.
Natoa mfano kwa visa nilivyoshuhudia nikiwa hapa Tanzania, mie ni mkazi wa kijijini sasa kuna sehemu ambako wazee kwa vijana, walikuwa wanakutana kupata supu hapa kijijini kabla wewe rais hujaingia madarakani lakini ulipochukua tu madaraka pametokea mgawanyiko mkubwa sana uliosababishwa na chuki zinazohubiriwa na watawala wa awamu hii na wewe ukiwemo.

Sasa kile kibanda cha supu kimechomwa moto na watu wasojulikana na watu hawachangamani tena kwa pamoja ila wanakaa kusikojulikana kutegemea na mlengo wao wa kisiasa yani mwanachama wa chama A, atakaa na wa chama A wenzake na yule wa chama B atakaa na wa chama B wenzake. Mambo hayakuwahi kufikia hatua hii hapo awali kabla yako madarakani hakika kama taifa tunaelekea kusikojulikana ndugu rais.

Siyo hivyo tu nachosikitika zaidi ni huku kijijini tulikuwa na utamaduni wa kusaidiana kwa hali na mali bila kujali itikadi zetu za aina yoyote ile, lakini ulipoingia madarakani hali imekuwa tofauti sasa watu wanasaidiana kwa itikadi zao za kisiasa tu.
Nimeshuhudia babu yangu akikataa kumuazimisha kitu jirani yake tena kwa kumkaripia kwa maneno makali kuwa jirani yake ni mwanachama wa chama cha kisiasa tofauti na chake hawezi kumsaidia na asimsumbue tena siku nyingine aende kwa wenzake wa chama chake. Hii ni hatari sana watanzania tumefika pabaya.

Nakushauri rais nusuru hii hali kwa kunusuru umoja wetu wa kitaifa, unda kamati ya maridhiano ikijumuisha wakuu wa vyama vya siasa nchini, viongozi wa kidini yani wachungaji, mashehe na maaskofu, watu kutoka asasi za kiraia nk ili kujadili kwa pamoja ili turudishe umoja wetu wa kitaifa tuliozoea kuwa nao hapo awali.

Tanzania ni nchi yetu sote na machafuko yakitokea tutakaoumia ni sisi watanzania siyo watu wa Rwanda au Burundi.
Tutaumia sisi watanzania.

Mungu ibariki Tanzania ,
Mungu ibariki Afrika.

NB:
Natumaini ushauri wangu utakufikia na utachukua hatua.
Lakini naomba univumilie kama nitakuwa nimekukwaza ndugu rais.
Haujihisi kuwashwawashwa hivi?
anyway...

haudhani pia kuwa ile kauli ya TUSIPANGIANE bado ipo na inakuhusu?

umesema unamshauri kwa mujibu wa katiba?...unadhani vyama vya siasa vimezuiwa kufanya siasa kwa katiba ipi...ni hiyohiyo unayotumia wewe au kuna nyingine inayotumika wewe huna?

...kuwa makini we are not usingvthat katiba ...not to that extent.
 
Japo kuwa mimi si MLENGWA wa hoja yako, nitasema ushauri wako ni mzuri tu kama raia mwema wa nchi yetu hii..

ISIPOKUWA umenishangaza kidogo kusikia kuwa watu vijijini WANANYIMANA hata chumvi ama MISAADA kama jirani kwa sababu ya ITIKADI za kisiasa.
Ningependa kuuliza yafuatayo:

1.Je mkuu huu unaweza kuwa ni UKWELI kabisa ama ni kuongeza chumvi katika hoja yako?
Ama mimi naishi nchi nyingine?

2. Mbona mimi SIJASIKIA?
3. Je Hicho kijiji unachotoka kwani HAMNA serikali?
Hata ya Wenyeviti wa VITONGOJI ili kutatua matatizo kama hayo?. Kwangu Hii haingii akilini.

