Mamlaka ya Bandari (TPA) yatoa ufafanuzi kuhusu hali ya ajira za Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,815
4,565
1711138014712.png

UFAFANUZI KUHUSU HALI YA AJIRA ZA WATUMISHI KAΤΙΚΑ BANDARI YA DAR ES SALAAM
Ijumaa 22 Machi, 2024 DAR ES SALAAM

Jumatano tarehe 20 Machi, 2024 Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ilitoa taarifa kwa Watumishi wake kuhusiana na mabadiliko ya uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, Gati namba sifuri (RoRo) hadi Gati namba saba.

Mabadiliko hayo yanatokana na Mkataba kati ya TPA na Kampuni ya DP World ya Dubai kuhusu uendeshaji na uendelezaji wa Gati namba 0-7 za Bandari ya Dar es Salaam kwa kipindi cha miaka thelathini (30) kuanzia tarehe 22 Oktoba 2023.

Kutokana na mabadiliko hayo katika usimamizi na uendeshaji wa maeneo tajwa, Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam walitakiwa kuchagua ama kubaki TPA au kusitisha mkataba wa ajira na TPA na kuajiriwa na DP World papo hapo.

Menejimenti ya TPA ilitoa taarifa hiyo kwa Watumishi baada ya kukamilisha pro- gramu maalum ya kuwaelimisha na kutoa ufafanuzi wa kina na taarifa sahihi kuhusiana na mabadiliko tajwa kwa Watumishi wake.

Katika taarifa ya Menejimenti, Watumishi watakaoridhia kujiunga na DPW kwa hiyari walielekezwa kuwasilisha taarifa zao (Notice) katika Ofisi zilizopo ghorofa ya 32 katika Jengo la Makao Makuu ya TPA (One Stop Centre) kabla au ifikapo tarehe 29 Machi, 2024. Aidha, Watumishi ambao hawatapenda kujiunga na DP World watabaki TPA kwa kuwa Mamlaka itaendelea kuhitaji Watumishi watakaotoa huduma katika Bandari zake zinazoendelea kuboreshwa katika maeneo mbalimbali Nchini.

Kwa kuzingatia ufafanuzi hapo juu, Menejimenti ya TPA inapenda kuujulisha Umma kwamba, taarifa inayosambaa ilitolewa kwa ajili ya Watumishi na TPA ilifanya hivyo ili kukamilisha taratibu za kuhamisha huduma kwa DP World.

TPA inauhakikishia Umma kwamba, itaendelea kuwathamini Watumishi wake ambao ni rasilimali muhimu zaidi katika Mamlaka na katika utekelezaji wa zoezi hili, maslahi ya pande zote husika yatazingatiwa kikamilifu kwa mujibu wa Sheria za Nchi yetu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Masoko na Uhusiano,
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (ΤΡΑ)

Habari zaidi, soma:
  1. Sakata la DP WORLD: Rais Samia asema Serikali itatafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar, sasa kuchangia robo tatu ya bajeti ya nchi
  2. - DP World wadaiwa kuanza mchakato wa kuajiri, Wafanyakazi wa TPA wadaiwa kutakiwa kuchagua kwenda DWP au kubaki TPA
 
Tuliwakatalia Oman na China kama awataki mkataba wa miaka 33 bandari ya Bagamoyo uwekezaji wa $10 billion dollars.

Halafu tumeenda wapa Dubai miaka 30 kwa uwekezaji wa $500m huku wanachukua sehemu kubwa ya Dar port.

Haki ya mungu hii nchi, uwekezaji wa DP World ni kweli unatija na strategic lakini ndio miaka 30.

Excuse my language sijapata kuona nchi ina viongozi wasiojielewa kama Tanzania. Hiyo hela DP world si anarudisha chini ya miaka minne tu.
 
Hawa wafanyakazi hawakupaswa kupewa jukumu la kuchagua TPA au DP World. Nionavyo mimi ilitakiwa TPA kukabidhi wafanya kazi wote waliokuwa chini ya TPA kwa DP world, Muundo wa TPA uvunjwe na ubaki uongozi wa TPA kusimamia tu uendeshaji wa DP world na kuhakikisha hawa DP World hawatanyanyasa wafanyakazi na kuhakikisha malipo yao yanafuata makubaliano ya mkataba, na kuhakikisha mkataba wenyewe unaenda kama ulivyopangwa.

