GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,099
Fasihi hiyo mkuu, Sio kila kitu unakichukilia kama kilivyoKatika hali ambayo nmeipenda ni Rais kuwa Mkweli kuwa kwa Mwanza amewapelekea Bomu. Uliandikwa humu Uzi kuwa Kwa nini ameamua kuwaadhibu wananchi wa mwanza kwa Kuwapelekea Chalamila.
View attachment 1806666
Anaposema ni MLIPUKAJI. KINACHOLIPUKA SI NI BOMU? au mimi nmewaza mbali sana? Then kwa nini uwapelekee watu kitu kinacholipuka? Si unataka kuwaua? Je haioneshi kuwa unawachukia? Au alitaka sema nini hapa?
Chalamila ni mchapa kazi sana sana, Tatizo Lake ni maneno mengi sana, Hata kitu kidogo anakikuza
Chalamila akiwaka na kama msaidizi wake nae akawaka mkoa utachimbika, Hofu itatawala
Magufuli alikuwa anawaka sana lakini Mama Samia alikuwa cool ndio uongozi
Kikwete alikuwa cool lakini lowasa alitikisa kama Waziri mkuu
Baba na Mama wote wakiwa wakali nyumbani upendo unapotea
Inabidi Baba akiwaka Mama anawapeti peti watoto
Au Mama akiwaka Baba unawapa faraja watoto
Wazazi wote wakiwa wakali nyumba mnakimbiana