Ila NAKUBALIANA nawe kwa jambo moja kuwa,
WANASIASA wote wanahitajika kuhubiri AMANI na UMOJA bila kubaguana kwa misingi ya itikadi za KISIASA KIDINI ama VYAMA.
Nchi ni MUHIMU sana kuliko CHAMA chochote kile wala MWANASIASA yeyote yule!.
kuna msemo wa waswahili wanasema" TEMBEA UONE "
sasa mkuu uko nyuma ya keyboard utasikiaje na kuona?
 
chuki imekuwa kwa kiwango cha juu sana yani we fahamu hapa sasa wanakijiji wamefikia hatua ya jino kwa jino na we ukienda kuazima kitu kwa wa itikadi tofauti na yako utafukuzwa kama mbwa mwizi.

Viongozi kila uchao wanahubiri chuki
Kijiji ama sehemu za wapi mkuu ?
Ili nijenge PICHA
 
Hashauriki. Yeye ndiye anashauri washauri wake.

I am serious. Kunamtu anaitwa Lawrence Mafuru alimshauri kwamba kuingilia mzunguko wa fedha kiholela ni kitu kitakachoharibu uchumi.

Hakusikia. Kamtoa kazini Hazina.

Leo kafanya anavyoona yeye bila kufuata ushaur, alichoonya Lawrence Mafuru kimetokea, mzunguko wa fedha umeharibika,uchumiunadidimia.

Lawrence Mafuru ni banker anayeheshimika anajulikana mpaka City of London. Youko Registered kwenye charted yao ya bankers huko.

Hakumsikiliza.

Atakusikiliza wewe hapa JF?
Kama rais amekuwa hivi basi hatuna budi kumkumbusha ya wahenga asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
 
juzi wanachadema walienda kuchangia damu hospitali mbona walizuiwa kisa tu damu inatoka kwa wafuasi wa chadema hilo nalo geni kwako?
Mkuu, hata mimi sikuelewa ni kwa nini.Labda vyombo husika walikuwa na sababu zao kwa nini walikatazwa. Pengine, na nasema PENGINE labda kutoa damu ilikuwa ni COVER UP ya kitu kingine tofauti na utoaji wa damu. Mimi sijui.
 
Japo kuwa mimi si MLENGWA wa hoja yako, nitasema ushauri wako ni mzuri tu kama raia mwema wa nchi yetu hii..

ISIPOKUWA umenishangaza kidogo kusikia kuwa watu vijijini WANANYIMANA hata chumvi ama MISAADA kama jirani kwa sababu ya ITIKADI za kisiasa.
Ningependa kuuliza yafuatayo:

1.Je mkuu huu unaweza kuwa ni UKWELI kabisa ama ni kuongeza chumvi katika hoja yako?
Ama mimi naishi nchi nyingine?

2. Mbona mimi SIJASIKIA?
3. Je Hicho kijiji unachotoka kwani HAMNA serikali?
Hata ya Wenyeviti wa VITONGOJI ili kutatua matatizo kama hayo?. Kwangu Hii haingii akilini.

Ila NAKUBALIANA nawe kwa jambo moja kuwa,
WANASIASA wote wanahitajika kuhubiri AMANI na UMOJA bila kubaguana kwa misingi ya itikadi za KISIASA KIDINI ama VYAMA.
Nchi ni MUHIMU sana kuliko CHAMA chochote kile wala MWANASIASA yeyote yule!.
Km ni msikivu ayafanyie haya, ni ukweli usiopingika mioyo ya watu wengi imejaa chuki, hasira juu ya matukio ya ovyo yanayoendelea Humu nchini
 
Kashakumbushwa mpaka sasa mara nyingi sana,hasikii.

Zaidi anawakaripia wazee wastaafu waliofanya kazi kabla yakekuja mjini. Wakimkumbusha anasema wanawashwa washwa.

Ukimkumbusha sana anaweza kukutumia"watu wasiojulikana" bure.

“Wastaafu wengine wanawashwa washwa” - Magufuli | East Africa Television
Ikifikia hatua ya kunitumia watu wasiojulikana mie nitajificha kusikojulikana lakini wasiwasi wangu ni tunaeza kuwa taifa la watu wasiojulikana linaloelekea kusikojulikana.
 
Natumia nafasi hii kama ilivyoelezwa kwenye katiba ya jamhuri wa muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kifungu cha 18, kipengele cha kwanza ambayo inasomeka hivi nanukuu:
18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
Mwisho wa kunukuu.

