Bima ya Afya kwa wote huenda likawa ni kaburi la afya za Watanzania

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,148
Muswada wa Bima ya afya kwa wote ulifanikiwa kupitishwa bungeni mwezi uliopita, na tayari umetiwa saini na Rais wa Tanzania kuwa sheria rasmi, hivyo mchakato wa kutengeneza kanuni na taratibu za ufanyaji kazi kabla ya kuanza kutekelezwa umeanza rasmi.

Bahati mbaya sana watu wengi hawajui mifumo ya bima namna inavyofanya kazi, wengi wanadhani kupitia sheria hii watu wote watapatiwa bure Bima ya Afya (NHIF!) na kuneemeka na huduma zote za Afya popote pale hapa Tanzania bureeeee! Wakati hali ni tofauti kabisa. Kwa kifupi sana hakuna cha bure, kila mtanzania atapaswa kuchangia (direct&indirect) ili kuwezesha kila mtanzania anapewa huduma za afya.

Kwanini ninasema huenda kupitia hii sheria, afya za watanzania zikaishia kaburini, hizi ni sababu za msingi;

1. Mifuko yote ya bima za Afya iliyoanzishwa na kusimamiwa na serikali imeishia kulega lega au kufa!. Kwa mfano, serikali ilianzisha bima ya afya jamii (CHF) ikafa kabla ya kufikia hata robo ya malengo yake, ikaja na bima ya afya iliyoboreshwa (iCHF) kwa maeneo mengi imeshakufa na maeneo machache ambapo bado inafanya kazi iko mahututi. Pia serikali inasimamia Bima ya taifa (NHIF) ambayo kwa sehemu iko hoi (huduma nyingi zimeondolewa, vikwazo vya kujiunga ni vingi, uhuru wa kujitoa kwa wafanyakazi haupo, ufisadi unatisha, imekaa kibaguzi, haieleweki, hasara, hasara, hasara tupu) kiasi cha kushindwa kufikia mategemeo ya wanachama wake.

2. Ufahamu, mtizamo, mategemeo na desturi ya watanzania wengi kuhusu Bima au Bima ya afya ni duni. Kwa mfano, watanzania wengi wanawaza haya;

-Bima ya afya ipo kumtibu akiugua tu. Yaani atataka (atalipa) kuwa na Bima ya afya wakati anaumwa/kujihisi kuumwa tu, ili Bima ya afya itumike kulipa gharama ambazo angelipishwa hospitali kwa wakati huo.

-Bima ya Afya atagharamia huduma zote za matibabu yake.

-Bima ya Afya itawezesha kuwepo kwa huduma zote za matibabu kwenye kituo cha afya ambacho yeye atafika kupatiwa huduma.

-Bima ya afya itatumika kwenye hospitali zote (umma na binafsi), hivyo itampa uhuru kufika hospitali yoyote kupatiwa huduma.

3. Hakuna kiongozi yoyote wa serikali anayejua au aliyeweza kueleza kwa ufasaha na kueleweka na watoa/watumishi wa afya namna bima ya afya kwa wote atafanyakazi kiasi cha kuwa sawa, kupita au kutatua changamoto za bima za afya zilizokuwepo au zilizopo sasa. Bado ni fumbo gumu.

4. Kupitia sheria hii itapaswa mifuko iliyopo sasa ya Bima ya afya iliyopo chini ya serikali (CHF, iCHF, NHIF) kufa rasmi(kumezwa), kuunganishwa (kuwa chini ya mwamvuli mmoja) au kuongezewa majukukumu makubwa zaidi. Hii ni sintofahamu kubwa.

5. Zipo dalili, taarifa na viashiria vya wazi kuwa, kupitia sheria hii serikali itakuwa imejiondoa kugharamia moja kwa moja matibabu ya wananchi wake na kulikabidhi jukumu hilo kwa mifuko ya Bima ya afya itakayoanzishwa. Jambo hilo kama litatokea ni hatari kubwa sana kwa wananchi wa vijijini, wenye vipato duni na wanatoka katika mazingira magumu.

MUDA NI MWALIMU MZURI, NGOJA TUSUBIRI KUONA.
 
Shida ni usimamizi

Wakiweza kusimamia vizuri itafanya vizuri

Wakishindwa itafanya vibaya.

Kwa hiyo ni wao kuamua wasimamie vizuri au wafanye mambo as usual.
 
Naona kufeli kwa jambo hilo hata kabla ya kufanyiwa Kazi,kwa aina ya watu waliopo kwenye sekta za serikali ni ngumu kupata mafanikio yoyote.

Bima ya afya kwa wote ni sera ya CDM,lakini wazee wa Kushika Nyoka katikati {CCM} wanakurupuka tu,kama viwavi jeshi.
 
Naona kufeli kwa jambo hilo hata kabla ya kufanyiwa Kazi,kwa aina ya watu waliopo kwenye sekta za serikali ni ngumu kupata mafanikio yoyote.

Bima ya afya kwa wote ni sera ya CDM,lakini wazee wa Kushika Nyoka katikati {CCM} wanakurupuka tu,kama viwavi jeshi.
Tatizo imeletwa kusiasa sio kitaalamu lazima itaumba sanaa na evetually itakufa tu.
 
