Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 118,221
- 219,400
Miongoni mwa siri zilizofichuliwa leo kuhusu Mkataba wa kuiuzia kampuni ya Waarabu Bandari za Tanzania, imo habari kwamba Bandari zitakazohusika ni zile za Tanganyika Pekee, za Zanzibar hazitahusika.
Ikumbukwe kwamba Bandari ni miongoni mwa mambo ya Muungano, ikiwa kama jambo hili lina faida kwanini tunaitenga Zanzibar. Je, Wazanzibar hawataki faida?
Bali kitu pekee ambacho tumekiona ni kwamba Waziri Aliyesaini Mkataba huu anayeitwa Makame Mbarawa anatokea upande wa Zanzibar kama alivyo Rais Samia Suluhu Hassan.
Pia soma > Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World
---
MAONI YA WADAU
Ikumbukwe kwamba Bandari ni miongoni mwa mambo ya Muungano, ikiwa kama jambo hili lina faida kwanini tunaitenga Zanzibar. Je, Wazanzibar hawataki faida?
Bali kitu pekee ambacho tumekiona ni kwamba Waziri Aliyesaini Mkataba huu anayeitwa Makame Mbarawa anatokea upande wa Zanzibar kama alivyo Rais Samia Suluhu Hassan.
Pia soma > Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World
---
MAONI YA WADAU
Mapato yatakayotokana na bandari za Tanganyika ni ya muungano na Zanzibar inapata mgao wake achilia mbali mgao wa 4.5% BoT kwa pato linalotokana na rasilimali za Bara.
Sasa hivi Zanzibar wana mpango wa kulipa wajumbe wa nyumba kumi mishahara. Tayari wazee wanalipwa pensheni na waliobaki wanatumia umeme bure. Hapo hawajui gharama za ulinzi , mambo ya ndani na nje au taasisi zingine za muungano.
Huyu Mbarawa anakuwaje waziri wa jambo lisilo la muungano? Sasa Rais wa JMT ni Mzanzibar, Rais wa SMZ ni Mzanzibar na Waziri ni Mzanzibar. Nani anamtetea Mtanganyika kwa usawa huo.
Uuzwaji wa bandari hauna uchungu isipokuwa kwa Watanganyika.
Nyerere, Mkapa, Kikwete , JPM walijua hilo hawakuwahi kufikiria. Walijua ni rasilimali na hazina za Watanganyika
Mwinyi aliuza Loliondo ''ujombani'' akiwa na Waziri Diria. Historia bwana!
JokaKuu Pascal Mayalla