RAIS SAMIA SULUHU NI NYOTA INAYONG'AA

Uweledi katika kuitekeleza diplomasia ya uchumi, mageuzi katika kuvutia wawekezaji na mazingira rafiki ya kuweza kufanya biashara nchini Tanzania. Leo hii wakati watanzania wanahitimisha maombolezo ya Hayati Magufuli ni hakika nyota njema imeonekana, Hotuba ya Mh.Rais Samia imetoa dira yenye tumaini.

Ujasiri, uthubutu, na misingi ya kiutawala aliyoisisitiza katika umuhimu wa kukusanya mapato kwa kufuata taratibu na sheria. Uwezo wa kuzingatia taaluma na ubobezi katika kuteua wasaidizi ni hakika Mh.Samia Suluhu ni kiongozi wa aina ya kipekee atakayeweza kuijenga Tanzania bora yenye uchumi jumuishi na endelevu.
 
Mama naye ndo yale yale makufuli ya China
Screenshot_2021-04-08-09-36-57.jpg
 
Habarini wa jf wenzangu.

Hayati rais magufuli kaiacha tanzania yenye mafanikio. Majawapo ni kua uchumi wa kati.

Mafanikio hayo pamoja na juhudi za wananchi, yametufanya tufahamike na tukue kiuchumi. Pia, mawaziri na watendaji wote wa rais, wamechangia sehemu kubw sana ya mafanikio hayo.

huyu rais wetu mpya ameanza vizuri, lkn akiendelea na teuzi/tenguzi nyingine, anatoa picha ni namna gani asivyotambua ugumu wa kazi iliyopo mbele.

Anajukumu, la kuhakikisha tabakia kua uchumi wa kati na kuendelea kukua zaidi kiuchumi. Wateule anaowatoa, ndio ambao wangemsaidia kufikia malengo hayo kwasababu wanauzoefu wa kutosha kutoka awamu iliyopita.

Akiendelea na tabia hii mpya, sitoshangaa kusikia tanzania tupo kundi la nchi masikini tena.
 
Siku 21 za Maombolezo ya Rais wetu Mpendwa Dr. John Pombe Magufuli yalikamilika siku ya Jumanne, tarehe 6 April 2021. Life goes on kwa Watanzania wengi na sina shaka Magufuli legacy will live on forever kwa taifa hili la Watanzania na kwa wapenda haki wote. Rip Dr. John Joseph Pombe Magufuli.

Tunaye Rais mpya sasa, Mama Samia Suluhu Hassan, aliyechujua madaraka kufuatia kifo cha Rais Magufuli. Mama huyu hakuwa ameota kwamba siku moja angekuwa Makamu wa Rais, let alone kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa hiyo mategemeo yangu kwake siyo makubwa sana, lakini namtakia kila la heri kwa sababu akifaulu, Tanzania imefaulu na akifeli, Tanzania imefeli. What surprises me the most kuhusu Rais Samia ni jinsi anavyotaka kujitenga na yale yanaitwa mabaya ya Maguguli,lakini akichukua credit kwa mazuri yote. Kote duniani, wanasema you dont speak ill of the dead, kwa kuamini kwamba utakachokisema chochote kibaya kwa mtu aliyekufa, hayupo kujisemea mwenyewe ama kujitetea, so it is a rule of thumb, huwasemi vibaya waliokufa.

Huyu mama anaonekana hili halijui. Ameanza kwa ukosoaji kama vile yeye hakuwa sehemu ya Serikali ya Magufuli na akiwa mshauri number moja. Kama kweli hakupenda yaliyokuwa yakifanyika chini ya Magufuli, kwanini alibaki hapo? Kwanini alikubali uteuzi wa mara ya pili kuwania nafasi ya Makamu wa Rais?

