Umeme pia kukatika mara kwa mara, Tanzania ili watendaji wa serikali na sekta binafsi wafanye kazi kunahitajika kuwa na kiongozi mkali tunahitaji kusukumwa sana ni aibu sana, kwa kweli gap la mwendazake linaonekana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona hata leo units hazinunuliki?. Nimejaribu kununua lakini imeshindikana.
 
Mama anakosea mwenyewe

Alitakiwa afanye kama meko alivyofanya.
Meko alifukuza watu wote wa JK.

Sasa mama anawakumbatia watu wa meko kuanzia waziri mkuu

Hii ni hatari

Watu wa meko wengi ni wakatili na walibebwa na meko na wote ni zero brain

Hawapendi kuona reformation yoyote inauokwenda kinyume na dikteta meko.

Kwa hio wanachokifanya ni kumhujumu mama wazi wazi
 
TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MANUNUZI YA LUKU KWA BAADHI YA WATEJA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi wateja wake kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye mfumo wa manunuzi ya umeme wa LUKU siku ya Jumatatu, Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme.

Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wanafanya kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa haraka.

Tutaendelea kutoa taarifa kadri huduma itakavyo kuwa ikirejea.

Tunawaomba radhi kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye mfumo wa manunuzi ya umeme wa LUKU siku ya Jumatatu, Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme. Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wanafanya kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa haraka.

---
Yaani kweli Tanesco watu wakae gizani kisa mmeshindwa kuteneneza system yenu

Bure kabisa

Kuna wajinga hapo kwenu inabidi wawajibishwe
 
Kama ni hivyo basi hiyo sukuma gang ni mtandao mkubwa sana: malori kukwama bandarini, tra mtandao uko chini, majambazi wanatest mitambo dar, etc
wa sukuma gang na gogo gang hautamwacha mama salama hataamini chadema itavokuwa na sukuma na gogo member wa kutosha na naomba kwa mungu akwame
 
Hao wasukuma wako wengi kiasi gani hadi kuwa kila sehemu ya tatizo ?mimi naona wapinzani wa sisiemu wanatumia hii njia kuwaondoa watu wa kanda ya ziwa upande wao bila kujua na ifikapo 2025 ndio utaona turnabout ki ukweli wasukuma hawajwahi kuwa na umoja wowote na hii sukuma gang nI tactic ya kuwaunganisha kuona kuwa wanabaguliwa na watu bila kujua wamekuwa wana shabikia hatimaye kisichokuwapo kitakuwapo na itakuwa kitu kibaya kuliko maelezo muda utaongea
Mkuu mgogo na msukuma wameanza kuunda mipango yao na wanaoshabikia hawajua kama wanafanya umoja kukoma watakuja kuchekea chooni
 
Nachokupenda kweli ww ni mpinzani hujawahi kusifia kuanzia leo nahama ccm kiroho Ila kimwili nipo kwao kwa masirahi nilimuelewa sana jiwe ila huyu mama sifikilii kuja kumuelewa anapotupeleka team jk tu ndo wanaelewa tuendako
Na mwenyewe alisema tutamkumbuka. Sasa sisi wa kupata 2000 leo ndio ununue umeme tunalala giza. Ina gikia mahali mtu unatamani kufunga loop wire nyuma ya meter upate umeme. Kuliko kusubiria umeme usio patikana.
 
Kuna watu Wana incubators na wamewekeza mayai zaidi ya 1000 ambapo vingetotolewa mtu angepata si chini ya TSH 2,500,000. Kwa hasara Kama hii Tanesco mnatuambiaje?
 
Mama anakosea mwenyewe

Alitakiwa afanye kama meko alivyofanya.
Meko alifukuza watu wote wa JK.

Sasa mama anawakumbatia watu wa meko kuanzia waziri mkuu

Hii ni hatari

Watu wa meko wengi ni wakatili na walibebwa na meko na wote ni zero brain

Hawapendi kuona reformation yoyote inauokwenda kinyume na dikteta meko.

Kwa hio wanachokifanya ni kumhujumu mama wazi wazi
Team jk mmetuharibia nchi bado nanyie mnaongea hivi msukuma na mtu wa pwani nani mvivu
 
Hi nchi ili ufanikiwe kuiongoza inatakiwa uiongoze kibabe kama JPM

Hata ile citiscan ya Muhimbili sasa hivi itaanza kuharibika tena

Ndani ya miezi 2 system muhimu zote zime collapse ilianza TRA ikaja TPA na Leo LUKU

Alisema mtanikumbuka sio kwa mabaya ila ni kwa mazuri
 
Mkuu nasoma computer science....katika programming hakuna hitirafu ,na hata virus ni program ya computer inayofanya kazi kwa kuipa ubize computa au kupiga copy au kudelete files muhimu na ni mtu anaeza tengeneza virusi, hebu nirud kwenye point, program ikiandikwa haibadiliki, ni pure number ile, I mean automation is perfect, Kama ilivo 1*1=1 it can't change.
Siyo kweli, kaongeze na darasa la Cyber security alafu uje ulete mrejesho.
 
Haiwezekani leo ni Siku ya Tatu, wananchi tunashindwa kununua umeme, huku mkitoa Majibu mepesi kwamba mnashughulikia, hii mbona haikuwahi kutokea enzi za Mwendazake?

Mnamuhujumu kwa Makusudi Mama Samia aonekane nchi itamshinda. Tayari tushaanza kusikia baadhi ya taasisi za dola, wafanyakazi wake wakiongea mtaani kutotoa ushirikiano kwa serikali ili kumfelisha Mama. Mama Samia amka, usicheke na Nyani. Hili la Tanesco ni namba moja.
 
jana nimehangaika kishenzi mwisho nikaamua kulala tu.

wacha mama aendelee kutubembeleza,tutafanya kazi kwa uhuru zaidi.
 
Habari zenu Watanzania wenzangu,

Nadhani kwa sasa ipo haja ya kuwa na kampuni nyingi tu kama vile ilivyo kwa mitandao ya simu sababu tunaotaabika ni sisi watu wa chini wenye pesa zao hawawezi pata tabu ya umeme kama sisi tusharudi kulekule tena ili watu wauze majereta yao.
 
Back
Top Bottom