Sasa TPA inabaki kufanya nini ilkiwa DP World anapewa Bandari ya Dar es Salaam na zingine na za maziwa yote, kama sikukosea mkataba ulikuwa unasemaje.

TPA iji disolve yenyewe, wafanyakazi wote waende kule DP World kwa mama Kizimkazi.
 

UFAFANUZI KUHUSU HALI YA AJIRA ZA WATUMISHI KAΤΙΚΑ BANDARI YA DAR ES SALAAM
Ijumaa 22 Machi, 2024 DAR ES SALAAM

Jumatano tarehe 20 Machi, 2024 Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ilitoa taarifa kwa Watumishi wake kuhusiana na mabadiliko ya uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, Gati namba sifuri (RoRo) hadi Gati namba saba.

Mabadiliko hayo yanatokana na Mkataba kati ya TPA na Kampuni ya DP World ya Dubai kuhusu uendeshaji na uendelezaji wa Gati namba 0-7 za Bandari ya Dar es Salaam kwa kipindi cha miaka thelathini (30) kuanzia tarehe 22 Oktoba 2023.

Kutokana na mabadiliko hayo katika usimamizi na uendeshaji wa maeneo tajwa, Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam walitakiwa kuchagua ama kubaki TPA au kusitisha mkataba wa ajira na TPA na kuajiriwa na DP World papo hapo.

Menejimenti ya TPA ilitoa taarifa hiyo kwa Watumishi baada ya kukamilisha pro- gramu maalum ya kuwaelimisha na kutoa ufafanuzi wa kina na taarifa sahihi kuhusiana na mabadiliko tajwa kwa Watumishi wake.

Katika taarifa ya Menejimenti, Watumishi watakaoridhia kujiunga na DPW kwa hiyari walielekezwa kuwasilisha taarifa zao (Notice) katika Ofisi zilizopo ghorofa ya 32 katika Jengo la Makao Makuu ya TPA (One Stop Centre) kabla au ifikapo tarehe 29 Machi, 2024. Aidha, Watumishi ambao hawatapenda kujiunga na DP World watabaki TPA kwa kuwa Mamlaka itaendelea kuhitaji Watumishi watakaotoa huduma katika Bandari zake zinazoendelea kuboreshwa katika maeneo mbalimbali Nchini.

Kwa kuzingatia ufafanuzi hapo juu, Menejimenti ya TPA inapenda kuujulisha Umma kwamba, taarifa inayosambaa ilitolewa kwa ajili ya Watumishi na TPA ilifanya hivyo ili kukamilisha taratibu za kuhamisha huduma kwa DP World.

TPA inauhakikishia Umma kwamba, itaendelea kuwathamini Watumishi wake ambao ni rasilimali muhimu zaidi katika Mamlaka na katika utekelezaji wa zoezi hili, maslahi ya pande zote husika yatazingatiwa kikamilifu kwa mujibu wa Sheria za Nchi yetu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Masoko na Uhusiano,
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (ΤΡΑ)

Pia soma:
- DP World wadaiwa kuanza mchakato wa kuajiri, Wafanyakazi wa TPA wadaiwa kutakiwa kuchagua kwenda DWP au kubaki TPA
Ufafanuzi unaendelea au wamemaliza?
 
Hawa wafanyakazi hawakupaswa kupewa jukumu la kuchagua TPA au DP World. Nionavyo mimi ilitakiwa TPA kukabidhi wafanya kazi wote waliokuwa chini ya TPA kwa DP world, Muundo wa TPA uvunjwe na ubaki uongozi wa TPA kusimamia tu uendeshaji wa DP world na kuhakikisha hawa DP World hawatanyanyasa wafanyakazi na kuhakikisha malipo yao yanfuata makubaliano ya mkataba, na kuhakikisha mkataba wenyewe unaenda kama ulivyopangwa.

Sasa TPA inabaki kufanya nini ilkiwa DP World anapewa Bandari ya Dar es Salaam na zingine na za maziwa yote, kama sikukosea mkataba ulikuwa unasemaje.

TPH iji disolve yenyewe, wafanyakazi wote waende kule DP World kwa mama Kizimkazi.
Prof mbarawa alaanike kwa kisasi chake chote
 
Back
Top Bottom