Wanne mbaroni kuhusiana na kesi ya James Temba

Wanne mbaroni kuhusiana na kesi ya James Temba

Huyu Lema ndo aliyepiga simu kwa mama yake na Temba akimuuliza kama Temba yupo nyumbani au la? Alipojibiwa hayupo alikata simu na kuizima alidhania yameisha.

Biashara ya kuuwana uchagani Iko sana mnauana kisa Nini? Pesa au mapenzi? Tangu lini mkajua mapenzi nyie?
mambo ya recycle bin hayo
 
Hapo ukiunganisha Dots si unaona kwamba Afisa Maabara Demu wake ni Happiness na James temba alikuwa anakula Happiness ,so Ofisa Maabara ikabidi akodishe hao Masela "Mputo" na "Tambali" ndiyo wakamaliza kazi ,Hayo majina yanaonyesha ni "MANDONGA WATU KAZI".
Pia Kigogo kati ni maskani ya vibaka wengi
 
Ndio huyo mkuu, mpaka leo sijaona updates yake kama jamaa walikamatwa au yule dada sijui alifariki au La watekaji walipatikana. Ilikua story kubwa humu JF. Hamnaga updates bongoland.
Yule dada alifariki mbona maana si walimchoma moto

Ile kesi haikusikika tena

Ova
 
Nuzulati Scott junior magnifico Jerusalem2006 Aizat

Tulipoingia kwenye kikao, wakasema wale wote mliowakamata hawajui lolote katika tukio la kulipua Ubalozi. Wakatuuliza tunaweza kupata askari anayelifahamu vizuri Jiji la Dar es Salaam? Tukawaambia ndiyo. Wakasema mleteni. Akaletwa (jina linahifadhiwa) kutoka makao makuu. Wakamuuliza unafahamu eneo linaloitwa Kimara? Akasema ndiyo. Wakasema tupeleke.....

Inaendelea......

“Aliwapeleka hadi Kimara. Wakamuuliza unaifahamu gereji ya (jina linahifadhiwa), akasema ndiyo. Wakamwambia tuonyeshe. Aakawapeleka hadi gereji. Pale gereji wakasema fundi anayeitwa (jina linahifadhiwa) yuko wapi? Akaitwa huyo fundi akaja. Wakajitambulisha kwake na kumweleza kuwa wao ni FBI kutoka Marekani na wanafuatilia ulipuaji wa Ubalozi wa Marekani. Wakamsihi asiwe na wasiwasi hawatamkamata, bali awape ushirikiano na taarifa watakazomwomba, ikiwa anazo.

“Wakamuuliza. Wiki mbili zilizopita ulitengeneza boksi la chuma hapa gereji? Akasema ndiyo. Wakamuuliza huyo mteja mlikuwa mnafahamiana? Akasema hapana, ila alikuja hapa alikuwa na kanzu nyeupe na ndefu nyingi, akanielekeza nimtengenezee boksi la aina hiyo.

Wakamuliza kama anajua anapoishi huyo mtu, akasema hajui. Wakamwambia alipigiwa simu na huyo mtu siku… baada ya hapo huyo fundi gereji waliongozana naye kwenda maeneo ya Ilala na kwingine ambapo walikamatwa watu wawili waliosaidia Ahmed Khalfan Ghailani kukamatwa nchini Pakistan na akawataja wenzake. Watu 14 dunia nzima walikamatwa na kuwekwa katika Gereza la Guantanamo Bay, Marekani.
Asante mkuu 🙏
 
Aah wap, kama mawasiliano yalikuwepo,oda akatoa ,muamala ukasoma atatokaje hapo Mzee?
Tambua kwamba Ofisa maabara hakushika shoka/kisu/panga kumchicha Temba na anaweza akawaambia Detectives waonyeshe DNA traces yake kwenye vielelezo kama alihusika kumuua Temba.

Issue za kumtia mtu hatiani inatakiwa kusiwe na loopholes za kuponyoka.
 
Wakitrace simu na mawasiliano yakaonekana kuwa alishawasiliana n a hao killers hakuna sehem atachomokea regardless alikuwa kilimanjaro
Kama namba ya simu labda imesajiliwa kwa jina lake hapo sawa ila kama jina la mtu mwingine anaruka FUTI 100.
 
Kesi za bongo hazinaga updates labda iwe kesi ya siasa. Kuna dada mmoja alitekwa kule kibaha akaenda akatupwa akaja kuokotwa hoi sijui alifariki au vipi, uzi wake uliwekwa humu na kuna jamaa wakawa wanajibu hoja kama vile ni washiriki wa waliomteka. Mpaka leo hamna updates wala kesi iliishia wapi. Bongo is like a jungle, survival for the fittest. 😀 😀 😀 😀
Yule alifariki, anaitwa martha kama sikosei
 
Mfano anaoponda system hapa JF ukisikia kauawa kikatili nani atamfahamu? maana wengi hapa ni fake IDs, unakuja kurubunika PM unatoa location, umeisha..

Mimi kiukweli imani na polisi sina. Kila wanachoongea naona ni uongo, siwaamini kabisa.
Kuna washenzi ni wakongwe humu, eti waakafurahia mfumo mpya wa jf utakao kuwa unaonesha location ya mchangiaji eti kuwadhibiti matapeli, elimu yetu Huwa ni fake, Haina msaada kama great thinker wa jf anashadadia huu mfumo bila kuangalia mbele, inafikirisha sana
 
Baba wa Marehemu wakati anahojiwa, alisema kuna bint alipiga simu na kuumuliza James, wakati familia inamtafuta, walipoipiga tena haikupatikana tena.....
Ukute hapo walikuwa washafanya yao sasa ameanza kuhangaika na damu ya mtu akapiga simu ili awape ishara flani washtuke labda, yaani basi tu yaani inauma mno
 
Aisee yaani mgeni anaijua Nchi kuliko mwenyeji kweli sie bado tunaishi enzi za ujima.
Watujua vizuri sana, ndio maana kunakuwa na uzito sana hata kuita wachunguzi kutoka nje wa matukio kama MO29, wale wakija itakuwa balaa.
 
Sheria ifate mkondo wake
Inasikitisha zaidi ya sana "APUMZIKE KWA AMANI JAMES TEMBA"
 
Ha ha ha pretty, kwani hio handset si kopo tu? Data zote zinabaki kwenye server za service provider. Wachunguzi wanaonba namba zote zilizowasiliana/alizowasiliana na victim. Wanaanza kufuatilia trend kama kuna msg ndio rahisi zaidi. Pia mawasiliano yataonesha waliowasiliana nae walikuwa wapi(minara ndio inasema hapa). Sasa wewe wadanganye siku ya tukio ulikuwa Rombo huku simu yako inaonesha uliitumia ukiwa Mbagala.
Ulikuwa Rombo wakati ulikuwa mbagala ni mstari muhimu sana lazima wakuminye.
 
Pia mawasiliano yataonesha waliowasiliana nae walikuwa wapi(minara ndio inasema hapa). Sasa wewe wadanganye siku ya tukio ulikuwa Rombo huku simu yako inaonesha
Hivi wakiingia huko kwenye mtambo wao si wanaweza pata na kuchukua Hadi voice note ambayo ni maongezi ya mipango hiyo ya mauaji ya hao majamaa?
 
Back
Top Bottom