Mitandao ya simu ipige faida ya internet kwa mara ya mwisho. Elon Musk kuleta internet ya Starlink Tanzania

Mwakani Elon Musk atazindua huduma ya internet kupitia kampuni yake ya Starlink. Elon Musk alisema kwenye tweet yake kuwa mwakani atazindua huduma ya internet ambayo itakuwa inapatikana dunia nzima bila kujali eneo gani upo.

Ikumbukwe kuwa internet ya Elon Musk itakuwa inarushwa na satellite zake yeye mwenyewe alizoweka angani huko. Naona kama mpango wa Elon Musk utaweza kuumiza biashara ya Internet inayotumika na mitandao ya simu inayotumia minara. Hivyo itaweza kuleta ushindani wa kibiashara.

Lakini na wasiwasi kama mitandao ya simu ya hapa Tanzania itaweza kushindana na Elon Musk kulingana na Teknolojia anayotumia?

Natamani Elon Musk angeanzisha hata mwaka huu ili tupumue gharama za vifurushi. Mitandao ya simu pigeni faida kwa mara ya mwisho. Kuanzia mwaka ujao bilionea atawanyanyasa sana. Je mtaweza kushindana naye?
Wanajukwaa mna mtazamo gani juu ya hili?
Safi sana kama WHATSUP call ilivyorahisisha mawasiliano kote duniani.
 
Elon Mask asisahau na kutuvumbulia na nishati ya Umeme iwe wireless,hawa Tanesco tumewachoka na mgao wao
 
Mbona ilishaanza kupiga mzigo na ina footprint sehemu kubwa ya Amerika na Uropa
 
Hiy hudum kwa sisi wala hoi bado mkuu kwan kujiunga na kuwa na vifaa vyote iliuwez kupat hiyo hudum dola 599 kwa kawaida na 2500 kwa bishara gharama ,a matumiz ya mwez ni dola 99 kwa sisi ni gharama kubwa saana nafhan tutasubir mpaka 2030 angalau ndo ghrama zinaweza shuka ila ni kitendawili
 
Tajiri mwenye vituko bilionea Elon Musk amevutiwa na mazingira ya uwekezaji Tanzania.
Kampuni yake ya Starlink kufanya uwekezaji mkubwa kuanzia Mwaka 2023.

Tovuti ya Starlink inayomilikiwa na mfanyabiashara ambaye pia ni mmiliki wa mtandao wa Twitter, Elon Musk imetangaza mpango wa kuleta huduma ya intaneti kwa njia ya satelaiti (starlink) nchi Tanzania kati ya Januari na Machi 2023 endapo itaruhusiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Jabiri Bakari amethibitisha kuwa kampuni hiyo ya Starlink ilituma maombi ya kutoa huduma ya intaneti nchini kupitia tovuti ya TCRA.

Wadau mbalimbali wametoa maoni yao kuhusu huduma hiyo akiwemo mchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Abel Kinyondo ambapo amesema ikiwa huduma hiyo itafika nchini itasaidia wakulima kupata habari kuhusu hali ya hewa na jinsi wanavyoweza kuboresha mazao yao, pia itawasaidia wafanyabiashara kufanya biashara zao mtandaoni na kupata mafunzo yanayokusudiwa.

Teknolojia hiyo ya intaneti inapatikana baada ya kuunganishwa kwa satelaiti nyingi ambazo hutumika kutoa huduma ya intaneti kwenye maeneo mbalimbali duniani hasa vijijini.


045BDD95-494E-4035-9CD6-A5B815AAEB66.jpeg
 
Hivi hatuwezi kuomba huyu jamaa ainunue Tanzania awe raisi wa kwa mkataba wa hata miaka 50 hivi?

Yaani awe ana control kila kitu mradi tu atupe maisha bora.

Maana naona tunakoelekea ni bora hata enzi za mkoloni.
 
Back
Top Bottom