#COVID19 Serikali ya Tanzania yatoa Katazo la Misongamano isiyokuwa ya lazima kukabiliana na UVIKO

Serikali yapiga marufuku mikusanyiko nchi nzima​



THURSDAY JULY 22 2021​

Gwajima pic

Summary

  • Serikali imetangaza uamuzi huo wakati idadi ya waathirika wa corona ikifikia 682 ambao wanapatiwa matibabu kwenye vituo vya afya mbalimbali nchini.


New Content Item (1)

By Tatu Mohamed
More by this Author

Dar es Salaam. Serikali imepiga marufuku mikusanyiko yote isiyo ya lazima nchi nzima na ile ambayo itaonekena ni lazima basi tahadhari zote zichukuliwe.


Hatua hiyo inalenga kukabiliana na hofu ya kuendelea kusambaa kwa mlipuko wa tatu wa janga la corona ambao tayari umeathiri mamia ya Watanzania.


Agizo hilo limetolewa Alhamisi ya Julai 22, 2021 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima ambaye amesisitiza utekelezaji wa agizo hilo.


Hata hivyo, agizo hilo limekuja wakati ambao tayari wakuu wa mikoa mbalimbali nchini, wakitangaza kupiga marufuku mikusanyiko isiyo ya lazima kwenye maeneo yao.


Katika agizo lake hilo, Dk Gwajima amewataka viongozi wa Serikali na wa sekta binafsi kuonyesha mfano wa namna wanavyochukua hatua kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19.


Dk Gwajima pia amesema kuwa mpaka sasa idadi ya wagonjwa wa Covid 19 imezidi kuongezeka na hadi kufikia Julai 21,2021 kulikuwa na wagonjwa 682 wanaopatiwa matibabu kwenye vituo mbalimbali.



Amesisistiza kuwa Serikali itaendelea kutoa takwimu hizo pamoja kufuatilia hali halisi ya mwenendo wa ugonjwa huo na kutangaza hatua mbalimbali za kuchukua.


“Ili kuimarisha zaidi kasi ya kuoambana na kudhibiti maambukizi ya UVIKO-19, natamka kuanzia leo tarehe 22/07/2021 nimekataza shughuli zote za misongamano yote isiyokuwa ya lazima . Nimekataza shughuli zote za misongamano na ile yenye ulazima tahadhari ya kutosha ichukuliwe bila kuathiri shughuli za kiuchumi na kitaifa.


“Naelekeza wakuu wa mikoa na wilaya nchini kuwapa ushirikiano waganga wakuu wa mikoa na wilaya kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria ya Afya ya Jamii Na. 1 ya Mwaka 2009 na kuweka utaratibu mzuri kwa wale wanaoomba vibali vya shughuli zenye ulazima,”amesema Dk Gwajima.


Pia, ametoa wito kwa wananchi wote kujiandaa kupata huduma ya chanjo kama ambavyo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alivyotangaza jana.


“Leo hii wataalamu wa afya wamekutana kupata mafunzo tayari kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma ya chanjo dhidi ya UVIKO-19 kwa hiari na bila malipo,” amesema.
 
Mikusanyiko ipi ni ya LAZIMA na ipi isiyo ya lazima, be specific

Kwa hiyo Covid-19 inachagua mikusanyiko ya kushambulia siyo.
 
View attachment 1863511
View attachment 1863512

TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI.

TAMKO LA KATAZO LA MISONGAMANO ISIYOKUWA YA LAZIMA

Tarehe 22 Julai, 2021 - Dar es Salaam.

Ndugu Wananchi, kama tunavyofahamu Tanzania iko kwenye mapambano ya kudhibiti maambukizi ya UVIKO-19 ikiwa ni wimbi la 3 la mlipuko huu tangu uingie nchini Machi, 2020. Itakumbukwa kuwa Wizara ya Afya na Viongozi wa Serikali kwa ujumla wake kwenye ngazi mbalimbali wamekuwa wakitoa taarifa, elimu na kuhamasisha juu ya kujikinga na kuwakinga wengine dhidi ya maambukizi ya UVIKO-19.

