Don't take it personal, we have been wasted by our leaders ,With all resources that we have,it doesn't make any sense that we r in this lower category of middle income economy few steps from ldc...we should've been an upper middle income like Botswana, Namibia or South Africa simply because we have everything.Inauma sana
Mambo ambayo Mwenyezi Mungu kwa busara yake aliwapa nyinyi na sisi tukakosa. Aliyekupa kiti ndiye aliyenipa kumbi. Haya mambo yote ambayo nitayataja nyie mnayo na sisi hatuna.
Nyie mna:
1.Gesi
2. Dhababu
3. Diamond (almasi)
4. Madini ya Chuma (iron ore)
5. Tanzanite
6. Lithium
7. Nickel
8. Cobalt
9. Silver
10. graphite
11. Uranium
12. Shamba kubwa yenye rutuba
13. Mnapokea mvua nchi nzima na hamna maeneo kame.
14. Mna watu wengi yaani mna nguvu kazi ya kutosha (watu 60 million na zaidi ya watu 20 million wana umri wa kufanya kazi).
15. Mnamiliki 49% ya Lake Victoria.
16. Mnamiliki asilimia kubwa ya Lake Tanganyika.
17. Urefu wa ufuo wa bahari wa Tanzania ni zaidi ya 800 km.
18. Mumezungukwa na majirani wanane mnaoweza kufanya nao biashara.
19. Mna amani hamjawahi kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Kenya tuna matatizo haya:
1. Hatuna madini kwa wingi isipokuwa soda ash na titanium.
2. Maeneo ya magharibi na kati ya Kenya ndio huwa yanapokea mvua ya kutosha. Maeneo ya Kaskazini hayapokei mvua yoyote hata tone. Mashariki inapokea mvua kidogo sana na hao watu huwa na shida ya ukame pia.
3. 25% ya ardhi ya Kenya ndio ina rutuba. 75% ya ardhi ya Kenya haina rutuba na mimea haimei vizuri kwenye ardhi hio au haimei kabisa.
4. Kenya ina watu 50 million wakati Tanzania ina watu 60 million. Kwa hivyo Tanzania ina nguvu kazi kubwa kushinda Kenya.
5. Kenya inamiliki 6% pekee ya Lake Victoria.
6. Kenya ina majirani watano pekee.
7. Ufuo wa bahari wa Kenya ni 500 kilometres pekee.
8. Kenya tuna amani lakini hatufikii amani ya Tanzania kwa maana sisi tumewahi kuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe mara kadhaa kwa mfano mwaka wa 1992 na 2007.
Lakini cha kushangaza ni kwamba licha ya matatizo ya Kenya, bado Kenya ina gdp, gni per capita na hdi kubwa kushinda Tanzania.