Wanne mbaroni kuhusiana na kesi ya James Temba

Wanne mbaroni kuhusiana na kesi ya James Temba

Tena vijana ndo makatili vibaya vibaya!

Kuna mahali nimeona eti huyu dogo alikuwa anamiliki kale karoho ka "Utapeli"
Maana eti ni mwanachuo still alikuwa winga kkoo, so ukilogwa kumpa pesa akuletee hizo iPhone zao, umekwisha, simu hupati na hela hakupi, last time nasikia kalala mbele sijui na milioni tatu za iphone...

Kumbuka hawa watuhumiwa ni vijana na hizo simu ndo roho zako so jiongeze!
Wewe sikia tu kuhusu utapeli , unauma sana .
 
Mfano anaoponda system hapa JF ukisikia kauawa kikatili nani atamfahamu? maana wengi hapa ni fake IDs, unakuja kurubunika PM unatoa loation, umeisha..

Mimi kiukweli imani na polisi sina. Kila wanachoongea naona ni uongo, siwaamini kabisa.
Na hiyo watu kutokuwa na imani na polisi,ina wapa njia watenda maovu,maana wanajuwa tukifanya tukio la kumteka mtu au kuua
Raia mtu wa kwanza kumhisi ni wazee wale wa ----
Na hali ikizidi kuendelea kama nchi itakuwa sehemu mbaya sana

Ova
 
Kama una gundu la bundi, siku mbili nyuma kabla ya kukatwa kichwa umewasiliana nae, na ukamuwashia moto, but hauhusiki na kifo chake, mara police wanatrace namba wanaikuta na yako iko juu juu current call...uwiii unaenda kuminywa mbupuu!
Na huu ndo ubaya wa vyombo vyetu vya usalama, unaweza kutana na rafiki yako leo, usiku likatokea tukio huko aliko na mishe zake labda kavamiwa na kuuawa, ukawa na wewe ni mingoni mwa watuhumiwa kisa tu ulikuwa wa mwisho kumpigia simu ukimuuliza kama yupo nyumbani.
 
Na hiyo watu kutokuwa na imani na polisi,ina wapa njia watenda maovu,maana wanajuwa tukifanya tukio la kumteka mtu au kuua
Raia mtu wa kwanza kumhisi ni wazee wale wa ----
Na hali ikizidi kuendelea kama nchi itakuwa sehemu mbaya sana

Ova
Wa kulaumiwa ni hao hao polisi.
 
Aiseee inasikitisha sana.

Mimi nahisi itakuwa issue za Mapenzi ndiyo navyoona katika ulimwengu wa jicho la tatu.

Navyoona ni kwamba James Temba alikuwa anagonga Demu ila huyo Demu ana msela wake ambaye ndiyo anamuhudumia ,sasa baada ya msela kustukia akaona amtafute James Temba na kummaliza MAZIMA.
Sasa kama ni mapenzi, hawa wengine wameingiaje? Just najiuliza tu

Binafsi nadhani ni mambo ya hela, itakuwa kawapiga hela wakaungana na kuamua kummaliza!
 
Na huu ndo ubaya wa vyombo vyetu vya usalama, unaweza kutana na rafiki yako leo, usiku likatokea tukio huko aliko na mishe zake labda kavamiwa na kuuawa, ukawa na wewe ni mingoni mwa watuhumiwa kisa tu ulikuwa wa mwisho kumpigia simu ukimuuliza kama yupo nyumbani.
Exactly mkuu...too bad 😞
 
Jicho langu la tatu ambalo naliamini kwa zaidi ya 95% inaniambia kwamba hapo ni issue ya Mapenzi na wala si Uwinga wa Simu Kariakoo.

Jicho langu la tatu linaniambia James alikuwa na Demu ila huyo Demu alikuwa na mtu wake(Msela) ,nahisi msela ndiyo kaamua amalizane naye.

Ngoja tuone polisi wataconclude vipi ila hao vijana waliokamatwa wasiwe wameangushiwa tu jumba Bovu maana Polisi wetu huwa kukiwa na tukio lililoHIT wanafanya FUTUHI kutuliza watu.
Na kibaya zaidi bongo ukituhumiwa just tuhuma tu, watu wana conclude we ndo muuaji!
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na uchunguzi wa tukio la mauaji ya kikatili ya mwanafunzi wa Chuo cha IFM, James Rogers Temba, ambaye mwili wake ulikutwa ukielea kwenye maji ya Mto Msimbazi, eneo la Kipawa Ilala ukiwa hauna kichwa, Aprili 30, 2026.

Polisi tayari imewakamata watuhumiwa wanne kuhusiana na tukio hilo, akiwemo Steven Rogers Chaka (31), mkazi wa Bomang’ombe mkoani Kilimanjaro na Afisa Maabara; Anna Frank Lema maarufu kama “Happines” (30), mfanyabiashara mkazi wa Tabata Chang’ombe; Twalibu Khamis maarufu “Mputo” (23) pamoja na Michael John maarufu “Tambali” (26), wote wakazi wa Kigogo Kati.
Pole sana kwa kijana james temba

NB. KUHUSU KIFO CHA DOGO NAPATA NADHALIA TATU TATA.

Na hakika nadharia zangu tatu lazima moja itakua ndio sababu.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na uchunguzi wa tukio la mauaji ya kikatili ya mwanafunzi wa Chuo cha IFM, James Rogers Temba, ambaye mwili wake ulikutwa ukielea kwenye maji ya Mto Msimbazi, eneo la Kipawa Ilala ukiwa hauna kichwa, Aprili 30, 2026.

Polisi tayari imewakamata watuhumiwa wanne kuhusiana na tukio hilo, akiwemo Steven Rogers Chaka (31), mkazi wa Bomang’ombe mkoani Kilimanjaro na Afisa Maabara; Anna Frank Lema maarufu kama “Happines” (30), mfanyabiashara mkazi wa Tabata Chang’ombe; Twalibu Khamis maarufu “Mputo” (23) pamoja na Michael John maarufu “Tambali” (26), wote wakazi wa Kigogo Kati.
Kama ni watuhumiwa wa kweli na siyo kubambikwa kupoteza maboya, tunataka waoneshe kichwa walipokipeleka.

Isije ikawa ni ishu
ya kushusha munkali ya jamii huku watuhumiwa og wakitokomea kusikojulikana.
 
Kazi nzuri polisi..
Usijifariji mapema na kutoa sifa

Kuna mtu yawezekana kati yao alikuwa anagongewa ila limemkuta kwakuwa walimwengu wamepima maumivu yake na tukio na wametoa ushirikiano

NB: Ni jambo jema kufatilia hili lakini kama vyombo vya usalama kwa heshima zote🙏

Mbaki jinsi mlivyo
 
Back
Top Bottom