Ndugu Wananchi, Serikali inatambua kuwa wananchi walio wengi wamekuwa wasikivu, wakiitikia na kutekeleza miongozo yote ya kujikinga na kuwakinga wengine ingawa kwenye baadhi ya maeneo mwitikio umekuwa siyo wa kuridhisha. Hali hii imeendelea kuchangia kuongezeka kwa maambukizi na hatimaye kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa waliolazwa ambapo kufikia tarehe 21/07/2021 katika vituo vya huduma za afya kote nchini kulikuwa na wagonjwa 682 waliokuwa wanaugua maradhi ya UVIKO-19. Aidha, watalaamu wa afya wameendelea kupambana kwa moyo mmoja kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa wakati lakini hata hivyo baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakipoteza maisha.

Ndugu Wananchi, Wizara itaendelea kutoa takwimu hizi ili kwa pamoja tuendelee kufuatilia hali halisi ya mwenendo wa ugonjwa huu huku tukiendelea kuchukua hatua za kutosha. Aidha, ili kuimarisha zaidi kasi ya kupambana na kudhibiti maambukizi ya UVIKO-19
natamka kuwa, kuanzia leo tarehe 22/07/2021 nimekataza shughuli zote za misongamano yote isiyo ya lazima na ile yenye ulazima tahadhari ya kutosha ichukuliwe bila kuathiri shughuli za kiuchumi na kitaifa. Naelekeza Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwapa ushirikiano Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria ya Afya ya Jamii Na. 1 ya Mwaka 2009 na kuweka utaratibu mzuri kwa wale wanaoomba vibali vya shughuli zenye ulazima.

Ndugu Wananchi, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau wake wote itaendelea kutoa elimu na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miongozo yote ya afya. Aidha, natoa wito kwa wananchi wote kujiandaa kupata huduma ya Chanjo kama ambavyo Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyotoa taarifa jana tarehe 21/07/2021. Leo hii wataalamu wa afya wamekutana kupata mafunzo tayari kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa huduma ya Chanjo dhidi ya UVIKO-19 kwa hiari na bila malipo. Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.

Ndugu Wananchi, Wito wangu tuendelee kushikamana kwenye mapambano ya kutokomeza kabisa adui UVIKO-19 kwa kuzingatia utekelezaji wa afua zote za kujikinga na kuwakinga wengine zikiwemo;

  1. Kuhakikisha sehemu zote zinazotoa huduma za kijamii zinakuwa na miundombinu ya huduma ya kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni na kama maji hakuna kuwe na matumizi ya vitakasa mikono.
  2. Wananchi wote wanaotoa huduma za kijamii na wanaofika kupata huduma za kijamii wahakikishe wamezingatia afua za kinga zikiwemo kuvaa barakoa safi na salama.
  3. Kwenye maeneo ya huduma za kijamii zinazokutanisha watu kadhaa kupata huduma kanuni ya kuepuka misongamano izingatiwe kwa kuchukua tahadhari zote.
  4. Kwenye vyombo vya usafiri utaratibu wa kuepuka kubeba abiria kwa kusongamana uzingatiwe na kabla abiria hao hawajaingia kwenye chombo husika kuwe na utaratibu wa kuhakikisha wamezingatia tahadhari zote za kujikinga na kuwakinga wengine.
  5. Vilevile, nawakumbusha Wananchi tuendelee kuzingatia lishe bora, kufanya mazoezi na kutumia tiba asili zilizosajiliwa na baraza la tiba asili pasipo kuchelewa kufika kwenye vituo vya huduma kwa ushauri wa kitaalamu.
Aidha, natoa wito kwa viongozi wa serikali na wa sekta binafsi na taasisi zake zote kuonesha mfano kwa wananchi jinsi ambavyo wao wanatekeleza maagizo ya kuchukua tahadhari za kinga dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19. Vilevile, natoa wito wananchi kujiepusha na taarifa zozote kuhusu UVIKO-19 kupitia watoa taarifa wasio rasmi.
Ile dawa ya Madagascar imeishia wapi? Tangu mheshimiwa aliyekwenda kutuletea alipoinywa kule haijasikika tena. Hata hivyo, baadae ilibainika alikunywa sampuli, si dawa.
 