Kama mshauri wa kwanza kabisa wa Rais Magufuli, anachotakiwa ni kuwa na hekima na busara na kusema tu "wao kama binadamu, katika kipindi cha Rais Magufuli kuna mambo yalikwenda sawa na kuna mambo hayakwenda sawa na kwamba huu sasa ni wakati wa kuyaangalia yake ambayo hayakwenda sawa na kuangalia jinsi ya kuyarekebisha" bila ku-point finger kwa marehemu Magufuli. Wote tunaelewa hakuna serikali inayofanya kila kitu ambacho watu wote watayapenda, hiyo serikali haipo duniani. Mama Samia anaweza kuwapenndezesha asimilia 1% ya hao wanaopenda kusikia Magufuli akisemwa kwa sasa, lakini kuna asilimia 99% ya Watanzania ambao wana wish Magufuli angepewa nafasi na Mungu ya kumaliza muda wake, lakini tumekubaliana na mapenzi ya Mungu.
Mama Samia can not take credits kwa yale mazuri na kunyoosha kidole kwa Magufuli kwa yale yanayosemwa na wapinzani na wale ambao hawakumpenda Magufuli.

Kikubwa anachotakiwa kufanya, ni kuyachukua yote na kutumia busara na hekima kurekebidha yale ambayo anadhani hayakwenda vizuri kwa busara. Kwa mwendo wa sasa akiendelea hivi, anatuambia alikuwepo kwenye serikali ya Magufuli kama bendera ya kufuata upepo na hakuwa na guts za kusema sikubaliani na hili, na angeweza kujiondoa kwa kujiudhuru. Anatuambia aliona bora akae tu kwenye nafasi ya Makamubwa Rais hata kama hakuwa na impact yeyote, bora tu alikuwa hapo akila pesa ya walipa kodi. Namshauri mama yangu ayachukue yote, mazuri na yasiyo mazuri na aje na mkakati wake wa kutimiza yale yote mazuri na ndoto ya Rais wetu mpendwa Magufuli. Hii ni pamoja na hiyo miradi imeeiita ya makaratasi, utadhani kuna mradi unaanzwa kutekekezwa bila kuanzia kwenye makaratasi. Ni vizuri akajifunza kuwa loyal, lakini pia ni vizuri kujua bila Magufuli dared, na yeye atuonyeshe uwezo wake. Tunajua kabisa bila Magufuli Samia had zero chance ya kuwa siyo Makamu tu, ya kuwa Rais wa taifa letu hili lililopiga hatua kubwa sana kimaendeleo katika kipindi kifupi cha Rais Magufuli. Tuonyeshe jinsi utakavyorebisha ukusanyaji kodi bila kuwa too critical kwa yale yaloyokuwa yakifanyika wewe ukiwa sehemu ya serikali. Tuonyesha jinsi utakavyotekekeza hiyo miradi ya makaratasi, tuonyeshe uthubutu wako. SGR haikuanzia kwenye utekelezaji, Nyerere Hydro Power haikuanzia kwenye utekekezaji, yote yalianzia kwenye makaratasi. Yaani kuna vitu unaongea, inaonyesha wazi ulikuwa upo upo tu kwenye nafasi ya Makamu wa Rais, kama vile ulikuwa hujui majukumu yako na nafasi yako ya kumshauri Rais.

