sodoliki
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 2,593
- 2,016
Nahisi serikali imepunguza matumizi yasiyo na maanaFaiza alipotelea wapi?kipindi cha JK alikuwa anashinda humu usiku na mchana kukitetea chama,tangu jiwe ashike madaraka haonekani tena
Nahisi serikali imepunguza matumizi yasiyo na maanaFaiza alipotelea wapi?kipindi cha JK alikuwa anashinda humu usiku na mchana kukitetea chama,tangu jiwe ashike madaraka haonekani tena
Nataman hili bandiko lako lifike Wizara ya Fedha na Magogoni maaana ni ujumbe wenye dhahabu.Na Thadei Ole Mushi.
Nasikia Dr Mpango huko bungeni kakubali kuwa uchumi umedorora kutokana na ukusanyaji wa Kodi kuwa mdogo. Huyu aliyekiri hivi ni waziri wa Fedha hivyo sina mashaka na chanzo chake cha Takwimu.
Haya Dr Mpango anayoyaeleza Leo binafsi niliwahi kuyafafanua hapa kipindi cha nyuma na kuhoji Washauri wa Rais katika maswala ya kiuchumi ni akina nani? Niliandika October 2017 kuwa:-
#Kila siku ikitoka ripoti ya utafiti kuhusu magonjwa ya akili lazma Tanzania iongeze asilimia zaidi ya jana na juzi. Tafiti zimekuwa zikitoka kila siku kuwa watanzania mara wana uwezo mdogo wa kufikiri, mara kila penye watanzania wanne mmoja wao ni kichaa, Mara Tanzania yaingia Kumi bora kwa raia wake kukosa raha yaan wanaishi kwa masikitiko nk.
#Haya ni magonjwa ambayo hushughulikiwa kisaikolojia zaidi kuliko kudungwa sindano au kupewa dawa. Yaani Tiba yake ni ya Kisaikolojia wakikupiga Sindano wanataka tu ulale usiwasumbue.
#Kama watanzania watapata mahitaji yao yote ya msingi inawezekana matatizo haya yakapungua kwa kiasi kikubwa.
Mwanasaikolojia Abraham Maslow aliwahi kutoa nadharia ya kinachoweza kummotivate mtu, katika nadahria yake hiyo (hierarchy theory) anadai mahitaji ya msingi ya mtu kwanza ni Psychological needs yaani mtu apate chakula kizuri, alale pazuri, apate maji nk ndio anaweza kufikiria mambo mengine.
Kwa hiyo kusononeka huko kwa watanzania kunaweza kuondolewa kwa kupata mahitaji hayo..... Hii ina Maana hata kama tutakimbizana na miradi mikubwa kama ya reli, fly over na Ununuzi wa ndege bado kama RAIA hawatapata mahitaji ya Msingi wataendelea kunungunika tu.
#WATAALAMU WA UCHUMI WANAWEZA KUWA TIBA YETU YA KWANZA.
#Watanzania kwa sasa hasa vijana ambao ni asilimia 35 ya watanzania wote ukiwauliza wanahitaji nini wengi watakuambia ni ajira yenye uhakika. Ukichukua asilimia 35 ya vijana wote wa Tanzania kwa mujibu wa sensa ya 2012 ni sawa na vijana 15, 750,000. Idadi hii haiwezi kuajiriwa hata nusu yake na Serikali. Hapo hatujagusa watu wazima ambao ni asilima 21 ya watanzania wote, hapo hatujagusa waliovuka umri wa utoto na kuwa vijana kwa kuwa sensa hii ilifanyika 2012.
#Kitu pekee ambacho kingeweza kutusaidia hapa ni Sector binafsi. Kwa jinsi mambo yanavyokwenda Tanzania Sector Binafsi inazotota siku hadi siku.
#Tanzania kuna Jumla ya makampuni makubwa ambayo ni (Corporate) 37 tu haya ni yale yenye mtaji mkubwa wa kuanzia bilioni 1 na kuendelea. Haya ndiyo yenye uhakika wa kutoa ajira. Kati ya hayo 8 ni ya Serikali na moja halifanyi kazi (eagle air) kwa hiyo yanabakia 28 tu ndiyo yanayoweza kuajiri watu zaidi ya elfu moja na kuwapa mikataba ya kazi haya mengine hayana uwezo huo. Pitia Link ifuatayo kuyaona makampuni hayo.
List of companies of Tanzania - Wikipedia
#Utafiti uliofanywa na Baclays bank 2012 unaonyesha kuwa kwa wakati ule Tanzania ilikuwa na makampuni haya makubwa 18 tu hii ni kabla ya kuja kina Dangote na wengineo. Wakati kwa Wenzetu Kenya makampuni makubwa kama hayo (Corporate) yalikuwa 500 unaweza kuona namna wenzetu walivyowekeza vizuri kwenye Sector binafsi.
#Kama hatutaangalia kwa mapana Sector hii binafsi huko mbeleni tutakuwa na tatizo kubwa mara Dufu la ajira. Serikali nayo itaparalyse kiuchumi. Makampuni haya ndio walipa kodi wakuu wa nchi hii na kama watatusaidia kuajiri maana yake wananchi nao watalipa kodi na mzunguko wa hela utakuwa mkubwa.
