Serikali iachane na Sera zinazobana Wawekezaji, mfano kumtaka Elon Musk kuweka ofisi za Starlink Tanzania

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,121
starlink.jpg

Kitendo cha Waziri Nape Nnauye kusema bado Serikali haijafikia muafaka wa kumruhusu Mwekezaji na Tajiri namba 2 duniani, Elon Musk kuwekeza nchini ili kutoa huduma ya Intaneti yenye kasi kupitia Satelite hadi atakapoweka ofisi zake nchini Tanzania, inaonesha wazi bado tumekumbatia Sera za kikoloni zisizoangalia fursa kwanza.

Kampuni ya Starlink imeshafanya uwezekaji kwenye Nchi nyingi duniani ikiwemo za Afrika ambako sidhani kama kote amepewa masharti ya kuweka ofisi kwanza. Mfano mzuri ni jirani yetu Rwanda ambaye tayari ameshatoa vibali kwa Elon kuwekeza huduma hiyo.

Ni kama vile sera zetu zinaangalia zaidi kubana uwekezaji kuliko kuangalia faida itakayopatikana baada ya uwekezaji kuanza. Kwanini hatujifunzi kwa Nchi nyingine zinafanya nini kwanza? Kitendo cha Elon kusema anasubiri Serikali impe kibali kimetuma picha mbaya kwa wawekezaji wengine na kuona Tanzania ina sera ngumu za uwekezaji.
 
Wanataka wajue wapi watapeleka Barua za haraka kupandisha yozo...kufungia twitter na Clubhouse maana wanajua kule Marekani email za TCRA na TRA hazitasomwa!!
 
Tanzania, inaonesha wazi bado tumekumbatia Sera za kikoloni zisizoangalia fursa kwanza.
SemperFi,
Niulize tu, hivi kuna sera ya kikoloni au ya mkoloni ambayo haikuangalia fursa za watu kama E.M? Ni kweli hayo? Je, kuifananisha Serikali ya Tanzania kuwa sawa na ya kikoloni ni sawa?

Nchi nyingi duniani ikiwemo za Afrika ambako sidhani kama kote amepewa masharti ya kuweka ofisi kwanza
Hudhani? Hivi katika utafiti mfupi(I assume kutokana na majibu yako)uliofanya umeona kuna nchi ngapi zinalegeza sheria zake ili kukumbatia mwekezaji mmoja? mbali na hizo"Duniani" hata na za 'Afrika'?

Sielewei kuna wale wa Duniani na wa Afrika? Afrika haiko Duniani?

. Kwanini hatujifunzi kwa Nchi nyingine zinafanya nini kwanza?
Zinafanya nini? Je, zinaacha kufuata sheria zilizojiwekea? Wanapuuza sheria? au Wanalinda na Kufuata sheria zilizopo kama anavyofanya Nape?
 
Tanzania, inaonesha wazi bado tumekumbatia Sera za kikoloni zisizoangalia fursa kwanza.
SemperFi,
Niulize tu, hivi kuna sera ya kikoloni au ya mkoloni ambayo haikuangalia fursa za watu kama E.M? Ni kweli hayo? Je, kuifananisha Serikali ya Tanzania kuwa sawa na ya kikoloni ni sawa?
Kwa misingi ipi?

Nchi nyingi duniani ikiwemo za Afrika ambako sidhani kama kote amepewa masharti ya kuweka ofisi kwanza
Hudhani? Hivi katika utafiti mfupi(I assume kutokana na majibu yako)uliofanya umeona kuna nchi ngapi zinalegeza sheria zake ili kukumbatia mwekezaji mmoja? mbali na hizo"Duniani" hata na za 'Afrika'?

Sielewei kuna wale wa Duniani na wa Afrika? Afrika haikoDuniani?

. Kwanini hatujifunzi kwa Nchi nyingine zinafanya nini kwanza?
Zinafanya nini? Je, zinaacha kufuata sheria zilizojiwekea? Wanapuuza sheria? au Wanalinda na Kufuata sheria zilizopo kama anavyofanya Nape?
 
Nape is an empty box with a big stomach.
Huyu jamaa huwa anawaza na kuongea ujinga tu.
 
Kwenye masuala ya kodi mnafahamu kitu kinaitwa Permanent Establishment? au mnajiongelea tu mambo bila kujua sababu ni nn. Sheria za kodi za Tanzania mtu hawezi kupigwa kodi kama hana permanent Establishment
 
starlink.jpg

Kitendo cha Waziri Nape Nnauye kusema bado Serikali haijafikia muafaka wa kumruhusu Mwekezaji na Tajiri namba 2 duniani, Elon Musk kuwekeza nchini ili kutoa huduma ya Intaneti yenye kasi kupitia Satelite hadi atakapoweka ofisi zake nchini Tanzania, inaonesha wazi bado tumekumbatia Sera za kikoloni zisizoangalia fursa kwanza.

Kampuni ya Starlink imeshafanya uwezekaji kwenye Nchi nyingi duniani ikiwemo za Afrika ambako sidhani kama kote amepewa masharti ya kuweka ofisi kwanza. Mfano mzuri ni jirani yetu Rwanda ambaye tayari ameshatoa vibali kwa Elon kuwekeza huduma hiyo.

Ni kama vile sera zetu zinaangalia zaidi kubana uwekezaji kuliko kuangalia faida itakayopatikana baada ya uwekezaji kuanza. Kwanini hatujifunzi kwa Nchi nyingine zinafanya nini kwanza? Kitendo cha Elon kusema anasubiri Serikali impe kibali kimetuma picha mbaya kwa wawekezaji wengine na kuona Tanzania ina sera ngumu za uwekezaji.
Nchi yetu bado Ina upuuuzi wa kisoshalisti
 
Back
Top Bottom