Tunategemea kwamba ndoto ya Magufuli itatimia, kana siyo chini yako, kwa wale watakao kuja baada ya wewe. Ndoto ya Magufuli ndiyo mkombozi wa kiuchumi wa Tanzania na hatuwezi kuiacha ife tu hivi hivi kwa sababu unadhani ipo kwenye makaratasi. Na lingine, ukifanya kila kitu kupendezesha wale unaohofia watakukosoa, kwa kuangalia dunia inasema nini ama ita react vipi? You are doom to fail. Utashindwa kufanya maamuzi yeyote magumu kwa kuhofia image yako na dunia itasema nini. Bila ndoto, hakuna kinachoweza kufanyika. Unaanza na ndoto, unazichambua na kuzipeka kwenye utekekezaji. Usipoota Mama, utatekeleza tu yale yaliyoasisiwa na Rais Magufuli na utabaki kulalamikia miradi ya makaratasi makaratasi sababu umeshindwa kubadilisha ndoto zilizopo kwenye makaratasi kuwa reality. Ni mategemeo yangu kwamba utarekebisha kasoro ndogondogo zilizojitokeza kipindi cha Magufuli bila kuwa too critical kwa Magufuli ambaye hivi sasa hawezi kujisemea mwenyewe. No human is perfect, including yourself, kwa hiyo makosa ya kibinadamu yarekebishwe kwa busara, and you should remain loyal kwa yule aliyekuwa sababu ya wewe kufika hapo. Yeye kutokuwepo isiwe sababu ya wewe kujiona kwamba ni Rais bora kuliko aliyekufikisha hapo. Nakutakia ufanikiwe,sababu ukifanikiwa, Tanzania imefanikiwa. Usimseme vibaya yule aliyekuwa sababu ya wewe kufika ulipofika hapo leo, lakini ukizingatia hawezi kujisemea mwenyewe leo. Know how to be loyal, you will be rewarded. Kila la heri Rais Samia Suluhu Hassan.
 
TASAC na ukitimba wa kuua bandari zetu.

Ushauri kwa Mh. Rais Samia ni kuangalia kwa upya na kwa upya wake, madhara ambayo serikali inayapata kwa sheria kandamizi ya kuwanyima sector binafsi kufanya biashara na kazi mbalimbali zinazohusiana na bandari.

Sheria hiyo ilipitishwa mwaka juzi, ambayo, inawapa Tasac uwezo wa kuwa:-
1) Wakala wa Meli pekee(Shipping Agent)
2) Wakala wa Forodha (kwa asilimia kubwa ya mizigo inayoingia
3) Kuwa kampuni pekee inayofanya Tallying

Bila Kusahau, Tasac ndiye mtoa leseni na msimamizi wa sector ya bandari.... hivi Tasac Agent akikosea atajikagua na kujinyima mwenyewe leseni?

Kwa sheria ile, Kampuni binafsi haziwezi kuwa wakala wa meli labda meli hiyo iwe imebeba containers. Yaani leo hii Bakhresa na wafanyabiashara wengine, wanalazimishwa na sheria kuwachagua Tasac kuwa agent wao, watake au wasitake, labda wasilete mizigo yao Tanzania.

Tunapohamasisha uwekezaji, tufahamu kuwa wawekezaji wengi wanatumia bandari kuleta mizigo yao, kuwalazimisba kutumia agent wa serikali sio sahihi.

Kwa sheria ile, maelfu ya Watanzania walioajiriwa kwenye sector za Shipping Agency, Clearing Agent and other 3rd Parties company wamepoteza kazi na wapo wanahangaika mitaani.

Huu ni ukweli, kwa mwaka mmoja ambao Tasac amekuwa the only agent, mizigo imepungua maana nchi jirani wanaikimbia bandari ambayo haina ufanisi. Serikali ibaki kuwa msimamizi, na ikilazimika, awe agent kwa mizigo ya serikali tu, lakini sio kuwalazimisha wafanyabiashara binafsi kutumia wakala wa serikali.

Tuokolee bandari zetu Mh. Raisi.
 
#Mama ongeza umakini, minong'ono imekuwa ni mingi sana sio bara sio visiwani Watu wanaanza kupoteza imani na wewe. Mpaka ndani ya bunge lako majadiliano ya pembeni yamekuwa ni mengi. Sikukosoi lakini kuna mambo ingefaa sana uyatafakari sana kabla ya maamuzi.

Wapo pia umewatia moyo kwamba kwao mambo yanaenda kukaa sawa sasa Hao ni wale, wanaoamini kuwa umasikin wao na njaa zao ni makosa yanayotokana na serikali tu Not their faults. Hao ni wale people of full of excuses, in the same time some of them are making money as well.