View attachment 1863511
View attachment 1863512

TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI.

TAMKO LA KATAZO LA MISONGAMANO ISIYOKUWA YA LAZIMA

Tarehe 22 Julai, 2021 - Dar es Salaam.

Ndugu Wananchi, kama tunavyofahamu Tanzania iko kwenye mapambano ya kudhibiti maambukizi ya UVIKO-19 ikiwa ni wimbi la 3 la mlipuko huu tangu uingie nchini Machi, 2020. Itakumbukwa kuwa Wizara ya Afya na Viongozi wa Serikali kwa ujumla wake kwenye ngazi mbalimbali wamekuwa wakitoa taarifa, elimu na kuhamasisha juu ya kujikinga na kuwakinga wengine dhidi ya maambukizi ya UVIKO-19.

Ndugu Wananchi, Serikali inatambua kuwa wananchi walio wengi wamekuwa wasikivu, wakiitikia na kutekeleza miongozo yote ya kujikinga na kuwakinga wengine ingawa kwenye baadhi ya maeneo mwitikio umekuwa siyo wa kuridhisha. Hali hii imeendelea kuchangia kuongezeka kwa maambukizi na hatimaye kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa waliolazwa ambapo kufikia tarehe 21/07/2021 katika vituo vya huduma za afya kote nchini kulikuwa na wagonjwa 682 waliokuwa wanaugua maradhi ya UVIKO-19. Aidha, watalaamu wa afya wameendelea kupambana kwa moyo mmoja kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa wakati lakini hata hivyo baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakipoteza maisha.

Ndugu Wananchi, Wizara itaendelea kutoa takwimu hizi ili kwa pamoja tuendelee kufuatilia hali halisi ya mwenendo wa ugonjwa huu huku tukiendelea kuchukua hatua za kutosha. Aidha, ili kuimarisha zaidi kasi ya kupambana na kudhibiti maambukizi ya UVIKO-19
natamka kuwa, kuanzia leo tarehe 22/07/2021 nimekataza shughuli zote za misongamano yote isiyo ya lazima na ile yenye ulazima tahadhari ya kutosha ichukuliwe bila kuathiri shughuli za kiuchumi na kitaifa. Naelekeza Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwapa ushirikiano Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria ya Afya ya Jamii Na. 1 ya Mwaka 2009 na kuweka utaratibu mzuri kwa wale wanaoomba vibali vya shughuli zenye ulazima.

Ndugu Wananchi, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau wake wote itaendelea kutoa elimu na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miongozo yote ya afya. Aidha, natoa wito kwa wananchi wote kujiandaa kupata huduma ya Chanjo kama ambavyo Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyotoa taarifa jana tarehe 21/07/2021. Leo hii wataalamu wa afya wamekutana kupata mafunzo tayari kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa huduma ya Chanjo dhidi ya UVIKO-19 kwa hiari na bila malipo. Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.

Ndugu Wananchi, Wito wangu tuendelee kushikamana kwenye mapambano ya kutokomeza kabisa adui UVIKO-19 kwa kuzingatia utekelezaji wa afua zote za kujikinga na kuwakinga wengine zikiwemo;

