Acheni Mama awe mkweli.
Bora CCM ife ili maisha watu wengi yawe mazuri. Mlipenda Sana kuaminisha watu vitu vya kwenye makaratasi lakn ukweli mnaujua. Hebu angalia mlivyoipamba ile project ya Mindege,Kumbe ni hasara tu tangia inunuliwe
 
Ilani lazima kuendana na utawala bora, sio unafanya miradi na wakati huo unakanyaga haki za WATU na katiba, pili vyema tukajua tu mwendazake alitamka wazi ukimshauri unaaribu, so makamu wenda ndio alikuepo KWA mjibu wa katiba ila nafasi ya kushauri wenda ilikua mdogo Kama ngamia pita kwenye tundu la sindano ,
 
Mkuu samahani Naomba Unifafanulie Sikusikiliza Hotuba Yake,
Unaposema Miradi Mingine ipo Kwenye Makaratasi Una maanisha Nini?
Yaani Stiegliers iachwe?
Au Kuna Miradi Mingine inakuja Ipo Ktk Makaratasi Au hii iliopo ipo kwwnye Makaratasi tuu?
Nifafanulie Mkuu Ahsante!
 
Mama Samia achana na cheap popularity haitakusaidia lolote unatakiwa usiwe muongeaji sana maana naona unaanza kutoboa matundu ya hela wakati huo ukiwa umewekwa kwenye mtego mgumu na mzito sana wa ilani yenye kurasa 300 ya kutekeleza miradi yote iliyoko kwenye ilani

Yaani kumbuka sasa hivi hauko kwenye meli mpya uko kwenye meli ileile sema tu imepata mawimbi katikati ya safari

Mama nimekushangaa sana unaposema kuna miradi mingine iko kwenye makaratasi wakati wewe na Hayati Magufuli ndio mliotembea nchi nzima kuinadi kwa hiyo tunataka ahadi zilizoko kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi

Tofauti na hapo hatutakuelewa tutanyima kura 2025 kama ukitaka kuomba ridhaa ya kugombea tena

Jitahidi sana kwenye suala la kodi usiwalaumu tu TRA waonye hata wafanyabiashara pia maana ni wakorofi.

Screenshot_20210406-202807.png
 
Mimi namshangaa sana Mama.....cheap popularity itammaliza
TIMU CHATO naona mnaanza kazi rasmi sasa baada ya mipango yenu niwaambie tu mmesha feli kabla hamjaanza MAMA HAKWAMI NG'OO! Kubalini kwamba huyo mungu mtu wenu kesha chukuliwa ili taifa lipone na mipango yake miovu na si vinginevyo

RAIS sasa ni SAMIA SULUHU HASSAN hakuna mjadala mtake msitake.
 
Kurasa 300 sio hoja, ni kipi kinatekelezeka ndani ya hiyo ilani hilo ndio la msingi. Mama anataka kodi lakini sio ya dhuluma, Magu alikuwa hakusanyi kodi tu, bali alikuwa anaendesha dhuluma kwa kisingizio cha kodi.Hiyo miradi huyo mama anajua baadhi ni utapeli wa wazi ndio maana akawa anaitaja.

Na kwa taarifa yako huyo mama huna lolote la kumtisha kuhusu kura, maana anajua fika ccm iko madarakani kwa wizi wa kura, na cheo cha urais ndio mbeleko ya ushindi wa ccm. Huyo mama akiaamua ushindani wa halali bila kutumia cheo chake, hiyo ccm itaifuata KANU ya Kenya hata kesho asubuhi.
 
TIMU CHATO naona mnaanza kazi rasmi sasa baada ya mipango yenu niwaambie tu mmesha feli kabla hamjaanza MAMA HAKWAMI NG'OO! Kubalini kwamba huyo mungu mtu wenu kesha chukuliwa ili taifa lipone na mipango yake miovu na si vinginevyo

RAIS sasa ni SAMIA SULUHU HASSAN hakuna mjadala mtake msitake.
Mama Samia ameshasema KAZI INAENDELEA! kwa hiyo kila kitu kinaendelea kama kawaida sasa nyinyi mnaoomba eti apige chini miradi ya ilani ya CCM mnapoteza muda wenu tu. Hangaikeni na Saccos yenu.
 
Back
Top Bottom