Binafsi nakuunga mkono Lakini usiturudishe Misiri utumwani kufanya vibarua. Hapa wale waliopitapita vyuoni hawatanielewa maana baadhi yao wanaishi kizamani yaan #Education is a key of success by being employed! right! but..Dunia inabadilika sana sio bongo tu ni kote ulimwenguni, if you expect for employment sometimes is so complicated. Ukimwambia kijana ajiajiri atasema ummpe mtaji, but mtaji ni maarifa..any way mimi sio Nanauka

Back to the point; Maneno yanazidi kuwa mengi na imani ya Watanzania kwa sasa wanaamini baadhi ya maamuz unayoyatoa si yako bali unatumika na watu flan kwa maslahi yao na mikakati yao. Mimi ni mmbeya tu nimeona nikuletee habari hii. Najua hujachaguliwa na wananchi Lakin uliaminiwa na yule aliyechaguliwa na wananchi kuwa unafaa kuwa mshauri wake ndio maana kwenye kikaratasi cha kura picha yako pia iliwekwa kwa pembeni.

Kumbuka ushindi wa 80% ulikuwa wa Mgombea urais naye alikuamini na wewe, Usipoamini haya ngoja Uchaguzi 2025 ndipo utasadiki haya niyasemayo.

Asante!
 
Binafsi yangu nna imani na mama yetu!Namuombea kwa Mungu amtunze na ampe afya njema ili alifikishe taifa pale linapotakiwa kufika!
 
#Mama ongeza umakini, minong'ono imekuwa ni mingi sana sio bara sio visiwani Watu wanaanza kupoteza imani na wewe...mpaka ndani ya bunge lako majadiliano ya pembeni yamekuwa ni mengi. Sikukosoi lakin kuna mambo ingefaa sana uyatafakari sana kabla ya maamuzi.

Wapo pia umewatia moyo kwamba kwao mambo yanaenda kukaa sawa sasa Hao ni wale, wanaoamini kuwa umasikin wao na njaa zao ni makosa yanayotokana na serikali tu Not their faults...hao ni wale people of full of excuses, in the same time some of them are making money as well.
Binafsi nakuunga mkono Lakin usiturudishe Misiri utumwani kufanya vibarua. Hapa wale waliopitapita vyuoni hawatanielewa maana baadhi yao wanaishi kizamani yaan #Education is a key of success by being employed ..!! right! but..Dunia inabadilika sana sio bongo tu ni kote ulimwenguni, if you expect for employment sometimes is so complicated. Ukimwambia kijana ajiajiri atasema ummpe mtaji, but mtaji ni maarifa..any way mimi sio Nanauka

Back to the point; Maneno yanazidi kuwa mengi na imani ya watanzania kwa sasa wanaamini baadhi ya maamuz unayoyatoa si yako bali unatumika na watu flan kwa maslahi yao na mikakati yao. Mimi ni mmbeya tu nimeona nikuletee habari hii. Najua hujachaguliwa na wananchi Lakin uliaminiwa na yule aliyechaguliwa na wananchi kuwa unafaa kuwa mshauri wake ndio maana kwenye kikaratasi cha kura picha yako pia iliwekwa kwa pembeni, Kumbuka ushindi wa 80% ulikuwa wa Mgombea urais naye alikuamini na wewe, Usipoamini haya ngoja Uchaguzi 2025 ndipo utasadiki haya niyasemayo.
Asante...!
Watu wapi unawasemea, binafsiii nina imani nae kubwa tu, na siko peke yanguu
 
Asilimia kubwa ya watu wana imani na mama,kumbuka sahvi yeye ndiyo rais na amiri jeshi mkuu
Muda bado upo mwingi mama kuweka
Mambo sawa

Ova
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzania haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli kafa, lakini spirit yake haijafa. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu, katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli kafa lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, na kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli haijafa. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60, kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Boss Asante Sana! Huyu mama ni Jembe ila aende kwa tahadhari! JPM hakupendwa tu hivi hivi bali kwa sababu ya uzalendo wake. Hakuwa malaika kwa hiyo kuna umuhimu wa mabadiliko lakini sio kwa mambo ya 'pride' yetu kama watanzania.
 