#NINI KIFANYIKE.
#Serikali isiwaze kwanza Kodi kubwa kwenye makampuni haya ila yawawezeshe ili yaweze kujiendesha.
#Serikali iwatambue wafanyabishara na wajasiriamali wa kati (SME) na itengeneze sera nzuri za kuwafanya wafikie kuwa makampuni makubwa.
#Kwa sasa inaonekana kama kuna vita kati ya Serikali na Wafanyabiashara yaani kila wakitaka kuibuka wanawatwanga Kodi wanafia hapo hapo na wanarudi mtaani.
#Serikali Isimhukumu mtu mwenye pesa nyingi kuwa ni Fisadi bali atengenezewe mazingira ya namna ya kumkuza ili watanzania wengine waajirike.
#Serikali isiache kuendelea kufanya biashara na Sector binafsi. Kwa mfano kitendo cha kutumia Jeshi kusambaza madawa na vifaa vya maabara wangeliweza kuwapa sector binafsi kufanya hivyo ili mzunguko wa hela uwafikie Raia.
#Kuna viashiria vya watu kuficha fedha mfano mabenki yanapofanya mnada kwa sasa watu wanashindwa kununua mali hizo. Hata nyumba za Lugumi kukosa wateja ni kiashiria cha kwamba matajiri wanaficha fedha zao. Serikali iangalie ninmazingira gani yanafanyike ili watu watumie fedha.
#Mzunguko wa Dola ni mkubwa kuliko Shilingi yetu ya ndani. Katika maduka ya kubadilishia fedha kuna tetesi dola ndio nyingi kuliko Shilingi yetu..... yaani ni maduka machache sana unaweza kupata milioni 100 kwa wakati mmoja kwa maana hiyo fedha hazipo kwenye mzunguko.
Kwa ufahamu huu mdogo wa kiuchumi wachumi wetu wanaofanya kazi kwa niaba ya Rais wanaweza kufanya mambo na magonjwa haya ya akili yakapungua.
LEO NOVEMBER 2018.
Kuna mambo ambayo bado yanafanyika yatakayotupunguzia Fedha za Kodi. Mfano kitendo cha kutekwa kwa Mo na watu wasiojulikana kimetafsiriwa kama kuwadisturb wafanyabiashara wakubwa ambao ndio walipa kodi wakubwa. Hili Litatuathiri baadaye.......
Operation tunazoziendesha kabla ya kuziendesha tuangalie Mikataba ya Kinataifa inasemaje. Naona aibu Kubwa kwa Waziri wangu kujitokeza Hadharani na Kusema kuwa anawalinda Mashoga.
Lazma waziri aaibike kwa kuwa anataka kuzilinda asilimia 40 za fedha ya budget toka njee. Kwa maana hiyo tunapotaka kufanya kitu lazma tufikiri kwa kina sana.
Siasa iliyoingia kwenye maswala nyeti kama ya Korosho nayo tukicheza yatatuumiza Mbeleni kiuchumi na Kisiasa.
Tukishafanya Matanga ya Mbaazi na kuna mtu aliwaambia wakulima waliokuwa wanatafuta Soko kuwa Mbaazi ina protini nyingi hivyo waile. Ndio majibu ya wataalamu wetu haya.....
MATATIZO TULIYONAYO BADO NI MAKUBWA.
Ajira kwa vijana, Mfumuko wa Bei kwa bidhaa za Ujenzi kama Semeti na Bati.
Kushuka kwa bei kwa mazao.Kuna haja ya kufikiria maeneo hayo kwa Kina sana.
Bidhaa muhimu kama Sukari nayo imepanda sana.
Tujadiliane kwa maslahi ya Taifa
Ole Mushi
0712702602View attachment 926193
kweli kabisa boss kwenye ushauri kuna options tatu kuuchukua au kuupotezea au kusave kwa matumizi ya baadae akili ikikua.mwisho wa siku utabaki kuwa ushauri tu wauchukue au wauache
MTOTO MAFTA MAFTA
Wawekezaji wa mitaro na maji taka??Ningekua mimi ni rais ningemwamuru kila mwakilishi wa tz (balozi) analeta wawekezaji wasiopungua 100 kuja kuwekeza kwa kujenga viwanda tz kila mwaka
Ningeweka hiyo kama qualification ya kuteuliwa kuwa balozi
Duniani kuna nchi 195 tuchukulie 80 duniani zina uchumi imara hapa nazungumzia uchumi mkubwa na wa kati
Viwanda 100 kila balozi avilete kwa nchi 80?
100×80=8000
Hapo ni viwanda 8000
Viwanda 8000 kila mwaka kwa miaka 5?
8000×5= 40000
Hapo jee hatutafikia uchumi wa kati? Hapo sijaweka viwanda vya wazawa, mapato ya kawaida ya tra, utalii nk
Jpm angefanya hivi toka kaingia 2015 leo tungekua mbali sana