Pale serikali inapoonesha nia ya kufanya jambo tutoe ushauri wenye lengo la kuboresha ila isiwe kila jambo ni la hovyo. Angalau serikali ya awamu hii imethubutu kuanzisha hilo hata kama litaanza kwa mapungufu lakini ni jambo la kupongezwa. Unaposema serikali itakuwa imejiondoa rasmi kugharamia matibabu ya wananchi sijaelewa kwamba kwa Sasa serikali inasaidia nini kwa wananchi wa vijijini kugharamia matibabu!
 
Shida ni usimamizi

Wakiweza kusimamia vizuri itafanya vizuri

Wakishindwa itafanya vibaya.

Kwa hiyo ni wao kuamua wasimamie vizuri au wafanye mambo as usual.
CCM haina uwezo wa kusimamia jambo lolote likafanya vyema.
Historia tunayo.
Bima ya afya iliyo bora bila ya kuwa na vyanzo vya uhakika vya mapato hiyo ni mchezo wa kuigiza.
 
Shida serikali yetu ujanja mwingi, upigaji mwingi, wanafanya vitu kwa faida zao za kisiasa na mifuko yao.
 
Pale serikali inapoonesha nia ya kufanya jambo tutoe ushauri wenye lengo la kuboresha ila isiwe kila jambo ni la hovyo. Angalau serikali ya awamu hii imethubutu kuanzisha hilo hata kama litaanza kwa mapungufu lakini ni jambo la kupongezwa. Unaposema serikali itakuwa imejiondoa rasmi kugharamia matibabu ya wananchi sijaelewa kwamba kwa Sasa serikali inasaidia nini kwa wananchi wa vijijini kugharamia matibabu!
Tatizo sio kuanzisha Bima ya afya kwa watu wote bali nia ya serikali katika kuanzisha hicho kitu sio nzuri na iko tofauti kabisa na wengi wanavyotaka au kutegemewa.

Kuhusu ushauri, tayari ushauri mwingi sana umetolewa na watu mbali mbali lakini serikali imeupotezea kabisa. Moja ya ushauri mzuri zaidi uliotolewa ni serikali kuboresha mifuko iliyopo sasa kwa kupanua wigo wa watu wengi kunufaika, kuongeza usimamizi mzuri na kukuza ufanisi ili kufikia malengo ya kuanzishwa kwa mifuko hiyo.
 
CHF imekufa.
NHIF ipo hoi.
Bima ya watoto imekufa.

Hii sijui itaitwa "universal health insurance" itawezaje ku-survive?

Hatujawahi kuwa vizuri kwenye implementation, sio serikali wala mtu mmoja mmoja.
Nadhani sasa ni muda muafaka kwa Mh. Rais kumuondoa Ummi kwenye hii nafasi na kumuweka hapo mtu mwingine mwenye mawazo tofauti.
Naona kama mchango wa Ummi kwenye hii wizara umefikia mwisho.
Aidha wanao simamia hii NHIF hawana ushauri mzuri kwa Waziri nao ni wakupumzisha pia.
Hatuwezi cheza na afya za Watanzania
 
Universal Health Insurance was quite a brilliant idea but it's modus operandi and timing ndiyo shida.

Kufikia universal health insurance kungefanyika on gradual pace na siyo kuanzisha kama uyoga. Uyoga asubuhi unaona unachomoza kama kajani, ikifika usiku unakuta huo umejenga bonge la kofia.

Universal health insurance hata USA inawasumbua. Ulaya wamefanikiwa kwa kuwa vinchi vyao ni vidogo vidogo.

Hii haikufanyiwa homework ya kutosha.

NHIF imeziweka pepmbeni fundamentals za Afya.

PREVENTION is key kwenye afya, Kama unaongeza nguvu na focus kwenye Treatment tena tertiary unaacha focus ya prevention basi gharama za kutibu zitakuzidi tuu.

Sasa NHIF, the focus has always been the tertiary care.
Daktari bingwa ni wa tertiary care na Tertiary care haitakiwi kuwa ndio key driver wa strategy ya matibabu ya watu ! (It might be the major cost driver)

Wewe unaumwa kichwa unataka ukamwone Neurologist halafu NHIF inamlipa kama specialist. survival ni ngumu mno hapo!
Kwanza umemtumia mtu sio na umepoteza muda wake huyo specialist ambapo angeweza kuona mtu ambaye anamhitaji!

I believe focus ingwekwa kwenye prevention, na prevention hii sio tu ya kuzuia watu wasiumwe, bali hata wakiumwa ugonjwa usiende mbele! KWa mfano tukifuata mfumo wa referral uliokuwepo, ukiumwa anzia hapa na kule pa kuazia kunawekwa vizuri kiasi mtu anajiskia kuanzia. Ili vitu vigundulike mapema!
 
Tatizo ni kutokujenga hospitali ya taifa yenye uwezo wa kutibu magonjwa makubwa ,hu mgawanyiko wa mara Moi au Muhimbili au Jakaya au Mloganzila ndiyo chanzo Cha wagonjwa kupeteza mda mwingi kwenye hospitali Moja bila kujuwa tattzo lake siyo la hapo anapitibiwa.Ingekuwa vizuri zote ziwe hospitali ya taifa.
 
Back
Top Bottom