#Mama ongeza umakini, minong'ono imekuwa ni mingi sana sio bara sio visiwani Watu wanaanza kupoteza imani na wewe. Mpaka ndani ya bunge lako majadiliano ya pembeni yamekuwa ni mengi. Sikukosoi lakini kuna mambo ingefaa sana uyatafakari sana kabla ya maamuzi.

Wapo pia umewatia moyo kwamba kwao mambo yanaenda kukaa sawa sasa Hao ni wale, wanaoamini kuwa umasikin wao na njaa zao ni makosa yanayotokana na serikali tu Not their faults. Hao ni wale people of full of excuses, in the same time some of them are making money as well.

Binafsi nakuunga mkono Lakini usiturudishe Misiri utumwani kufanya vibarua. Hapa wale waliopitapita vyuoni hawatanielewa maana baadhi yao wanaishi kizamani yaan #Education is a key of success by being employed! right! but..Dunia inabadilika sana sio bongo tu ni kote ulimwenguni, if you expect for employment sometimes is so complicated. Ukimwambia kijana ajiajiri atasema ummpe mtaji, but mtaji ni maarifa..any way mimi sio Nanauka

Back to the point; Maneno yanazidi kuwa mengi na imani ya Watanzania kwa sasa wanaamini baadhi ya maamuz unayoyatoa si yako bali unatumika na watu flan kwa maslahi yao na mikakati yao. Mimi ni mmbeya tu nimeona nikuletee habari hii. Najua hujachaguliwa na wananchi Lakin uliaminiwa na yule aliyechaguliwa na wananchi kuwa unafaa kuwa mshauri wake ndio maana kwenye kikaratasi cha kura picha yako pia iliwekwa kwa pembeni.

Kumbuka ushindi wa 80% ulikuwa wa Mgombea urais naye alikuamini na wewe, Usipoamini haya ngoja Uchaguzi 2025 ndipo utasadiki haya niyasemayo.

Asante!
Usipende kurejea ushindi wa uchaguzi kila mtu anajua huo ulikuwa mchezo wa kuigiza, ila mama ni afadhali mara 200 kulinganisha na yule bwana.
 
Mhe. Rais pamoja na kuwa hujakaa muda mrefu katika nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Tanzania, binafsi ninakushauri umteue Professa Assad kuwa Mbunge na baadaye kumpa nafasi ambayo atakusaidia sana katika masuala ya fedha. Professa Assad ni mwadilifu, mwaminifu, mkweli, weledi. Kusema ukweli ndo ulimwondoa katika nafasi yake ya CAG kabla kutimiza miaka 65 ambayo ni miaka ya kisheria kwa CAG.
 
Boss Asante Sana! Huyu mama ni Jembe ila aende kwa tahadhari! JPM hakupendwa tu hivi hivi bali kwa sababu ya uzalendo wake. Hakuwa malaika kwa hiyo kuna umuhimu wa mabadiliko lakini sio kwa mambo ya 'pride' yetu kama watanzania.
Nashukuru ndugu yangu. Upo sahihi sana, hakuna yeyote asiyependa mabadiliko chanya, lakini kama ulivyosema JPM alitengeneza pride ya kitanzania iliyokwishapotezwa na tawala kadha wa kadha nyuma yake. Mama ajitahidi "kuboost" morale na pride ya watanzania kupitia speech zake na matendo yake. Body language kwenye uongozi ni kitu cha msingi sana, na mtangulizi wake alifanikiwa sana kuambukiza confidence miongoni mwa raia.
 
Back
Top Bottom