  1. Kuhakikisha sehemu zote zinazotoa huduma za kijamii zinakuwa na miundombinu ya huduma ya kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni na kama maji hakuna kuwe na matumizi ya vitakasa mikono.
  2. Wananchi wote wanaotoa huduma za kijamii na wanaofika kupata huduma za kijamii wahakikishe wamezingatia afua za kinga zikiwemo kuvaa barakoa safi na salama.
  3. Kwenye maeneo ya huduma za kijamii zinazokutanisha watu kadhaa kupata huduma kanuni ya kuepuka misongamano izingatiwe kwa kuchukua tahadhari zote.
  4. Kwenye vyombo vya usafiri utaratibu wa kuepuka kubeba abiria kwa kusongamana uzingatiwe na kabla abiria hao hawajaingia kwenye chombo husika kuwe na utaratibu wa kuhakikisha wamezingatia tahadhari zote za kujikinga na kuwakinga wengine.
  5. Vilevile, nawakumbusha Wananchi tuendelee kuzingatia lishe bora, kufanya mazoezi na kutumia tiba asili zilizosajiliwa na baraza la tiba asili pasipo kuchelewa kufika kwenye vituo vya huduma kwa ushauri wa kitaalamu.
Aidha, natoa wito kwa viongozi wa serikali na wa sekta binafsi na taasisi zake zote kuonesha mfano kwa wananchi jinsi ambavyo wao wanatekeleza maagizo ya kuchukua tahadhari za kinga dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19. Vilevile, natoa wito wananchi kujiepusha na taarifa zozote kuhusu UVIKO-19 kupitia watoa taarifa wasio rasmi.
Huyu mama huwa simuelewi kabisa... Kwa nini asiwacoach watu namna ya kujifukiza kama alivyofanya enzi zile.
 
Unafiki mtupu!
Imekuwa unafiki tena? Si mlikuwa mnapiga kelele sana kwamba corona ipo Tanzania wakati ule serikali ilipokuwa inasema haipo? Sasa serikali inasema corona ipo Tanzania kuanzia Machi mwaka huu, nyie mnasema ni unafiki tupu. Wananchi wawaeleweje sasa? Akili yenu ikoje?
 
Tumesoma Tamko la Wizara ya Afya lenye kichwa: Tamko la Katazo la Misongamano isiyokuwa ya lazima" lililotolewa na kusainiwa tarehe 22 Julai 2021 na Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Dkt. Dorothy Gwajima (Mb.). Kwa mtazamo wetu, maudhui ya tamko hilo kwa kiasi kikubwa yanatoa mwanya kwa watu wa makundi mbalimbali kutoa tafsiri mbalimbali kuhusu maana ya 'misongamano isiyokuwa ya lazima'. Je, ni nani mwenye mamlaka ya kuamua kama msongamano ni wa lazima au sio wa lazima? Ni Polisi, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Mganga Mkuu wa Wilaya au Mkoa, Mwenyekiti wa Kijiji au Kitongoji, Diwani au Mbunge, Waziri, nk?

Je, msongamano ni nini na unaanzia watu wangapi? Je, misongamano kama ni yazima lakini ni hatarishi zaidi kwa maambukuzi ya Covid 19 inaweza kuruhusiwa kwa kuwa ni ya lazima? Je, misongamano kama siyo ya lazima inaweza kuzuiliwa hata kama siyo hatarishi kwa maambukuzi ya Covid 19? Maswali ni mengi zaidi kuliko majibu.

Kwa muono wetu, sisi Askofu Mwamakula tunaona kuwa katazo hilo linatoa mwanya wa manung'uniko ndani ya jamii. Kuna uwezekano mkubwa kwa watu wenye mamlaka wakawa wanatoa tafsiri ya neno 'misongamano isiyokuwa ya lazima' kwa lengo la kulinda maslahi ya tabaka hilo. Kwa sababu hiyo, tuna hofu kuwa mazingira hayo yanaweza kuleta misuguano katika jamii hasa endapo baadhi ya makundi yataonekana kubebwa na mengine kukandamizwa! Kwa sababu hiyo, tunatoa wito kwa Wizara husika kulichakata zaidi tamko hilo, vinginevyo litaonekana kama ni 'tamko la kisiasa' lisiloweza kutekelezeka zaidi ya kutaka kudhibiti baadhi ya makundi katika jamii na kuyainua mengine!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
 
Wangekuwa seriously..
au tungeona wa maana.
wangefungia nyumba za ibada
pamoja na kuzuia minada maana huko ndipo kuna mikusanyiko isiyokuwa na utaratibu maalumu.

unazua mikusanyiko huku, dala dala zinafurika.
huku minada (Sagula)
zikishika kasii?

huu utawala umeanza kuonesha makucha yake mapema sanaa.

na wasipokuwa makini utawahi KUISHA mapema zaidii
Kweli akina Samia wanajichanganya vibaya mno sijui kwanini wanakosa akili ndogo ndogo tu!
 
Tatizo la vuguvugu lolote la kuleta mabadiliko Tanzania huwa lipo mitandaoni tu not otherwise.

Tuna reference nyingi tu na juzi mzee wa escort ya balozi to Ubelgiji alitoa tamko watu wamwagike barabarani nani alithubutu?.

Kiukweli bado sana wasomi na watz kwa ujumla kuthubutu.
 
Nilitehemea watataj in za mikusanyiko hiyo, mfano harusi, mikutano ya kidini n kisiasa, sherehe mbalimbali , michezo, jumuiya za nyumba kwa nyumba, baa,.. N. K
 
Tumesoma Tamko la Wizara ya Afya lenye kichwa: Tamko la Katazo la Misongamano isiyokuwa ya lazima" lililotolewa na kusainiwa tarehe 22 Julai 2021 na Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Dkt. Dorothy Gwajima (Mb.). Kwa mtazamo wetu, maudhui ya tamko hilo kwa kiasi kikubwa yanatoa mwanya kwa watu wa makundi mbalimbali kutoa tafsiri mbalimbali kuhusu maana ya 'misongamano isiyokuwa ya lazima'. Je, ni nani mwenye mamlaka ya kuamua kama msongamano ni wa lazima au sio wa lazima? Ni Polisi, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Mganga Mkuu wa Wilaya au Mkoa, Mwenyekiti wa Kijiji au Kitongoji, Diwani au Mbunge, Waziri, nk?

Je, msongamano ni nini na unaanzia watu wangapi? Je, misongamano kama ni yazima lakini ni hatarishi zaidi kwa maambukuzi ya Covid 19 inaweza kuruhusiwa kwa kuwa ni ya lazima? Je, misongamano kama siyo ya lazima inaweza kuzuiliwa hata kama siyo hatarishi kwa maambukuzi ya Covid 19? Maswali ni mengi zaidi kuliko majibu.

Kwa muono wetu, sisi Askofu Mwamakula tunaona kuwa katazo hilo linatoa mwanya wa manung'uniko ndani ya jamii. Kuna uwezekano mkubwa kwa watu wenye mamlaka wakawa wanatoa tafsiri ya neno 'misongamano isiyokuwa ya lazima' kwa lengo la kulinda maslahi ya tabaka hilo. Kwa sababu hiyo, tuna hofu kuwa mazingira hayo yanaweza kuleta misuguano katika jamii hasa endapo baadhi ya makundi yataonekana kubebwa na mengine kukandamizwa! Kwa sababu hiyo, tunatoa wito kwa Wizara husika kulichakata zaidi tamko hilo, vinginevyo litaonekana kama ni 'tamko la kisiasa' lisiloweza kutekelezeka zaidi ya kutaka kudhibiti baadhi ya makundi katika jamii na kuyainua mengine!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Umeanza chokochoko!! Huu waraka ni kumbushio tu, hakuna kitu kigeni hapo!! Lengo kubwa hasa ni kuwapoza watu fulani waone tunatekeleza ushauri wa kidunia maana Tanzania siyo kisiwa japo kwa habari ya corona wapende wasipende, Mungu ameifanya Tanzania kuwa kisiwà!! Ndiyo maana wanaotutakia mabaya tuokote miili barabarani watasubiri sana!!
 
Najibu kutokana tu na headline kwani sijataka kupoteza muda kusoma unafiki wa serikali kudhani we the people are stupid and we can't read between the lines or rather that we can't read through them.
1)Watoto wetu wataendelea kuhudhuria masomo.
2)Kwenye mabasi ya mwendo kasi utatumika utaratibu gani.
3)Vipi kwenye mechi hasa hii 'Kariakoo derby' kule Kigoma mashabiki hawatakuwepo uwanjani?
4)Masoko kama Kariakoo yatafungwa au utatumika utaratibu gani?
5)Vipi kwenye nyumba za ibada, ibada zitasimamishwa kila mtu asalie nyumbani kwake mpaka pale tutakapoi-contain hiyo Covid19?
 
Back
Top Bottom