Natumia haki yangu ya kikatiba kama inavyoeleza hapo juu kumshauri rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ambaye ni ndugu John Magufuli, kuendelea kudumisha, kuimarisha na kujenga umoja wa kitaifa katika taifa ambalo watanzania sote tulizoea kuishi kwa upendo kama ndugu kwa kuvumiliana na kusikilizana hivyo kushiriki katika umoja wetu huo ulioasisiwa na Mwalimu Nyerere katika ujenzi wa taifa letu pendwa vizuri.

Siku zinavyozidi kwenda mbele inedhihirika wazi ule umoja wa kitaifa unasambaratika kwa spidi kali sana na kupotea.
Natoa mfano kwa visa nilivyoshuhudia nikiwa hapa Tanzania, mie ni mkazi wa kijijini sasa kuna sehemu ambako wazee kwa vijana, walikuwa wanakutana kupata supu hapa kijijini kabla wewe rais hujaingia madarakani lakini ulipochukua tu madaraka pametokea mgawanyiko mkubwa sana uliosababishwa na chuki zinazohubiriwa na watawala wa awamu hii na wewe ukiwemo.

Sasa kile kibanda cha supu kimechomwa moto na watu wasojulikana na watu hawachangamani tena kwa pamoja ila wanakaa kusikojulikana kutegemea na mlengo wao wa kisiasa yani mwanachama wa chama A, atakaa na wa chama A wenzake na yule wa chama B atakaa na wa chama B wenzake. Mambo hayakuwahi kufikia hatua hii hapo awali kabla yako madarakani hakika kama taifa tunaelekea kusikojulikana ndugu rais.

Siyo hivyo tu nachosikitika zaidi ni huku kijijini tulikuwa na utamaduni wa kusaidiana kwa hali na mali bila kujali itikadi zetu za aina yoyote ile, lakini ulipoingia madarakani hali imekuwa tofauti sasa watu wanasaidiana kwa itikadi zao za kisiasa tu.
Nimeshuhudia babu yangu akikataa kumuazimisha kitu jirani yake tena kwa kumkaripia kwa maneno makali kuwa jirani yake ni mwanachama wa chama cha kisiasa tofauti na chake hawezi kumsaidia na asimsumbue tena siku nyingine aende kwa wenzake wa chama chake. Hii ni hatari sana watanzania tumefika pabaya.

Nakushauri rais nusuru hii hali kwa kunusuru umoja wetu wa kitaifa, unda kamati ya maridhiano ikijumuisha wakuu wa vyama vya siasa nchini, viongozi wa kidini yani wachungaji, mashehe na maaskofu, watu kutoka asasi za kiraia nk ili kujadili kwa pamoja ili turudishe umoja wetu wa kitaifa tuliozoea kuwa nao hapo awali.

Tanzania ni nchi yetu sote na machafuko yakitokea tutakaoumia ni sisi watanzania siyo watu wa Rwanda au Burundi.
Tutaumia sisi watanzania.

Mungu ibariki Tanzania ,
Mungu ibariki Afrika.

NB:
Natumaini ushauri wangu utakufikia na utachukua hatua.
Lakini naomba univumilie kama nitakuwa nimekukwaza ndugu rais.
Rais wako katumwa na Kagame ili kuiharibu Tanzania yaani haivuruge ili itokee vita na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe ndio itakuwa furaha ya Kagame na Magufuli atakimbilia Rwanda mara atakapoona tunaanza kuchinjana. Ameshaanza kujengewa palace nchini Rwanda. Magufuli anataka kuiaribu Tanzania iliyokuwa na amani tele na anaiaribu kutokana na umaskini wa baadhi ya watanzania walio wengi na wasiokuwa na elimu. Kwani asingetumwa na Kagame asingefanya haya anayoyafanya sasa rais wa nchi hawezi kusema kuwa mwanaccm asimsalimie ndg yake au mtoto wake alieko opposition. Mfano mnao alivyotaka kumvua ubunge mtoto wa Bulembo kisa ameolewa na Zito
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom